Monday, December 30, 2013

VITA KATIKA KUSAMEHE!!!


Kusamehe mtu aliyekukosea ni moja ya mambo magumu ya KIIMANI ambayo LAZIMA uweze kama unataka KUMUONA Mungu katika maisha yako.

Sababu na faida za kusamehe ni nyingi lakini nitataja chache. 1. Tunasamehe watu waliotukosea ili na sisi tusamehewe DHAMBI (madeni yetu) na Mungu. Katika sala ya Bwana kuna sehemu tunamwambia Mungu “utusamehe dhambi (deni) zetu kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea (wanaotudai). [nitarudi kueleza habari ya deni hapo baadae]. 2. Dhambi zina NGUVU ya kuficha uso wa Mungu usiuone, KUZIBA sikio lake ASIKUSIKIE na kuzuia Mkono wake USIKUOKOE. Nabii Isaya anasema hivi “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.” (Isaya 59:1,2).

Kumbuka KIPIMO ya KUSAMEHEWA dhambi na madeni yako kwa Mungu UNAJIPIMIA mwenyewe kwa JINSI unavyowasamehe wengine. Na hii unamwambia/unamwomba Mungu katika sala ya Bwana kila unaposali. Kwa lugha nyingina UNAMSIHI Mungu “USINISAMEHE kama jinsi ambavyo SIWASAMEHI watu walionikosea!”. Sasa, kwanini tunasema kwamba KUSAMEHE ni VITA? Kwa sababu anayetaka USISAMEHE sio wewe ila ni IBILISI! Mtu ataniuliza nimejuaje? Angalia hapo juu Isaya anasemaje: kwanza, “ili Ibilisi afanikiwe KUKUZUIA wewe kuuona USO wa Mungu anahakikisha una DHAMBI!”, pili, “ili Mkono wa Mungu USIKUFIKILIE na kukuokoa katika SHIDA, KILIO, na MAUMIVU yako, anakufarakanisha na Mungu kwa kuweka WINGU la uovu kati yako na Mungu na KUZUIA SIKIO lake kukusikiliza”! Mungu anasema “SITAKI kusikia” maombi yako. Ibilisi anachunga sana hii SIRI ili usije ukaondoa UOVU na DHAMBI zako maana ukifanikiwa kuondoa UOVU katikati yako MKONO wa Mungu utadhihirika katika maisha yako katika mambo YOTE na utakua UMEMSHINDA Ibilisi. Sikiliza, Mungu “hulitizama Neno lake na kulitimiza”. Usije ukasema Ibilisi kamdhibiti Mungu! Haiwezekani, ila Mungu ndio kasema HUTANIONA, SITAKUSIKIA na MKONO WANGU HAUTAKUAOKOA, kama kuna UOVU katikati yako! Na Ibilisi analikamata hilo Neno na kulitumia kukutesa. [kama ulikua hujui Ibilisi ni mtendaji wa Neno kuliko watu wengi sana japo huwa analitumia kinyumenyume, na kupambana naye ni LAZIMA ujue Neno na kulitumia kama silaha yako ya VITA. Bila Neno, wewe ni mawindo rahisi ya Ibilisi]

(Yeremia 29: 11-13) “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho. Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza. Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.” Madhara ya kukaa na DHAMBI ni MENGI kuliko unavyoweza kufikiri. 1. Unajikuta unapoteza MATUMAINI (future hope). Huko mbele kwenye maisha yako unaanza kuona giza na kukata tama maana bila sababu, matumaini yanapotea ndani yako! Hii ni kazi ya Ibilisi. Kama unaona unaanza kupoteza matumaini na huko mbele ya maisha yako unaona hakuvutii usihangaike, saka WATU wa kusamehe maishani mwako! Ondoa UOVU katikati yako! Ukiwasamahe “wote” hii hali inakwisha kwa maana MATUMAINI ya mambo MAZURI ni ahadi ya MUNGU wa watu wake na Ibilisi anataka kuinyakua kutoka kwako kwa KUTOSAMEHE. Kama kuna kitu unahitaji ni MATUMAINI, hii ni nguvu ya ajabu sana inayokupa nguvu ya kusonga mbele hata kama uko katika majaribu mazito. “Abrahamu alipoiona ile ahadi…”, “Yesu alipoona huko mbele ya msalaba kuna nini….alishinda msalaba na maumivu yake yote”. Lazima uone MBELE/future na huwezi kuona kama huna MATUMAINI na Ibilisi anakuondolea MATUMAINI ili uzidi kushindwa katika VITA naye. Kitu anachotumia kukuwekea WINGU hili la kutokuona mbele ni nini? Jibu ni UOVU katikati yako! 2. Katika shida na mahitaji yetu mbali mbali huwa tunamwita Mungu. Naye anasema “mtakwenda KUNIITA na KUNIOMBA nami NITAWASIKILIZA, MTANITAFUTA na KUNIONA ila kwa BIDII”. Bidii inatakiwa kwa sababu gani? Ni VITA, Ibilisi hataki UITE na Mungu asikie, wala hataki UKIOMBA na KUMTAFUTA Mungu umuone. Sasa kwa kuwa hawezi KUMZUIA Mungu, anakuja kukudhibiti wewe kwa kuhakikisha UNASHINDWA kusamehe watu waliokukosea! Matokeo yake ni KUZUIA majibu ya maombi yako!

Mtu atauliza kwani Ibilisi anaweza kuzuia majibu ya maombi kutoka kwa Mungu? Sikiliza, Wakati Danieli anaomba, Mungu anamtuma malaika Gabriel kumpasha habari kwamba hizi siku 21 alizokua busy anaomba ajue kwamba ALIJIBU “tangu” ulipoweka NIA ya KUOMBA, (sio wakati alipoanza kuomba) ila kuna VITA hapo juu na MAJIBU ya maombi yako yamezuiliwa, hivyo nimemtuma MIKAELI ashuke kupambana ili huyu MKUU wa giza hapo anayekamata majibu ya maombi yako aachilie! Sasa, ukifuatilia sehemu nyingine utaona Danieli aliomba na alianza kwa “toba” kwanini? Ili kusafisha NJIA ya kupokea Majibu. Ndio maana tunafundishwa kwamba “kila tusimamapo kusali sameheni”! Ayubu alijua SIRI hii pia, sio kwamba alitubu kwa ajili yake tu, alitubu hata kwa ajili ya watoto wake, “isije ikawa wamemkosea Mungu mahali”, (isije ikawa…maana yake anatubu hata kama hajui dhambi iliyofanyika! Kama ipo au haipo, yeye anatubu tu na KUACHILIA). Sasa watu wengi sana wamekwama na wameteseka na kila namna ya SHIDA na MAUMIVU mengi kwa sababu WAMESHINDWA kusamehe. Sasa, hebu chukua MUDA kidogo wa kutafakari ile LIST ya mambo uliyoomba na unayotarajia Mungu kukujibu na mengine unakiri umepokea. Kisha kumbuka WATU uliogoma kuwasamehe na ulinganishe FAIDA ya kumsamehe “huyu mtu” na HASARA utakayopata kama ile LIST yako ya maombi HAIJIBWI na Mungu. Pima mwenyewe na chukua hatua. Ukiamua kusikiliza uongo wa shetani ni juu yako, Mungu analeta hili Neno AKUOKOE na KUKUHUDUMIA.

Ngoja nikwambie kitu shetani anafanya hadi unashindwa kusamehe halafu ntakwambia cha kufanya. 1. Ibilisi anajua DHAMBI zako kwa maana yeye ndio amekusababisha UFANYE au amesamabisha watu WAKUKOSEE. Kwahiyo anajua ni wapi ameweka KUFULI ya kukutesa. Ili kuimarisha ile kufuli ikamate sawasawa, unapomwaza “yule mtu” aliye kukosea ghafla unasikia HASIRA au UCHUNGU, halafu analeta VIDEO na PICHA hata na SAUTI ya “yale mambo” ili KUHUISHA ule UCHUNGU na HASIRA ndani yako. Na hii inatokea mara nyingi na UNASHINDWA kumsamehe “huyu mtu” aliyekukosea. 2. Ibilisi anakupa SABABU na VISINGIZIO vya kutokusamehe. Utasikia mtu anasema ndani ya moyo wake au kwa kinywa, “kama kweli uliamua kunisaliti wakati nipo mimi nimekukosea nini?”, “yaani pamoja na kujitahidi kufanya haya yote umeamua kunifanyia hivi?”, nk. Ukisikia SAUTI hizi ndani yako jua ni IBILISI anakuhubiria injili MFU ili ushindwe kusamehe na afanikiwe kukutenga na USO, SIKIO na MKONO wa Mungu na ukose MSAADA wa Mungu. 3. Dhambi inasema! Kila ukisimama kuomba au ukijitahidi kusimama katika BWANA unasikia “sauti ya dhambi” ikipiga kelele moyoni mwako kukuvunja UJASIRI. Kwa lugha nyingine naiita “deni ya dhambi” (guilty)! Kama umewahi kua na deni mtu anakudai na anakusumbua utaelewa nasema nini. Kila ukikumbuka lile deni ni kama “linasema” na wewe huko ndani ya moyo wako kwa sauti! Hii ni vita ya Ibilisi na HUWEZI kuzima hiyo sauti bila MSAADA wa Mungu na Damu ya Yesu. Ndio maana utasikia “kikaribieni kiti cha Rehema kwa UJASIRI kwa Damu ya Yesu”, huu ujasiri unapatikana kwa DAMU ya Yesu.

Kwa sababu MAMBO yako MAZURI na Majibu ya maombi yako kwa WATOTO, KAZI, BIASHARA, nk, yamedhibitiwa na KUTOKUSAMEHE kwako, jua IMEKUPASA kusamehe kwa FAIDA yako KWANZA na sio ya aliyekukosea. Tena, kama unataka uwepo wa Mungu ukutembelee na kukufunika kila wakati na MKONO wake kua pamoja na wewe na USIPUNGUE katika maisha yako ni LAZIMA uondoe UOVU katikati yako. Kumuona Mungu maana yake ni “kumuona akikupigania na adui zako wakishindwa huku na huku na wewe ukiwa mshindi BILA sababu”! Hii lugha ni ngumu lakini sikiliza, Mungu anasema kwa kinywa cha DAUDI kwamba “hii nchi hamkumiliki kwa sababu ya upanga wenu wala mkuki, (sio nguvu zenu, au hamkufanya chochote) ila ni nuru ya uso wangu umewaangazia” sasa kumbuka DHAMBI zako zinaficha USO wa Mungu usiuone! Kwa lugha nyingine pamoja na KUPAMBANA sana na UPANGA wako bado ni NGUMU, ila Yule aliyeondoa UOVU katikati yake nakwambia HATASHINDA kwa upanga, Mungu anatangulia mbele zake na kumpa ushindi bure! Mungu anasema “kabla ya kuomba mimi Bwana nitajibu, na mkiwa katika kunena Nitasikia”. Mungu anamwambia Danieli, “ulipotia tu nia mimi nilijibu” Sasa iweje leo watu wanafunga na kuomba na INAKWAMA? Ondoa UOVU na DHAMBI katikati yako! Sio tu kwa KUTUBU dhambi zako ILA na KUWASAMEHE walio kukosea hata kama ni NGUMU. Kumbuka kwa NJIA mbili zote kwa pamoja 1. Tubu (na geuka) na acha dhambi 2. Samehe dhambi zote watu walizokutendea. HAKIKA utamwona Mungu maishani mwako kwa namna hujawahi kutarajia.

Kwanini unapata ujasiri wa kutenda dhambi? Hii ni SIRI nyingine nataka nikupe kabla ya kumalizia kukupa DAWA ya kupona. Kufanya dhambi inahitaji ujasiri wa aina yake. Umewahi kufikiri mtu anachukua KISU anamchoma mwenzake? Bila ujasiri huwezi. Au umewahi kufikiri mtu mzima anavua NGUO zake mbele za mtu mwingine wa JINSIA tofauti na anazini? Kwa kweli inahitaji ujasiri na huu unaupata kwa Ibilisi. Sasa kabla ya kufanya “hii dhmbi” lazima akupe ujasiri. Utasikia ndani yako “kama huyu jamaa hanijali basi na mimi nafanya ngono na huyu mwingine kwa sababu angalau yeye ananijali”, “kama kila mtu anakula rushwa kwani nini na mimi nisichukue hiki kidogo tu?”, “kama amenirusha hela yangu na mimi simpi msaada”, “kama Fulani alianguka katika uzinzi na yuko kanisani mi naona hii ni ngumu kwa hiyo watu wataelewa”, “watasema mchana na usiku watalala”, “hii ni ZAWADI sio rushwa”, nk., ghafla! unapata UJASIRI kwa kufanya KITU ambacho ni KIOVU ndani yako UKISHUHUDIWA kwamba UNAMKOSEA Mungu ila Ibilisi kashakujaza UJASIRI kwa hiyo unajikaza na KUFANYA. Sasa kumbuka ukifanya dhambi “moja”, madhara huwa yanakua zaidi ya moja! 1. Unauzuia Mkono wa Mungu kukuokoa, Uso wake usikuone, na Sikio lake lisikusikie 2. Unatengwa na Mungu, 3. Unazuia majibu ya mombia yako. Haya mambo matatu yanatokea kwa pamoja! Sasa kumbuka nimetaja matatu ila ni mlolongo wa mambo mengi sana uko hapo. Kwa sababu kuzuiliwa “majibu ya maombi” yako itawaathiri na wale waliokua wanapona kwa WEWE kuwaombea! Kwa maana ni majibu ya maombi YOTE yamedhibitiwa. Unaanza kushangaa watoto wako wanateseka na uko busy kuwaombea na hakuna kinatokea! kumbe kisa HUTAKI kumsamehe baba yao, nk!

Kumbuka siku zote, Ibilisi AKIKUSUKUMA kutenda dhambi sio ili UFAIDI, NO! ni ili akutenge na Mungu na apate nafasi ya KUKUANGAMIZA! Sasa, Neema ya Mungu hututetea (hasa tunapokua wajinga). LAKINI ukilijua Neno hili na ukaufanya moyo wako MGUMU, utaangamia! Kwa maana Mungu hulituma Neno kuwaponya mataifa lakini wasipolipokea Maangamizi hufuata, ila kabla ya HUKUMU lazima Neno litangulie. Unaweza kushangaa nasema nini, lakini ukisoma maandiko utaona Nuhu alihubiri kwa miaka takriban 100 akiwaambia watu watubu, na hawataki NDIPO gharika ikaja. Sememu nyingine tunasoma “aonywaye MARA NYINGI akishupaza shingo itavunjika na dawa hapati”. Hii ina maana KABLA ya shingo kuvunjika Mungu anakuletea Neno MARA NYINGI kukuonya na ukikataa KUTII basi Ibilisi anakumaliza. Sehemu nyingine tunaambiwa kwamba Yesu atakuja kuhukumu Ulimwengu, lakini ni baada ya INJILI kuhubiriwa kwa KILA kiumbe! Ili aije sema mtu sikusikia. Hii ndio tunaita Neema! Ndani ya Neema kuna muda wa Mungu kukusubiri UTUBU, ukichezea huu muda na “kikombe kikijaa” Unaangamia! SIKIA SAUTI yake LEO na UFANYE maamuzi na KUGEUKA.

DAWA ya kupona ni KUZIUNGAMA (kutaja dhambi kwa majina yake) kwa Mungu DHAMBI zako na KUWATANGAZIA wale watu waliokukosea kwamba UMEWASAMEHE BURE! Sasa, sikiliza. Kuwatangazia watu MSAMAHA pia ni VITA, tena NGUMU sana kutokana na MAJERAHA uliyopata “ulipokosewa” na hawa watu. Ndio maana utakuta mtu ANALIA tu kila akikumbika MTESI wake, Jipe moyo, Mungu anaona MAUMIVU yako. Anza na KUMTANGAZIA huyo mtu msamahawa wake kwenye MAOMBI, kisha chukua hatua ya IMANI na kumtangazia masikioni kwamba “NIMEKUSAMEHE bure”! Na ukiona ile hali inarudi huku ndani, kimbilia magotini tena na MTANGAZIE na IBILISI kwamba hii dhambi haipo nimesamehe na Yesu kafuta kwa Damu yake. Sisitiza hili katika Maombi hadi usikie UHURU wa ndani. Ukivuka hapo ndio sasa kile kipengele ya KUSAMEHE na KUSAHAU kitaanza kuwa dhahiri kwako, la sivyo ni NGUMU kibinabadu asikudanganye mtu. Bila Mungu huwezi KUSAMEHE na KUSAHAU, tafuta msaada wa Mungu kushinda VITA ya KUSAMEHE.

Uwezo wa kusamehe mtu (tolerance) Kimungu ni ndefu hakuna awezaye kufikia. Yesu alisema 7x70 kwa siku. Tena ni mtu huyo huyo anarudia kukukosea na kuomba msamaha kwa SIKU! Unatakiwa kumsamehe, hata kama ANARUDIA makosa yale yale. Nakubaliana na wewe kwamba unaweza kukosewa mara “moja” ikawa kubwa kuliko “Elfu”! Sawa, ndio maana nasema ni VITA na unahitaji msaada ya YESU kushinda na UWEZE kusamehe maana madhara ya KUTOKUSAMEHE ni MAKUBWA kuliko unavyofikiri. Kumbuka, kama WEWE unatakiwa uwe na UWEZO wa kusamehe mara 490 kwa siku, Je! Yesu ANAWEZA kukusamehe wewe mara ngapi ukimkosea? Jifunze KUJISAMEHE na KUJIACHILIA mwenyewe maana kila dhambi ULIYOITUBU Yesu alifuta ghafla! Pale ulipoanza tu kutubu.

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na Upendo wake Mungu Baba Ukae nanyi tangu sasa na hata milele.

Frank Philip.

No comments:

Post a Comment