Showing posts with label Women. Show all posts
Showing posts with label Women. Show all posts

Thursday, December 26, 2013

NDOA YA YUSUFU NA MARIA!!!


Nimetamani sana tujifuze jambo katika ndoa ya Yusufu na Maria. Nimechukua mfano huu kama ndoa/uhusiano wowote wa mwanaume na mwanamke ambao lengo lake ni kuishi kama mke na mume.

Kuna mambo kadhaa najifunza kwa maisha ya binafsi ya Yusufu na Maria. Yusufu alikuwa mtu wa haki, mtu mwenye heshima yake na jina jema katika jamii iliyomzunguka. Aliukuwa na kazi yake ya useremala ambayo yamkini ilimwingizia kipato. Kwa upande mwingine hatuambiwi Maria alikuwa anajishughulisha na nini ila alikuwa BIKIRA, ikimaanisha alikuwa msichana aliyejitunza na kuishi maisha masafi. Hawa wawili walikuwa wachumba na walidumu katika UHUSIANO huo katika USAFI wote. Kuna mambo manne (4) nataka tuone hapa. (Luka 1)

i. Kipindi cha Giza

Wakati maisha yanaendelea, ghafla! Malaika analeta habari kwa Maria kwamba atapata mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu na atazaa mtoto wa kiume. Kwa Maria ilikuwa ni habari ngumu ila alikubali kama MTUMWA kwa Bwana wake kwa sababu alijua ni mapenzi ya Mungu. Sasa nisikilize vizuri, wakati Malaika Gabriel analeta habari kwa Maria kwamba AMEBARIKIWA, tena amebarikiwa kuliko wanawake wote, na kwamba mtoto atakayezaliwa atarithi kwenye kiti cha mfalme “Daudi”, Maria anasikai raha hadi anaenda kwa ndugu yake Elizabeth [mama yake Yohana mbatizaji], anamshangilia Mungu kwa wimbo na wanajazwa Roho Mtakatifu pale na Yohana naye anashangilia kwa kucheza akiwa huko tumboni kwa mama yake. Sasa nataka uone kitu ambacho mimi nakiona. Wakati Maria anaitwa AMEBARIKIWA kuliko wanawake wote, kwa Yusufu ilikuwa sio Baraka ila ni balaa tupu. Kwa maana binti aliyemwamini kabisa sasa ni mjamzito katika mazingira ambayo hayaelewi, wala hajawahi kusikia kitu cha sampuli hii kimetokea wapi (all was new experience), hakuna mahali pa kurejea (reference) na wala hakuna mtu anaweza kumshauri kwa maana katika ELIMU ya dunia wakati huo hakuna mahali kitu kama hicho kimeandikwa/kimetokea. Watu hawajui nini kinaendelea. [Angalizo: Sio kila jambo kwenye ndoa/uhusiano wako utapata mjuzi wa kukusaidia, jifunze kujipanga na Mungu kwa mambo ya ndoa yako]

Katika hali hii ya GIZA, Yusufu akaamua KUMWACHA Maria kwa siri! Hii ni hali ya kuchanganyikiwa ambayo wengi wanafika katika mazingira magumu katika mahusiano yao. Ghafla tu unaona hiki “kitu” ni kigumu na unaona hakuna njia tena na unajiambia “basi bwana kama ndio hivi basi mimi naacha” au “mimi nimefanya sehemu yangu ila mwenzangu amenisaliti, naachia ngazi”, au “kwani mimi ndio wa kwanza kuachika”, “kwa vile ameenda kupata mimba huko basi na mimi sioni tena haja ya kujitunza”, “kwanza nina kazi yangu na simtegemei, potelea mbali maisha yataendelea”, nk. Ni hali ya kukata tamaa. Hiki ni kipindi cha giza. Na mwili unataka kuleta majibu ya haraka (instant solutions), kukimbia na kupotelea mbali. Lakini Malaika anakuja kusema na Yusufu na kuugeuza Moyo wake. Sijui kama Yusufu alikuwa mwombaji ila tunaambiwa Mungu alisema naye, akasikia na KURUDISHA moyo nyuma. Usipo jifunza kukaa katika MAOMBI ni vigumu kuvuka hii ngazi. Hapa ni kipindi cha KUNGOJA maana unajisikia huku ndani kwamba BADO hujapata/hujafika mahali unataka. Kumbuka “wamngojao Bwana watapata NGUVU mpya”. Unahitaji Nguvu mpya kila siku kuvuka hapa. Utagundua ule “upendo wa zamani umepoa”, sasa unahitaji NGUVU mpya. Muombe Mungu akupe nguvu mpya.

ii. Kutembea katika Baraka

Mara nyingi watu wamefikiria Baraka za Mungu kwa upande mmoja tu wa kuwa na hela, majumba, magari au kufanikiwa katika mambo ya mwilini na kusahau upande mwingine. Utasikia watu wanasema “count your blessings” (“hesabu Baraka zako”). Sasa unajua huwezi kuhesabu KITU ambacho hukijui na wala hukioni. Nakwambia Leo kuna Baraka nyingi sana Mungu anatubariki na hatuwezi kuziona wala kuzihesabu kwa maana ziko kwa jinsi ya ROHONI na kwa sababu huzioni hujui kwamba UMEBARIKIWA na unabaki ukilalamika na kunung’unika kwa sababu ulishamwekea Mungu vigezo na vitu fulani kwamba “hiki kisipotokea basi sijabarikiwa bado”. Kama mambo yako “hivi” basi bado hakijaeleweka, nk. Maria alichukuwa tu kama Malaika alivyosema na “akayatia moyoni mwake” huku akijua kwamba AMEBARIKIWA kuliko wanawake wote. Kwanini aliweka moyoni mwake? Kwa maana hakuna mtu wa kawaida anaweza kuelewa hii lugha ya kupata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Akajua ni Mungu na hakuna haja ya kutoa maelezo ya ziada au kuuliza watu au kupeleka umbea. Akakaa mimya.

Hebu mfikirie Yusufu. Wakati anajua kabisa hii mimba sio yangu ila anamhudumia Maria. Wanaenda huko mbali mji mwingine kuhesabiwa na mama hajiwezi mimba ni kubwa. Yamkini huko njiani Yusufu alitembea kwa mguu wakati mkewe mjamzito yuko juu ya punda na yeye anakokota huku mbele, ila mimba sio yake! Yule mama anajifungua hapo, Yusufu anamsaidia, ila mimba sio yake! Ni mambo magumu kuelewa ila Yusufu alikaza USO kufanya MAPENZI ya Mungu kama Malaika alivyosema. Hapo hampendezi Maria, ila Mungu, kwa maana yeye alichagua kitu cha kumfanyia Maria tayari, yaani KUMWACHA kwa SIRI! Sasa huu mpango wa kubaki ni mpango mpya ambao anaambiwa na Malaika na anaamua kuutimiza mpango huu japo haelewi vizuri. Mimba sio yake! Na sio hivyo tu, hajawahi kumgusa kabisa huyu mama! Analea mimba miezi 9, akijua kabisa sio yeye!

Kumbuka sio kila kitu Mungu atafanya juu ya maisha yako UTAELEWA. Baraka nyingi sana tunapata sio BINAFSI. Mungu amelenga KUWABARIKI wengi kupitia BARAKA alizokupa. Katika kubariki wengi LAZIMA kuna UDHIA. Ndio maana Yesu alisema “hakuna mtu aliyeacha ndugu, wazazi, shamba, nk. na kumfuata asipate hivyo “vitu” mara 100 hapa duniani ila na UDHIA pia”. Watu wengi sana wanapenda BARAKA ila BINAFSI, wanasahau kwamba Mungu akishusha Baraka mara nyingi sana hulenga wengi sana kwa Baraka hiyo hiyo, na imekuwa udhia. Kwa maana sio UPENDAVYO wewe ila sasa ni kama WAPENDAVYO wengine pia kupitia Baraka hiyo hiyo. Hebu fikiri wewe ni Maria (mama wa Yesu), unaitwa MBARIKIWA kuliko wanawake wote, ila kijana hakai nyumbani, anapita mitaani KUHUBIRI vitu hata huelewi, ukimuuliza anasema anafanya MAPENZI ya Baba yake! Huku Yusufu naye haelewi pia. Ghafla! Watu wanajaa kila mahali hata hakuna muda wa kula na kuongea kama familia! Huwezi tena kusema huyu ni MWANANGU kwa maana hata yeye anasema “hawa wa hekaluni ndio mama na ndugu zangu”. Kijana anasema lugha ngumu-ngumu tu kila saa! Huku mtaani wanasema kachanganyikiwa (karukwa na akili) na wengine wanasema kijana ana pepo! Hebu fikiri hii ndio ile kitu Mungu anasema ni BARAKA!

iii. Machozi kwenye Baraka Yako

Bila shaka Maria na Yusufu walikuwa na vipindi vigumu na Yesu, japo waliitwa WABARIKIWA. Ghafla wanaambiwa wahame nchi kwa maana Herode anataka kumuua mtoto! Wanakimbilia Misri, sijui walikuwa na usafiri gani ila najua haikuwa rahisi. Hebu fikiri ghafla! unajikuta unaanza kupiga mahesabu ya kuacha kazi yako kama Yusufu kwa sababu ya hii BARAKA iliyokuja kwenye familia. Hebu fikiri wale wateja wake ambao alikuwa anawatengenezea furniture, anawaagaje? Hebu fikiri wale ndugu zake sasa hapo mtaani anawaagaje? Eti, anahama nchi! Maana sio tu hawamwelewi, ila wanamwona kachanganyikiwa pia. Hii ni BARAKA imeingia katika familia na watu wanaanza kuhangaika. Sasa ukifika mahali pa kukata tamaa jua UNAHARIBU ile Baraka ya Mungu kwa maana sasa inakuja kwa MTINDO ambao haujautarajia. Nakwambia kila mtu atakuelewa ukiamua kuitupilia mbali hiyo BARAKA isipokuwa Mungu. Lakini nakwambia ni aheri KILA mtu asikuelewe ila Mungu akuelewe inapofika kufanya MAPENZI yake.

Ndoa nyingi sana ni BARAKA katika maisha ya watu na pia Mungu amelenga hizi ndoa ziweze kuwa BARAKA kwa watu wengine. Utakuta hapo katikati kumetokea MAMBO magumu na watu wamesamabaratika na KUTOKA nje ya kusudi la Mungu. Sawa watu watakuelewe kwa maana kwa kweli “huyu jamaa” amekuwa kama kichaa kabisa, ila kusudi la Mungu ni nini? Nakwambia kuna BARAKA ambayo Mungu alitarajia watu wengine waipate kupitia NDOA yako ila sasa Ibilisi ameisambaratisha na amefuta BARAKA kubwa ambayo wengi wangeipata kupitia NDOA yako! Sio kila KUACHANA ni suluhisho hata kama mazingira yote ya KISHERIA na KIJAMII yamekaa sawasawa na kila mtu anakuunga mkono. Kumbuka Yusufu angeweza kumwacha Maria mapema tu akiwa kama mtu wa HAKI, ila alikaza uso kutimiza Mapenzi ya Mungu. Je! Unajua mapenzi ya Mungu kwa NDOA yako? Je! Kila mmoja anajua WITO wake na mlichoitiwa kufanya shambani mwa Bwana? LAZIMA kipo. Hebu fikiri hii MISUKOSUKO yote ya NDOA ya Yusufu na Maria halafu hawajui WITO wao ingekuaje? Mkijua kila mmoja alichoitiwa mtapona kwa urahisi zaidi katika VITA vya adui.

iv. Mahali pa Ushindi

Wakati Maria na Yusufu wanapita nyakati mbalimbali ngumu na BARAKA ya mtoto Yesu, inafika takriban miaka 30 ambapo sasa KIJANA anakomaa kuwa mtu mzima. Mara kijana anakuja na agenda za KUFA kwa ajili ya ULIMWENGU! Maria haelewi wakati kijana anasema “mkila mwili wangu na kunywa damu yangu mnauzima wa milele”! Pamoja na kupita hivi vipindi vizito sasa kijana anataka KUFA! Eti yeye ni kondoo wa SADAKA. Matarajio ya Maria alijua siku moja yeye atakuwa mama wa MFALME, mtu tajiri mtaani na watu wote, wakubwa kwa wadogo wanamwamkia na kumheshimu. Maria anapiga picha ya KIONGOZI mkubwa kwa jinsi ya mwili lakini KIJANA anakuja na AGENDA za kusulubiwa sasa. Yamkini nguvu ya kushinda mambo yote magumu ilikuwa kwenye matumaini kwamba SIKU MOJA huyu kijana atakuwa mfalme kwenye kiti cha Mfalme Daudi na hapa nitapumzika. Mambo yanakuja kinyume na matarajio yake japo anajua kuwa AMEBARIKIWA. Huyu mama anafuata kila hatua, anaona kijana anakamatwa, anapelekwa Golgotha kusulubiwa kama MHALIFU. Hebu fikiri hapo. Mama anamjua mwanae vizuri sana. Anajua ni mcha Mungu leo ghafla tu anasingiziwa vitu VIGUMU na sasa wamempiga vibaya damu inatiririka kila mahali na wanampeleka kumgongomelea MASALABANI. Mama analia Yesu anasema “USINILILIE mama, jililieni wenyewe!” Yesu alijua ili hii BARAKA ikamilike ni LAZIMA asulubiwe kwa maana yeye ni “Mwana-kondoo wa Mungu achukuaye dhambi za ulimwengu”. Hii ni Baraka kubwa ila haijakaa kwa namna watu wengi wataiona kama Baraka! Wengi wangelalamika na kuona ni BALAA kubwa kwenye familia! Kama unatarajia UZIMA wa Milele jifunze kusoma LUGHA za rohoni katika Baraka zako kwa maana nyingine zinakuja kwa mtindo ambao unaweza kukemea ukidhani ni Ibilisi au jaribu. (Luka 23)

Lengo la somo hili ni kutaka kukufungua macho juu ya mambo ambayo Mungu anafanya katika maisha yetu na tukumbuke kumshukuru hata kama hatuelewi kila kitu kwa maana “Mungu amekusudia mambo mema kwa ajili ya watoto wake kila siku”. Angalia usibebe roho ya KISASI kwa mambo yatakayokukuta katika MAHUSIANO kwa maana KILA uhusiano/ndoa itapita katika VIPINDI vigumu na vyepesi, vipindi vya huzuni na furaha, vicheko na vilio, nk. Angalia sana katika VIPINDI hivi usimkosee Mungu kwa sababu tu HUELEWEI mwenzako anafanya nini. Yamkini ameamua kukusaliti na wanawake/wanaume wengine na umejua. Kwa maana kama wewe ni mtu wa Mungu “hutakosa kuzijua HILA za Ibilisi na Mungu hatawaficha watu wake jambo”, na umefika mahali UMEJUA. Chunga USIMKOSEE Mungu kwa sababu mwenzako amemkosea Mungu. Uhusiano/NDOA ina mwisho ila uhusiano wako na Mungu hauna mwisho. Ukijua kwamba MATESO yako ni ya KITAMBO tu, usikubali KUPOTEZA hatma yako (mambo ya milele) kwa sababu ya mambo ya kitambo tu. Kaza uso wako kwa Mungu na kaa katika KUSUDI lake na WITO ulioitiwa ili ile BARAKA Mungu aliyoweka katika maisha yako ISIPOTELEE njiani. Tafakari yaliyo juu aliko Kristo kwa maana huku Duniani kuna ufisadi mwingi. Angalia MWISHO wa safari yako na ujitie moyo katika Bwana. Mambo yanayotokea kwenye uhusiano wako yasiujaze moyo wako hata ukakosa shukrani kwa Mungu wako.

Neema na Rehema zitokazo juu ziwahifadhi NIA zetu tangu sasa na hata milele. Bwana yu karibu.

Frank Philip.

Wednesday, March 27, 2013

USIONEKANE TU MZURI KWA MBALI LAKINI UZURI UKO MBALI NA WEWE(01)

Shalom!

Nawasalimia wasomaji wote kwa Jina la Yesu Kristo, Bwana na mwokozi Yesu Kristo!

Natumai mko vema na mnaendelea vema, kuna mengi sana ya kuzungumza katika misingi hii ya Injili bora na leo nimesukumwa kuongea na wadada na wanawake jambo moja la muhimu kweli,lizingatieni hili litawasaidia mno.

Mungu alipokuumba mwanamke wala hakukosea,alikuumba kwa kusudi maalum na ana mpango kamili na maisha yako.
kila alichokiumba Mungu ni kizuri ingawa binadamu huona tofauti,maana wanadamu wametafsiri uzuri kama mapendezo ya macho sawasawa na tafsiri kichwa cha mwenye macho!
Mungu amewaumba wasichana na wanawake kwa namna ya kipekee na uzuri wa ajabu, ndio hata kama watu hawatasema lakini kuna uzuri upo unaowafanya muwe mapambo ya Dunia!

Mungu amemuumba mwanadamu kwa hatua,naama kila kiumbe pia hupitia hatua fulani katika kiushi kwake....mwanadamu huwa na maisha ndani ya wazazi na kisha kuzaliwa>huwa mtoto>hukua na kuanza kutembea na kufanya mengi>na muda ukifika hupevuka na hapa ndio mtu huwa mrembo na mzuri sana,kisha kuna kipindi chwa mwanzo cha ujana,ujana huja na hatimaye utu uzima na kisha uzee kabla ya kupumzika katika maisha haya ya ulimwengu!!

Kila hatua Mungu aliyoiumba ina raha na manufaa yake kwa kila kiumbe na kwa kuwa hapa nazungumza na wadada na wanawake, nataka nisistize kuwa kila hatua ya kukua kwenu ina maana sana katika maisha yenu na kwa Mungu pia! imekupasa kujifunza vema kutumia muda vizuri na kufurahia kwa kina kila hatua ya maisha yako.
ukiwa na ule usichana mdogo imekupasa kucheza michezo yote ya rika hilo na unapopevuka basi fanya yale maadili yote yakupasayo,maana nawaona watu wengi hufanya makosa sana na baadae kufanya mabo ya kitoto wakiwa watu wazima!


Mungu amekuumbia mpango maalum wa maisha ya baadae,kama hujaamua kuifuata njia ua utawa,maana yake unahitaji kuwa na familia bora,lakini hiyo familia bora haipatikani kwa nadharia bali kwa kujiandaa vema,katika ndoa mna ndio maana kila mahali biblia husema...mke mwema nani awezaye kumuona?

Nimeona wasichana wengi wa kipindi hiki wamekulia maisha ya kudeka na uvivu, kiasi cha mpaka nguo zao za ndani zinafuliwa na wasichana wa kazi au mashine,si ajabu kumuona binti mwenye miaka zaidi ya 20 hajui kupika wala kufanya kazi za nyumbani!

Si mbaya bado muda unao,kama kweli unataka kuolewa na kuwa na familia bora imekupasa kuanza kujiandaa sasa,kwa kujifunza yale yote yakupasayo kujua ili uwe mke mzuri na mama mwenye akili wa familia,zaidi unapaswa kujiandaa kisaikolojia,kiuchumi,kijamii na kiakili....kuna somo nimewahi kusikia mtumishi mmoja akifundisha na alisema;
.....UNTIL WHEN YOU ARE SINGLE,THEN YOU ARE REDY TO BE MARRIED!!!
na hapo kuwa single ina maanisha ukifika mahali unaweza kujitegemea na kujisimamia mwenyewe kimaamuzi,kimaisha,kiuchumi na kijamii,hapo ndipo unaweza ukamkaribisha mtu moyoni mwako ili awe mume wako!

kiini cha maada hii ni hiki,yamkini unajiona mzuri sana,na labda watu wengi wamekusifia hivyo na yamkini ndivyo ulivyo,na tangu umesifiwa na kusumbuliwa na vijana kadhaa kukutaka basi tena umekuwa na kiburi,madaha na nyodo za kutosha mrembo,na kwa kuwa una kazi nzuri labda na kagari basi tena umeona maisha yamefika mwisho,si mbaya siwezi kukulaumu labda ndivyo ulivyolelewa au ni ulimbukeni tu!

*******************************************************************************
lakini natamani utambue jambo moja uzuri wa msichana sio muonekano pekee bali na tabia, hivyo unaweza ukanga'ara sana kwa mbali lakini watu wakikukaribia hawatakaa watakimbia tu....jijengee heshima ya kipekee ambayo itawafanya watu wakuite dada hata kabla hujawakolomea
....."YOU LOOK GOOD FROM FAR BUT ON ACTUAL FACT YOU ARE VERY FAR FROM GOOD" (Unaonekana mzuri toka mbali lakini ukweli ni kuwa uko mbali na uzuri)
na yamkini sasa hivi hilo hulioni,jaribu tu basi kujitathmini na ujue watu wanakuonaje,itakuwa vizuri kama utaanza na marafiki wa karibu kabisa!
Uzuri na ubaya wa maisha ni huu,yaani hata kama wewe hujui kiasi gani bado ukweli utakuhukumu tu!
HONGERA SANA KWA KUWA MZURI,LAKINI JENGA TABIA YAKO.....A WOMAN IS NOTHING WITHOUT A CHARACTER!!!
......Your beauty might take you higher but what can make you remain there is character!!!!
Natamani kama ungenielewa,binafsi sipendi kabisa kuona wasichana warembo wanaangukia katika mikono ya waharibifu,wachafuaji,wafiraji na wasiojiheshimu eti kwa kutekwa na fedha na mali za wanaume hao ama kuwakomoa wale waliojisumbua kuwafuata!!!!
*******************************************************************************

Yamkini umekuwa ukiwajibu vibaya sana na kuwatesa wakaka au vijana wanaokutongoza kwa minajili ya kukuoa,sisemi uwakubali lakini unawajibuje? unajua hekina ni kitu kidogo sana lakini ndio msingi mkuu wa mafanikio!
YAWEZEKANA UNAJIDANGANYA SANA NA KIOO CHAKO CHA CHUMBANI NA UNADHANI UREMBO WAKO WA SASA UTADUMU, AU UNADHANI SASA UNA MUDA HIVYO UNAENDELEA KUWASUMBUA WAKAKA UKIAMINI KUWA WATAENDELEA KUJA TU....MMH NATAKA NIKWAMBIE MUDA WA UZURI NI MFUPI SANA,MUDA WA KUNG'ARA NA KUWAVUTIA WENGI NI WA KITAMBO TU,UKIONA MUDA HUO UMEPITA UTAPATA SHIDA SANA,MAANA UTATAMANI WAJE NA HATA WALE WALIOWAHI KUJA HUTAWAONA TENA NA HATA WALE WABAYA HAWATAKUJA,Hapo ndipo wengi hupata mishtuko na presha na kuamua tu kuolea na yeyote ilimradi na maisha hayo hayawezi kuwa mazuri hata kidogo,maana ni maamuzi ya ilimradi!!

NIMESHUHUDIA WASICANA NA WANAWAKE WENGI SANA AMBAO WARIRINGA WAKATI WA USICHANA WAO NA WAMEKUJA KUOLEWA NA 35,40 NA 45,TENA KWA KUJIOZESHA KWA VIJANA WADOGO AMA WAZEE WALIOFIWA NA WAKE ZAO NA WAKATI HUO HATA MAISHA HAWAYAFAIDI VIZURI.


Usijaribu kijiringanisha na wanaume maana wao hata umri ukienda bado wanaweza kuoa tu,tena wasichana wazuri wa kipindi hicho,hivyo acha maringo na madaha yasiyo na maana,acha kuwatesa vijana na achana na tabia ya kushindanisha wanaume kutokana na vitu walivyo navyo,ukimpata mtu anaekupenda kwa dhati tia baraka mfukoni kisha mshukuru Mungu, mali na vitu hupatikana tu na hasa kama wewe una akili njema vitakuja vingi sana tena sana!!

UKIWA KAMA MSICHANA UNAYO NAFASI NZURI YA KUFANYA VIZURI KATIKA MAISHA YAKO,USIKURUPUKE KUFANYA MAAMUZI,USIKIMBILIE VITU,USIPUPARIKIE MAISHA,JIFUNZE NA UJIPANGE KUAMUA NA HAKIKISHA UNAMUHUSISHA MUNGU 100%KATIKA MAAMUZI YAKO,NA MUHIMU UKUMBUKE KUWA UKIAMUA TU,HAYO NDIYO MAISHA YAKO!!!

#UNAWEZA UKARINGA NA KURUKARUKA UTAKAVYO LAKINI IKIFIKA SAA UTANASWA TU,SASA UKINASWA NA MTEGO NI MATESO YA MAISHA YAKO YOTE NA UKIANGUKIA KWA YULE AKUPENDAE BASI HIYO ITAKUWA PARADISO YAKO NDOGO HAPA DUNIANI!!!

natamani nimalizie andiko langu hili  kwa kusisitiza jambo hili
.....YOUTH IS GLORIOUS BUT IS NOT A CARRIER!!!

Na KING CHAVALA
+255 713 883 797

>>>>>>TO BE CONTINUED!!!!!!

Friday, December 14, 2012

TIPS>>Wife's Role In A Christian Marriage(1)

Crucial to any family's success is the wife's role in a Christian marriage
A good God-fearing woman is the glue that holds the family together. First and foremost a help "mate," or suitable for a husband, a godly wife is a woman of faith, virtue, intelligence and beauty. A virtuous woman is not ignorant or slothful, but an enterprising leader, using time, talent and abilities for the good of the family and community. The role she plays is also a pivotal one between the father and the children; and at times requires the gift of mediation to help facilitate communication and good will, especially with adolescents. A godly wife is a good steward over the family resources, shows kindness to the poor, and possesses such Christian qualities and character to bring honor to God and to a husband. Proverbs, Chapter 31 perfectly describes the wife's role in a Christian marriage: "Who can find a virtuous woman? for her price is far above rubies. The heart of her husband doth safely trust in her, so that he shall have no need of spoil. She will do him good and not evil all the days of her life" (Proverbs 31:1-12). 
A virtuous woman's goal, then, is to live life above reproach to win the husband's trust. The chaste conversation of a godly woman becomes an example of virtue, purity and holiness bringing honor to the husband.

Incorporated in the wife's role in a Christian marriage is not only the ability to properly manage the household, but primarily to minister to her own husband. A wife has the God-given power to make or break a man. By understanding a man's need for intimacy and acceptance, a godly wife can help the husband become all that God intended for him to be. Christian women need not be concerned about infidelity when the effort is made to love, honor, obey and cherish their mates. Keeping the home fires burning is part of a wife's role, and should not be a duty but a distinct pleasure. "Now concerning the things whereof ye wrote unto me: It is good for a man not to touch a woman. Nevertheless, to avoid fornication, let every man have his own wife, and let every woman have her own husband. Let the husband render unto the wife due benevolence: and likewise also the wife unto the husband. The wife hath not power of her own body, but the husband: and likewise also the husband hath not power of his own body, but the wife. Defraud ye not one the other, except it be with consent for a time, that ye may give yourselves to fasting and prayer; and come together again, that Satan tempt you not for your incontinency" (I Corinthians 7:1-5). 

As women of integrity, many females fulfill the wife's role in a Christian marriage not only by meeting the needs of the husband and family, but by also extending charity to the poor and performing good deeds. In so doing, the godly Christian wife brings honor to the husband, possibly a leader in the community or in the church. Part of good stewardship is tithing, giving a tenth to the Church; and offerings for the work of Christian ministry at home and abroad. The wife's role in a Christian marriage which extends beyond the homefront might include volunteering to deliver meals to the sick and shut in, helping the elderly, or accompanying the family on mission trips abroad. In any case, the godly married woman sees a need and makes a sincere effort to meet it whenever possible. 

Women married to ministers or laypersons should always live an exemplary life and not bring shame upon their husbands, but honor. Because of a lifestyle that is chaste, holy, and pure, the wife's role in a Christian marriage is a witness not only to the community at large but also to the family and spouse. Godly women lead by being an example of the believer in word and in deed. The wife's responsibility is to teach a daughter and other young women how to be a godly wives, while demonstrating to young men the proper way to earn respect and submit to the husband's authority. The wife's role in a Christian marriage includes teaching others by example. " But speak thou the things which become sound doctrine: That the aged men be sober, grave, temperate, sound in faith, in charity, in patience. The aged women likewise, that they be in behaviour as becometh holiness, not false accusers, not given to much wine, teachers of good things; That they may teach the young women to be sober, to love their husbands, to love their children, To be discreet, chaste, keepers at home, good, obedient to their own husbands, that the word of God be not blasphemed" 

(Titus 2:1-5). 

Lastly, the wife's role in a Christian marriage is to display Christ-like attributes and the fruit of the Spirit that emanate both natural and spiritual beauty, to the glory of God. The virtuous wife possesses love, joy, peace, longsuffering, gentleness, goodness, faith, meekness, and temperance. Because she fears, or reverences the Lord, the godly wife is able to excel in virtue above other women, so much so that works of honor, humility, and true holiness earn a reputation in the church and at home. "Let no man despise thy youth; but be thou an example of the believers, in word, in conversation, in charity, in spirit, in faith, in purity" (I Timothy 4:12).


TO BE CONTINUED.....!!!