Friday, December 13, 2013

KAZI YA UVUVI [UPDATED] !!!


Kazi ya UVUVI ni moja ya kazi ambazo zinahitaji uzoefu lakini pia Imani. Umewahi kujiuliza mvuvi anaposhusha nyavu zake huko chini kwenye maji ambapo haoni kitu ila anasubiri kwa IMANI akijua samaki wataingia?

Petro alipoambiwa anabadilishiwa kazi kutoka kuvua SAMAKI kwenda kuvua WATU ilikau inahitaji shule zaidi kidogo ili aelewe somo. Siku moja Petro akaenda kwa UZOEFU, kumbuka sio ZIWA/BAHARI au maeneo asiyoyajua, anajua sana na ana uzoefu nayo. Si akakesha sasa usiku kucha na hakupata kitu! Yesu akaja, akamwambia “Petro shusha nyavu” na akampa maelekezo ya ziada. Petro akajiuliza, “nimehangaika usiku kucha ila sikukamata kitu na sasa unasema nishushe nyavu?”, akapiga moyo konde na kusema, “kwa Neno lako nitashusha”. Hao samaki aliokamata hakuweza kuvuta nyavu maana ni wengi hadi nyavu kuchanika! Akasema “ondoka kwangu mimi mwenye dhambi”! Kwanini? [kufanya kazi ya Mungu bila mapenzi yake ni kosa na itakugharmu].


Sikiliza. Watumishi wengi sana wa Mungu wanahangaikal na KINA na UZOEFU wa nondo (mafundisho, nyenzo, nk.) wanazotumia na USTADI wa kupiga MAKASIA. Bila KUSUDI la Mungu utakesha hapo nakutahadharisha. Sio katika HUDUMA tu ila hata katika michakato ya maisha, biashara, nk. Hakikisha unashusha NYAVU mahali ambapo unajua YESU amekuongoza. Huwezi kosa SAMAKI asilani. Uzoefu wako na UJUAJI vitakuponza tafuta KUSUDI la Mungu katika maisha yako na utaona MATUNDA yakimimnika maishani mwako kama MVUA. Mafanikio ya Petro hayakutegemea KINA cha maji, AINA ya nyavu, MTUMBI, UREFU wa MUDA, wala UZOEFU wake! Ila NENO la Yesu! Ukipata Neno la wakati huo katika MUKTADHA (context) na MAUDHUI (content) na MUDA (timely), mafaniko yako katika HUDUMA, BIASHARA, KAZI, SHULE, nk., yatakua makubwa kuliko kujitahidi kwa NGUVU zako mwenyewe na AKILI zako. Jifunze kumshirikisha Yesu nawe utaona HATUA atakazokufikisha.

Kumbuka. Mungu hulituma Neno lake “kama mvua ishukavyo kutoka juu kuangukia ardhi”, na LITATIMIZA makusudi yake, halitarudi bure. Ukijua Yesu anasema nini juu ya UVUVI wako, sema kama Petro “kwa Neno lako nitashusha nyavu” halafu tukikutana utanipa ushuhuda. Barikiwa.

Frank Philip

No comments:

Post a Comment