Showing posts with label Gospel Music. Show all posts
Showing posts with label Gospel Music. Show all posts

Tuesday, April 22, 2014

KEKE NA AYO WATIA FORA TAMASHA LA PASAKA 2014!!!


Sikukuu ya pasaka ya mwaka huu ilikuwa na mwimbaji mahiri toka Afrika kusini, ali maarufu kama Keke, huyu mbaba ni mwimbaji na mwabuduji mzuri tu na ni mchungaji pia
Katika tamasha hilo la pasaka ambalo huandaliwa na Msama Promotion pamoja na Changamoto ya mvua bado muitikio wa watu ulikuwa mzuri tu na waimbaji mbalimbali toka hapa nchini na nje  ya nchi walikuwepo kumtukuza huyo Kristo aliyefufuka


Miongoni mwa wanamuziki waliohudumu katika tamasha hilo ni pamoja na Upendo Nkone, Upendo Kilahiro, Sara K kutoka Kenya, Glorious Worship Team, John Lisu, Jessica BM,Meccy Chengula,Edson Mwaisabwite,Masanja Mkandamizaji,Mwanamuziki kutoka UK na Keke Kutoka South Africa pamoja na Rose Muhando bila kumsahau Efraimu Sekeleti toka Zambia!

Mhe. Benard Membe ambaye alikuwa mgeni rasmi katika tamasha hilo kwa niaba ya Mh.rais Jakaya Mrisho Kikwete akisikiliza risala kutoka kwa Mchungaji Mwasota ambaye ni Mwenyekiti wa Makanisa ya Pentekoste Ukanda wa Dar-es-Salaam na baadaye kutoa hutuba fupi akiweka msisitizo wa Mchakato wa uundaji wa katiba mpya kuwa utakuwa wa amani tu na wananchi wasubiri kuipigia kura.

Keke mwanamuziki kutoka Africa Ya Kusini akihudumu katika Uwanja wa Taifa kwa makeke ya hali ya juu sana!


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Membe akiongea siku ya Jana kuhusu Mchakato wa Katiba Mpya 

Laura Msama Mke wa Msama akiwa amekunja goti wakati akisalimiana na Mhe. Membe 

Mhe. Membe akiwa anasalimiana na Keke, mwimbaji toka Afrika kusini.
 Mwanamuziki kutoka Zambia Ephrahim Sekeleti akiwa anapasha pamoja na Backers Vocalists wake, aliowaomba hapo uwanjani maana hawa ni Living Water toka Makuti kawe kwa Apostle Onesmo Ndegi!. 

Upendo Kilahiro akiwa anaenda sawa katika Uwanja wa Taifa 

Mise Anaeli akuwa anapuliza tarumbeta Uwanjani sambamba na Upendo kilahiro

Sarah K Mwanamuziki Kutoka Kenya akiwa anaimba Wimbo Wake "Liseme" akisaidiwa back up na wanamuziki wa Glorious worship team


"Kwani Ni Jambo Lipi hilo, Yeye asiloliweza" 
 Baadhi ya Waimbaji Wa Glorious Worship Team wakiwa Jukwaani wakienda sawa 

Kijana ni Kijana tu, Hawa hawakuwa mbali kwenda sawa na mishindo ya jukwaani!

Mwanamuziki Nguli kutoka Africa Ya Kusini Keke akiwa Jukwaani 



Backers Vocalists wakiwa wanaenda sawa 

Mpiga drums nambari moja wa Keke akiwa anaenda sawa 

Na mpaka hapo kwa uchache ndivyo tamasha la pasaka lilivyokuwa, Mwanamuziki wa mwisho alikuwa Rose Mhando na alikuja na vibao vyake vipya vya album yake mpya ya Facebook na kwa hakika alifanya vizuri!
Tamasha lilimalizika majira ya saa 2 usiku na hapo ndiyo ikawa mwisho na tutaonana tena Christmass ijayo na pasaka Mungu akipenda!
Naamini mambo haya yakifanyika katika dhamira ya kweli tupu tutafika mbali sana, Mungu awabariki watumishi wote watumikao madhabahuni kwa uaminifu!!

Thursday, February 13, 2014

WASANII "KUREJEA MADHABAHUNI" NDANI GOSPEL ARTISTS BREAKFAST!!! 22/02/2014

SHALOM!
Kwa mara nyingine tena Ikiwa ni ukurasa wa kwanza wa msimu wa pili na mara ya kwanza kwa 2014, Chavala Ideas Platform (Mahali yanapozaliwa mawazo mapya na makutano ya mawazo yanayotekelezeka) kupitia Wavuti ya Kikristo Gospel Standard Base wamekuandalia tena Staftahi maalum kwa ajili ya mwili wako na nyingine kubwa zaidi kwa ajili ya roho yako wewe ulipewa kipawa na unatumika madhabahuni kwa Bwana iitwayo "GOSPEL ARTISTS BREAKFAST"
Chai hii maalum kwa ajili ya waimbaji wa aina zote za nyimbo za injili,wachezaji,wapiga vyombo,wazalishaji,wasmbazaji,watangazaji,wachekeshaji,waigizaji na kila mwenye kipawa chake anachokitumia madhabahuni itanyweka pale WORDALIVE CENTRE-Sinza Mori, Jumamosi ya tarehe 22/02/2014 Kuanzaia saa 2 asubuhi mpaka 5:59 asubuhi!
Maada au msingi wa chai hii utakuwa ni juu ya wasanii wa injili "KUREJEA MADHABAHUNI" na Mchungaji na mwanamuziki wa siku nyungi Rev.DAVID NKONE atatuhudumia!

Hii sio fursa ya kukosa na sio kwa ajili ya mtu fulani tu maalum,bali ni kwa ajili ya kila anayemaanisha kutumika madhabahuni!
Hakuna Kiingilio na ukiwahi utafanya jambo la maana zaidi!!!

Chai hii inandaliwa na MODERN EVENTS CEREMONERZ
Kwa kusirikiana na WordAlive Centre na

Imedhaminiwa na
1.Great Potentials Ltd
(......Living your Dreams by your potential!!)
2Quality Vision Picture

(Quality vision pictures inafanya Gospel Videos.na sasa kwa watu  20 wa mwanzo kuna ofa maalumu kwa mawasiliano wafike officen Kimara. 0715416961,na 657295614)

NJOO UONGEZA MAARIFA,NJOO UCHANGAMOTISHWE NA NJOO UFAHAMIANE NA MARAFIKI WENGINE,NI MATUMAINI YANGU KUWA HAUTAKUJA PEKE YAKO!!!

0713 883 797

Sunday, December 22, 2013

KAMA UNATAKA MUNGU AONEKANE NA WATU JIFUNZE HII SIRI



Kipimo cha UDHIHIRISHO (MANIFESTATION) wa Mungu kwenye HADHIRA (PUBLIC) ni MUDA, BIDII na HALI ya MOYO wako UKIJIHUDHURISHA mbele Zake mkiwa wenyewe wewe na Mungu pekeyenu (SIRINI).

Kama UKIJIHUDHURISHA mbele za Mungu wako kwa BIDII na kwa UELEKEVU mahali pa SIRI, basi Mungu ATAJIDHIHIRISHA mbele ya WATU hadharani.

Ukitaka Mungu aji-present kwa watu basi jifunze kuji-present kwa Mungu.

Ni aheri ukose MUDA wa kuandaa PRESENTATION kwa watu na sio MUDA wa kuji-present kwa Mungu, kwa maana unaweza ku-present kitu chochote mbele za watu ILA HUWEZI kum-present Mungu! Ndio maana kazi ya Mitume ilikua KUHUBIRI na KAZI ya Mungu likua KULITHIBITISHA hilo Neno kwa ISHARA na MAAJABU.

Kazi ya Musa ilikua kuji-present kwa Mungu na kupata maelekezo na KAZI ya Mungu ilikua KUTENDA miujiza (kuji-present) mbele za Farao!

Frank Philip.

Wednesday, November 20, 2013

JUMAPILI HII HAPATATOSHA CCC-UPANGA KWA UJIO NA MOTO MPYA WA CHRISTINA SHUSHO!!!!!

KAMA HABARI HII HAIJAKUFIKIA BASI NAOMBA NIKUJUZE RASMI!
MWANAMAMA ANAYETAMBA NA MAHADHI YA KIPEKEE KATIKA MUZIKI WA INJILI TANZANIA NA AFRIKA MASHARIKI,IKIWA TU BAADA YA KUJINYAKULIA TUZO YA MWANAMUZIKI BORA WA INJILI AFRIKA UKANDA WA AFRIKA MASHARIKI KWA 2013,SASA ANAKUJA KIVINGINE,ANAKUJA UPYA,NDIO AMEAMUA KUHAMA KABISA TOKA KUIMBA KWA KUTUMIA CD MPAKA KUIMBA MOJA KWA MOJA......NI JUMAPILI HII NDANI YA UKUMBI WA CCC-UPANGA!
JUKWAANI ATAIMBA PAMOJA NA BAHATI BUKUKU,UPENDO KILAHIRO,JOSHUA MLELWA,AMANI KAPAMA,PAUL CLEMENT,THE VOICE ACAPELLA PAMOJA NA KINONDONI REVIVAL CHOIR!
MAJIRA YA SAA NANE GETI LITAKUWA WAZI NA SAA TISA TAMASHA LITAANZA RASMI,KAMA WEWE NI MGENI MAHALI HAPO BASI FIKA POSTA MPYA SAA NANE NA HAPO UTAPATA GARI MPAKA UKUMBINI KWA BEI YA KAWAIDA!
UTAKUWA SEHEMU YA HISTORIA HII KWA KUCHANGIA KWA KUNUNUA TIKETI TSH 10,000/= KAWAIDA,20,000/=VIP NA 3000/= KWA WATOTO!
NI VIZURI KUPATA TIKETI YAKO MAPEMA PALE SILVERSPOON-MLIMANICITY,MWENGE-PUMA KITUO CHA MAFUTA NA STEERS-POSTA,INGAWA HATA MLANGONI ZITAKUWEPO!
ZINGATIA KUWAHI,ZINGATIA KUWATAARIFU WENGINE NA KWA JAMBO LOLOTE LA ZIADA BASI USISITE KUWASILIANA KUPITIA
0713883 797 AU 0713 905 118

Tuesday, November 5, 2013

KWA MARA YA KWANZA "CHRISTINA SHUSHO" KUIMBA LIVE KATIKA TAMASHA LAKE LA "NATAKA NIMJUE" 24/11/2013 PALE CCC-UPANGA!!!!

Shalom Tanzania!
Baada ya kimya kirefu, mizunguko mingi ya ndani na nje ya nchi kihuduma, Hatimaye Mwanamama, Mtumishi, Mwimbaji alijinyakulia tuzo ya Uanamuziki bora wa nyimbo za injili Ukanda huu wa Afrika Mashariki, CHRISTINA SHUSHO, Sasa amekuja na jambo kubwa la kipee na hili ni TAMASHA LA KUSIFU NA KUMWABUDU MUNGU!
katika TAMASHA hili lililopewa jina "NATAKA NIMJUE", CHRISTINA SHUSHO ATAIMBA LIVE (BILA KUTUMIA CD) na atasindikizwa na Waimbaji kama
1.BAHATI BUKUKU
BAHATI BUKUKU

HUYU NI MWANAMUZIKI ANAYETAMBA NA ALBUM YAKE MPYA KWA SASA IITWAYO "DUNIA HAINA HURUMA"
2.UPENDO KILAHIRO
Pia Vijana wanaochipukia kwa sasa, hapa ninamzungumzia PAUL CLEMENT na mpiga DRUM maarufu mjini na mwimbaji AMANI KAPAMA
PAUL CLEMENT

AMANI KAPAMA
Mkongwe na Muasisi wa Live JOHN LISSU Ambaye amefanya LIVE RECORDING yake kipindi sio kirefu lilichopita mwaka huu!
CHRISTINA SHUSHO & JOHN LISSU

JAMBO KUBWA ZAIDI NI KUWA TAMASHA HILI LITAONGEZEWA VIONJO VYA kwaya ya KINONDONI REVIVAL, watu waliouvuma sana na ule wimbo wao wa "KWANINI UNATAKA KUJIUA?" pamoja vijana wa THE VOICE Acapella!
KINONDONI REVIVAL CHOIR

THE VOICE
TAMASHA HILI LINATARAJIWA KUFANYIKA KATIKA UKUMBI WA CITY CHRISTIAN CENTRE, TAREHE 24/11/2013 KUANZIA SAA NANE MCHANA MPAKA MOJA JIONI KWA VIINGILIO VYA TSH 10,000(Kawaida) na 20,000 (VIP)
Tiketi zinapatikana SILVERSPOON-mlimani city
Kituo cha MAfuta Mwenge-PUMA,kwenye baadhi ya makanisa pamoja na
Banana kwa Giddo
CCC-Mlangoni.....Kumbuka Usafiri kutoka Posta utakuwepo kuwaleta watu tamashani kwa wale wasiopafahu.

Na King Chavala-MC
Publicity & Protocal Manager

KWA MAELEZO ZAIDI
Piga 0713905118 au 0713883797

Monday, November 4, 2013

NEEMA MBISE KUZINDUA ALBUM YAKA YA SAUTI NA VIDEO TAR 17 NOV MOSHI MJINI!!!

MWANAMUZIKI WA INJILI ANAYECHIPUKIA, ANAYEVUMA SANA PANDE ZA KASKAZINI MWA TANZANIA, BAADA YA KUREKODI SAUTI NA KUFANYA VIDEO YA ALBUM YAKE IJULIKANAYO KAMA "SINA CHA KUKUPA"
HATIMAYE YUKO TAYARI KWA AJILI YA KUIWEKA WAKFU AMA KUZINDUA KAMA WENGI WALIVYOZOEA KUITA...TAMASHA HILI KUBWA LA KIPEKEE LINATARAJIA KUWAKUSANYA WAKAZI WA MOSHI NA ARUSHA PAMOJA NA VITONGOJI VYAKE, NEEMA MBISE ATASINDIKIZWA NA WAIMBAJI KAMA VILE
1.AMBWENE MWASONGWE
2.AMBELE CHAPANYOTA
3.LEMBO JUNIOR
4.DANIEL SAFARI
5.GRACE WAGANA
6. ANTONY FRANK NKONDOLA
7.ARUSHA MASS CHOIR NA
8.THE SPRING OF PRAISE
NA WENGINE WENGI BILA KUMSAHAU MISE ANAEL ANAYEABUDU NA KUSIFU KWA KUTUMIA KIFAA KIITWACHO SAKSAFONI!

TAMASHA HILI LITAFANYIKA JUMAPILI YA TAREHE 17/11/2013 PALE UKUMBI WA MR PRICE CITY MOSHI-MKABALA NA TANESCO, KUANZIA SAA NANE MCHANA

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO, MHESHIMIWA LEONIDAS GAMA NDIYE ANAYETARAJIWA KUWA MGENI RASMI NA TAMASHA HILO LITAENDESHWA NA MSHEREHESHAJI NA MCHEKESHAJI MAARUFU TANZANIA, KING CHAVALA-MC TOKA DAR ES SALAAM!!

NI MUHIMU SANA NA WEWE KUWA SEHEMU YA TAMASHA HILI....TIKETI NI 2000 TU KWA WATU WAZIMA NA 1000 KWA WATOTO!

NEEMA MBISE NI MWIMBAJI WA MAZINGIRA YETU YA NYUMBANI...HEKO WATU WOTE WA MOSHI TUJITOKEZE KUMPA MKONO WA KUMTIA MOYO BINTI YETU!!

GOSPEL STANDARD BASE INAWATAKIENI MAANDALIZI MEMA NA TAMASHA JEMA!!!

Monday, September 30, 2013

JOHN LISSU KUANDIKA HISTORIA YA MUZIKI WA INJILI TANZANIA TAR 06/10/2013!!!



UKO HAPA DVD LIVE RECORDING
 NA JOHN LISSU,
06/10/2013,CCC-UPANGA, DAR ES SALAAM, TANZANIA.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA WATANZANIA WOTE;
SALAM TANZANIA!

Shalom Dar es salaam, Shalom Tanzania!
Ndugu wanahabari na watanzania wote kwa ujumla!
Naamini tuko salama na tunaendelea na shughuli zetu za kila siku alizotupatia Mungu wa mbinguni, tumshukuru Mungu sana kwa Amani na utulivu aliotupa na tuendelee kumuomba ili atuepushe na kila aina ya dhahama na uharibifu wa Yule adui!
Kama tulivyosikia hivi karibuni, yale yaliyotokea nchi jirani ya Kenya, kwa hakika tunawapa pole sana kwa mkasa huo, pole kwa wale waliowapoteza wapendwa wao na wale waliojeruhika tunawaombea wapone haraka, tunaamini hekima ya Mungu itakuwa juu ya serikali yao kushughulikia jambo hilo kikamilifu.
Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai, hata sasa tunapoende kumalizia robo ya tatu ya mwaka 2013, tumeshuhudia mambo mengi sana mwaka huu ya kila aina, yapo yale yalionza kwa mara ya kwanza na mengine yamekuwa ni mwendelezo tu wa yale yadumuyo au yalioyaanza hapo kale, tumeshuhudia michezo mbalimbali na vipaji lukuki vikiinuka na kuimarika katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu, na kwa yote mema na mazuri tunampa Mungu Utukufu kwa hakika!


UTANGULIZI JUU YA JOHN LISU;

John Lisu ni mmoja wa waimbaji/Waabudishaji wanaoheshimika katika Tasnia ya muziki wa Injili kutokana na mchango wake mkubwa alioutoa katika kukuza na kuendeleza muziki wa Injili nchini Tanzania na nje ya Nchi. Nyimbo nyingi alizozitunga na kuziimba zimekuwa zikitumika katika makanisa mbalimbali kama nyimbo za kusifu na kuabudu; pia waimbaji wengine waliokua wakiimba naye wameweza kukua na kufikia uwezo wa kuwa waimbaji wa kujitegemea. John Lisu pia ametia hamasa kubwa miongoni wa wanamuziki wa Injili kuanza kufanya muziki wa live. John Lisu ameweza kufanya tours za ndani ya Tanzania, Africa na Bara la Ulaya kwa ajili ya huduma.
CHRISTINA SHUSHO

John Lisu anategemea kufanya Project II ya Live recoding inayojulikana kama "UKO HAPA" baada ya project ya kwanza ya Jehova yu hai kufanya vizuri sana. Tamasha litafanyika ndani ya ukumbi wa City Christian Centre (CCC) Upanga tarehe 6 Octoba 2013, kuanzia saa 8. mpaka saa 2 usiku.
PAUL CLEMENT

 Tamasha litasindikizwa na waimbaji nguli kama Christina Shusho, Neema Gospel Choir, Paul Clement, Pastor Safari Paul, Bomby Johnson Waimbaji wote wamethibitisha kuwepo. 

BOMBY JOHNSON

VENUE:
City Christian Centre (CCC) mkabala na chuo kikuu cha mzumbe
Si mbali saana kutoka Diamond Jubilee
MIRIUM LUKINDO WA MAUKI


USAFIRI (basi zilizobandikwa matangazo ya tamasha) utakuwepo kutoka posta mpya kwenda ukumbini kuanzia saa saba na nusu mchana kwa bei ya kawaida.
PASTOR SAFARI PAUL

HABARI NJEMA-MUHTSARI!!!!!

Sasa kwa mara pili nchini Tanzania, mwimbaji WA NYIMBO ZA INJILI na mwabuduji JOHN LISSU wa jijini Dar Es Salaam, atakuwa anafanya Ibaada kubwa ama Tamasha la kusifu la Kuabudu(LIVE PERFORMANCE), litakalorekodiwa moja kwa moja (DVD LIVE RECORDING) lenye jina “UKO HAPA” (Yaani Mungu na Uwepo wake).
Tamasha hilo litafanyika jumapili ya Tarehe 6, Octoba 2013  katika Ukumbi mkubwa wa kisasa wa Kanisa la City Christian Centre (CCC)- Upanga, mkabala na Chuo Kikuu Mzumbe – tawi la Dar es salaam, kuanzia saa nane mchana.
Tunataraji watu 5000 kuwa sehemu ya tamasha hili la kipekee,Utakuwa sehemu ya tamasha hilo kwa tiketi ya 10,000/= (kawaida), 20,000/= (VIP) na 3000/= (Watoto);
na Kwale watakaohitaji tisheti maalum za tukio hilo, basi zinapatikana kwa kati ya 12,000-15,000/=, wewe wasiliana tu na (0713905118)
NELLY-MKE WA JOHN LISU


VITUO VYA KUUZIA TIKETI;
1.   MWENGE – Tarakea duka la Kanda
2.   KINONDONI – DPC
3.   MLIMANICITY – Silverspoon Restaurant
4.   KARIAKOO – Mbogo Shop
5.   UKONGA BANANA – KWA GIDO
6.   POSTA - DUKA LA MSAMA

T-SHIRTS

-T-shirts maalumu kwa wanaume na wanawake zinapatikana katika vituo vya kuuzia tiketi kwa bei ya elfu kumi, mpaka elfu 15(kutegmeana na aina).

N.B; Kwa tiketi ya VIP, mnunuzi atajipatia na Audio CD ya John Lissu ya “Uko Hapa”

USAFIRI UTAKUWEPO!!
Siku ya tamasha kutakuwepo usafiri kutoka Posta Mpya mpaka CCC-Upanga,eneo la tukio, hivyo kama wewe ni mgeni na hupafahamu mahali hapo, basi utakachotakiwa kufanya ni kupanda magari toka ulipo mpaka posta mpya kabla ya saa nane,na hapo utayakuta mabasi yenye mabango ya Tamasha, basi utajongea humo na hapo utawezeshwa kufika eneo la tukio, muhimu ni kuzingatia muda!

MUHIMU SANA!!

JOHN LISU NA TIMU NZIMA WAKIWA MAZOEZINI


Tamasha hili ni muhimu sana kwa Tanzania, hasa ukizingatia JOHN LISSU ni mmoja wa waimbaji wa kwanza kuimba live kila mahali anapoalikwa na ni mwimbaji wa kwanza binafsi kufanya LIVE DVD RECORDING pale Ubungo plaza, na ile ya kwanza iliitwa “JEHOVA YU HAI” na sasa anafanya LIVE RECORDING kwa viwango vingine bora zaidi, maana Mungu hutupa hatua moja zaidi kila siku.
Ni muhimu kwa kila mtanzania kujivunia kipaji na tukio hili muhimu katika historia, njoo umwabudu na kumsifu Mungu pamoja, Njoo ujifunze, Njoo umuunge mkono mtanzania mwenzako na njoo uje ufanyike sehemu ya Historia hii kwa Utukufu wa Jehova.
NEEMA GOSPEL CHOIR-KWAYA PEKEE ITAKAYOSHIRIKI "UKO HAPA"


MWALIKO MAALUM;
Kipekee Ninapenda kuwakaribisha wachungaji, mitume, manabii, wainjilisti, waalimu na viongozi wote wa makanisa na huduma mbalimbali, ninawakaribisha viongozi wote wa kisiasa na kijamii kutoka serikalini na vyama vya siasa vyote, ninapenda kuwakaribisha wanaharakati na wanataaluma wote, ninapenda kuwakaribisha waimbaji wote wa nyimbo za injili na wanasanaa wote, ninapenda kuwakaribisa wanafamilia wote, asiwepo wa kubaki nyuma, ninapenda sasa kukukaribisha wewe unaesoma hapa, naam nisaidie kumkaribisha na mwenzako na yeye aje na mwenzake, kimsingi tukio hili ni letu wote bila kujali kitu chochote, njooni tumsifu na kumwabudu Bwana na Mungu hataacha kuibariki Tanzania!
EMMANUEL NDIYE ATAKAYEMPIGIA JOHN LISU LEADING GUITOR


SHUKRANI;
Tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa Hakneel Production (Wadhamini wakuu), na Jonn Lissu na timu nzima ya maandalizi; Kanisa la CCC-Upanga; vyombo vya habari hususani Praise Power na WAPO Radio; Clouds TV kupitia CHOMOZA na Clouds Radio kupitia GT; Sibuka Tv kupita Gospel Hits; Bloggers hususani Christian Bloggers, magazeti na vyombo vingine vyote vya habari! Shukrani hizi zimfikie kila mtu mmoja mmoja aliyetoa mchango wa mawazo, fedha, ushauri, maombi, ubunifu, yaani mchango wowote wa hali na mali na Mungu awabariki nyote!
MIRIUM LUKINDO WA MAUKI


MUHTASARI MKUU;
Tukio; TAMASHA LA KUSIFU NA KUABUDU, LITAKALOREKODIWA
(DVD LIVE RECORDING CONCERT)
Mhusika; JOHN LISSU
Jina: “UKO HAPA”
Mahali; UKUMBI WA KANISA LA CITY CHRISTIAN CENTRE (CCC)- UPANGA
Lini; 06TH OCTOBA, 2013
Muda; KUANZIA SAA NANE MCHANA
Kiingilio; Tsh 10,000/= (kawaida); 20,000/= (VIP) na 5000/= (Watoto)

Wasindikizaji; CHRISTINA SHUSHO, MIRIUM LUKINDO, PASTOR SAFARI, BOMBY JOHNSON, NEEMA GOSPEL CHOIR-AIC Chang’ombe na PAUL CLEMENT.

Mengineyo; USAFIRI UTAKUWEPO TOKA POSTA MPAKA CCC-UPANGA na Unaweza kujipatia Tisheti pia.
Wahusika; WATU WOTE MNAKARIBISHWA!


UKIPATA HABARI HII USIACHE KUMSHIRIKISHA NA MWENZAKO, NAAMINI HAUTAKOSA TUKIO HILI MUHIMU LA KIHISTORIA KATIKA NCHI YA TANZANIA KWA UTUKUFU WA MUNGU!!





KWA PICHA NA TAARIFA ZAIDI;





MAWASILIANO:
O713 240 397 – JOHN LISU
0713 905 118 –PROSPER MWAKITALIMA – EVENT MANAGER
0713 883 797 - FREDY CHAVALA - PUBLICITY


Imetolewa na;
Fredy E. Chavala <King Chavala (MC)>
Publicity Manager
+255 713 883 797
On Behalf of The Organizing Committee