Wednesday, November 27, 2013

UMUHIMU WA MASHABIKI!!!


Katika MASHINDANO, kwa mfano riadha, huwa kuna MCHUANO mkali na MKIMBIAJI anapokaribia MAHALI pa USHINDI huwa inakua ni ngumu sana maana NGUVU za mwili zinaisha japo MOYO u radhi.

Sasa, wakati MKIMBIAJI anajitahidi, jasho linatiririka huku kambi ya ADUI ikizomea na kambi ya Mungu ikishangilia, kwa kadri MASHABIKI wa kambi ya Mungu wanavyoshangilia MKIMBIAJI anajikuta anapata NGUVU na anaongeza mbio. Akifika mahali WASHANGILIAJI wamekaa kimya au wanazomea, huyu ndugu hujikuta anakosa NGUVU ya KUSHINDANA na anakata tamaa hata mara nyingine kuzimia moyo, kuanguka au KUJIUZULU mashindano.

Katika NJIA ya IMANI ndani ya Yesu, sio tu kwamba njia IMESONGA ila pia ni NGUMU na kuna mambo mengi sana magumu. Kama hakuna KUTIWA moyo katika hii njia nakwambia wengi sana watazimia NJIANI kwa sababu KAMBI ya ADUI imezidisha KUZOMEA na kambi ya MUNGU haishangilii au imejiunga na kambi ya ADUI kumzomea MKIMBIAJI! Wengi wamerudi nyuma kwa sababu tu hawajapata watu wa ku-appreciate ka-hatua kadogo wanakojitahidi kupiga katika UDHAIFU na UCHANGA wao.


Hawa walio tutangulia, ambao mara nyingi wameishia KUJIGAMBA kwa MEDALI zao na kuhesabu madhaifu ya hawa WAKIMBIAJI wachanga, imekua KWAZO na ndio maana Yesu anasema OLE wake AKWAZAYE “mmoja kati ya WADOGO hao” kwa maana ni aheri angefungiwe jiwe la kusagia na KUTUPILIWA mbali kwenye vilindi vya bahari. Sasa mara nyingi sana watu wanadhani vita kali katika Injili ni ya WAMATAIFA, No! Katika maandiko fuatilia waliokua wanampa shida YESU kwenye huduma yake ni akina nani? Ni WAKUU wa DINI! Wakati Bwana anatandika Injili, wao wanakuja na VITABU vyao KUPIMA ujumbe ili wapate mahali pa KUMHUKUMU badala ya kujifunza au kumsaidia KIHUDUMA! Hakuna mahali tunaambiawa WAKUU wa DINI walijikusanya kwa MAOMBI kwa ajili ya huyu “dogo” wa Nazareti aliyeibuka hapa JUZI. Walitafuta kumhukumu! Nikodemu akagundua SIRI, ila kwa kuogopa, akajisalimisha kwa siri. Sasa usifikiri ilikua rahisi, maana Yesu alikuwa kijana mdogo sana tu, wa takriban miaka 30, na hawa WAKUU wa DINI ni MIJIBABA ya NGUVU iliyobobea katika KILA ELIMU. Na haikua rahisi kupenya hapo. Wakamsulubisha Bwana wangu ili wazimishe CHANAGAMOTO kubwa aliyokua akiibua katika ile jamii hadi wale WAKUU wakaona UMAARUFU wao unapata shida.

Nazungumza na TAWI changa muda huu. Kumbuka SIRI ya kuzaa ni kukaa katika MZABIBU (Yesu). Na Kuzaa MATUNDA ni LAZIMA! Ila pamoja na UCHAFU wako na UNYONGE wako usikatishwe tamaa. Jipe moyo. Hivyo hivyo usikatishwe tamaa kwa maana BWANA alisema “ukizaa” UTASAFISHWA ili uzae zaidi. Kwanini USAFISHWE kama wewe ni SAFI tayari? Hakuna asiye na MADHAIFU, ila usiangalie udaifu wako au wa wengine ukashindwa KUSIMAMA katika nafasi yako na KUZAA matunda. Mara nyingine UTAZOMEWA badala ya KUSHANGILIWA sio tu na Ibilisi ila hata na wale waliopaswa KUKU-SUPPORT nao watakaa kimya au kukufanyia FITNA! Kaza uso wako kwa BWANA kama STEFANO, usihesabu MAWE unayopigwa, Mtizame BWANA aliyekuita, na USISAHAU kuwasamehe wanaokurushia MAWE. Njia imesonga, ukisikia kubanwa jua hujapotea njia. UWE na AMANI TELE.

Frank Philip.

No comments:

Post a Comment