Friday, November 22, 2013

UJUMBE kwa WANAFUNZI!!!



Elimu ya kawaida tunayosoma mashuleni ni sehemu ya makusudi ya Mungu ili uweze kuishi maisha BORA na uweze KUFANIKIWA kwa urahisi katika shughuli za kila siku ikiwemo na kumtumikia Mungu. Mungu hapendi “mbumbumbu” Soma kwa bidii.

Kuna vitu vya msingi nataka niweke hapa. Kwanza jua kuna uhusiano wa MAFANIKO yako ya kielimu na TABIA yako. Tabia ni mjumuisho wa mwenendo wako ambao unajidhihirisha katika matendo, maneno, mawazo na hisia zako. Tunajifunza katika Neno la Mungu kwamba “maneno mabaya huharibu tabia njema”. Kama unataka kuchunga tabia yako, jifunze kuchunga “makundi” ya watu na mambo wanayoongea katika makundi hayo. Imani yoyote huja kwa “kusikia” au kwa kuona, na hicho unachokisikia/kiona ndicho kitakujengea imani fulani ambayo ina athari kubwa katika utendaji wako wa kila siku. Ukisikiliza sana Neno la Mungu utakua na IMANI ya kiungu, ukisikiliza sana mambo ya KICHAWI utajikuta unaanza kuamini katika ushirikina, nk. Tengeneza imani yako na ilinde sana maana itakupa ushindi katika VITA mbalimbali za kitaaluma.

Biblia inaita elimu ni “uzima wako” na inasema umshike sana na usimwache aende zake huyu mdudu anaitwa Elimu, kwa maana kuna faida kubwa. Na kwanini unshike sana? Kwa sababu anateleza! Ni ngumu kukamata, inahitaji jitihada na Elimu “hakungoji”. Changamoto kubwa ya elimu ni MUDA, kila kiwango cha elimu kinapimwa kwa muda na muda haukungoji.

Kabala Mungu haja mtumia Musa kufanya kazi kubwa sana ya Ukombozi wa taifa la Israel alikaa kwanza shule, akasoma elimu “yote” ya Misri! Sio elimu ya DINI, No. Elimu ya Misri. Kuna wale vijana watatu mashujaa sana majina yao ni Shedrack, Meshak na Abednego, pamoja na Daniel, wakiwa huko Babeli kitu kimojawapo walichofanya ni kujifunza shule kwanza, miaka 3 darasani! Usije ukadhani walikua mabingwa wa KUSALI tu, hapana walikua WANAPIGA kitabu kwa msuli mkubwa pia. Baada ya kufuzu ndio wakapata AJIRA IKULU.

Ukiangalia kwenye again Jipya. Yesu alijifunza kusoma ndio maana alipoingia hekaluni aliomba Gombo la chuo na akasoma Mlango wa 61 wa kitabu cha nabii Isaya. Ukifuatilia idadi ya machapisho kwenye Agano jipya utagundua Mtume Paulo aliandika karibia ¾ (robo tatu) ya Agano jipya, kwanini? Alikua msomi kuliko wenzake! Alikaa chini ya Mafarisayo nguli akasoma sheria na Torati na alikau msomi kamili.

Sasa Vijana wengi sana wanafikiri wataenda chuo kuu kwa IMANI! Ni sawa kabisa, LAKINI imani bila matendo imekufa. Lazima ujichimbie na uwe na nidhamu ya kukaa LIBRARY/MAHALI na KUSOMA kwa ADABU na kwa BIDII. Achana na michezo ya kupoteza muda na mafariki wabaya. Komboa muda wako maana hizi ni saa za uovu. Ibilisi ameharibu watu wengi sana wakiwa katika ngazi ya UANAFUNZI kwa sababu mbalimbali. Kwa mfano, uwezo mdogo wa wazazi kukupa hela za matumizi na “tamaa” ya kula na kumiliki vitu vizuri inakuzonga. Waswahili wanasema “tamaa inaua” lakini katika maandiko imo hiyo kwamba “Mungu hamjaribu mtu, ILA mtu hujaribiwa na tamaa zake mwenyewe, na tamaa ikikomaa huzaa dhambi na dhambi ikishakukomaa huzaa MAUTI”. Kila mtenda dhambi ni MTUMWA wa zambi, na sifa ya mtumwa ni kutokua na uhuru wake! Sasa sikiliza MWANAFUNZI, ukianza kuishi maisha ya dhambi, ghafla unakua “mtumwa” wa hiyo dhambi na unaanza kuitumikia kwa AKILI na MAWAZO yako na shule inakua NGUMU. Mara nyingi mtu aliyeko katika ngazi hii hajui kiwango cha madhara hadi yatokee ndo maana naleta huu ujumbe ili ufanye uamuzi LEO.

Kama mtu angerudisha miaka 20 nyuma kwa watu wote, nakwambia hutaamini jinsi watu wangesafisha “DIVISION” zao na yamkini idadi ya Division ZERO ingekua ndogo sana au hakuna aliyefeli. Kwanini? Majuto ni mjukuu. Wengi wamechezea MUDA wao wakiwa shuleni na wamefeli na maisha yanawachapa FIMBO kila siku na wamekosa nafasi za muhimu kwa sababu ya kigezo cha ELIMU! Wangepata nafasi ya kurekebisha UFAULU wao nakwambia asingekuwepo hata mmoja angefeli baada ya “kichapo kikali cha maisha”. Ila pia kwa bahati mbaya sana wengine wamejikuta wamepata “magnjwa magumu sana” wakiwa shuleni, Mungu awarehemu tu na bado Mungu ana DAWA ya kuwasaidia hata hao, waje tu watapata REHEMA.

Kumbuka mwanafunzi. Anayelala sasa akiwa shuleni atarajie kukesha kwa ugumu wa maisha na anayekesha sasa hivi akijitahidi na kufaulu ajue huko mbele atafaidi matunda manono. Jua pia kwamba MFUMO wa Elimu umewekwa ili KUBAGUA nani afanye kazi chafu/ngumu kwa mapato KIDUNCHU na nani afanye kazi safi/nzuri kwa mapato MANONO. Chagua unataka nini na anza kujipanga kwa maombi na kufanya kazi kwa bidii. Chunga simu za mkononi, Internet, magazeti, tamthilia, TV, michezo mbalimbali, nk. Hivi vitu ni vya muhimu sana ila uwe na HEKIMA maana vimepoteza wengi. HATIMA YAKO IKO MIKONONI MWAKO. MUNGU ATUSAIDIE. AMEN

Frank Philip

No comments:

Post a Comment