Tuesday, November 5, 2013

MILITARY COMMANDOES IN ACTION!!!


(A commando is a soldier specially trained to carry out raids and ‘special missions’)

Mara nyingi tumesikia habari za vita na matetesi ya vita au mashambulizi ya kigaidi amabayo ni magumu na yanahitaji UJUZI na SILAHA malumu katika kukabiliana nayo.

Sio kila askari au mtu anaweza kuhusika na ‘kushinda’ katika baadhi ya “mission” fulani dhidi ya adui. Kuna mission ambazo zinahitaji Ma-COMMANDO tu! Kibaya zaidi adui akija anaangamiza bila huruma. Kazi ya adui ni: KUIBA, KUHARIBU na KUCHINJA (Yohana 10:10), huja kama “simba angurumaye na huzunguka akimtafuta askari aliyekaa vibaya ili ammeze”(1Petro 5:8)

Mafanikio ya askari yeyote KATIKA UAWANJA WA VITA yanategemea mambo kadha:
1. Kujua uwezo wa silaha zake na wapi zinafanya kazi: “Maana silaha za vita vyetu SI ZA MWILI, bali ZINA UWEZO KATIKA MUNGU hata kuangushya ngome; tukiangusha MAWAZO na kila kitu kilichoinuka, KIJIINUACHO JUU YA ELIMU YA MUNGU; na tukiteka nyara kila FIKIRA ipate kumtii Kristo; tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, KUTII KWENU KUTAKAPOTIMIA” (2 Wakor. 10:3-6).
2. Maarifa: “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa”, Askari akikosa maarifa anaangamizwa na adui, (Hosea 6:4).
3. Kujua Neno na Nguvu za Mungu: “ Askari asipojua hilo anapotea katika uwanja wa vita” (Yesu)
4. Ushuhuda: “Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao..” (Ufunuo 12:11a)
5. Damu ya Yesu: Simply like a bullet proof! (Ufunuo 12:11)
6. Silaha zote: Helmet (wakovu), mkanda (kweli), Dirii ya kukinga kifua/moyo (haki), upanga/bunduki (Neno la Mungu), boot (Injili), ngao (imani).
7. Jina la Yesu: “KILA atakayeliitia JINA hili ataokoka”. “Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa UWALINDE hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. 12 Nilipokuwapo pamoja nao, MIMI NALIWALINDA KWA JINA LAKO ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie. (Yohana 17:11b, 12)

Waefeso 6: 10 “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu Zake. 11Vaeni silaha zote za Mungu ILI kwamba mweze kuzipinga hila za Shetani. 12 Kwa maana kushindana kwetu si juu ya nyama na damu, bali dhidi ya falme, mamlaka, dhidi ya wakuu wa giza na majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. 13 Kwa hiyo vaeni silaha zote za Mungu ili mweze kushindana siku ya uovu itakapokuja nanyi mkiisha kufanya yote, simameni imara. 14 Kwa hiyo simameni imara mkiwa mmejifunga kweli kiunoni na kuvaa dirii ya haki kifuani, 15nayo miguu yenu ifungiwe utayari tuupatao kwa Injili ya amani. 16 Zaidi ya haya yote, twaeni ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu. 17Vaeni chapeo ya wokovu na mchukue upanga wa Roho, ambao ni Neno la Mungu. 18Mkiomba kwa Roho sikuzote katika sala zote na maombi, mkikesha kila wakati mkiwaombea watakatifu wote.”

Je! Wewe umejifunza kutumia silaha ngapi na kwa uhodari gani? IDADI, UMAHIRI na UZOEFU wa kutumia silaha NYINGI zadi kwa USAHIHI, pamoja na kujua MBINU za adui, SIRI na MAARIFA ya uwanja wa VITA vitakufanya uwe mmojawapo wa ma-COMANDO wa Yesu!
 
Na Fank Philip 

No comments:

Post a Comment