Sunday, January 5, 2014

SIRI ya MAFANIKIO YAKO!!



SIRI ya MAFANIKIO YAKO
(UMUHIMU wa KUJIFUNZA NENO la MUNGU)

Wakati tunatarajia MEMA katika MWAKA mpya 2014 nimeona nikupe SIRI ya jinsi haya MEMA yanaweza kukujilia maishani mwako. Kumbuka sio kila AHADI ya kwenye Biblia ni yako hata ukiikiri USIKU na MCHANA. Kuna KIWANGO cha IMANI katika KUPOKEA AHADI za Mungu. Kumbuka “imani huja kwa kusikia na kusikia huja kwa Neno la Kristo”. Sasa nataka ujifunze kwamba unapata ZAIDI ya IMANI pale unapojifunza Neno la Mungu.

Unapojifunza Neno la Mungu KIWANGO chako cha KUMJUA Mungu kinaongezeka. Haiishii hapo, kila unapoongeza KIWANGO cha kumjua Mungu mambo mawili yanatokea (i) AMANI yako inaongezeka (ii). Mema yanakujilia. (Ayubu 22:21)

Hakuna kitu nafurahi kama kusikia feedback kwamba kuna MTU amebarikiwa na FUNDISHO la UFALME (Mambo ya Mungu). Ukisikia umebarikiwa mara nyingi sana inamaanisha umepata UFUNUO fulani (Mungu amefunuliwa kwa njia fulani zaidi katika maisha yako kupitia hilo Neno). Sasa huku mimi najua sio tu UMEBARIKIWA na kuongeza MAARIFA ya kiroho, ila na kiwango cha AMANI na KUFANIKIWA kwako katika mambo yote na MEMA yanaongezeka katika maisha ya kila siku.

Basi tusiwe wavivu kujifunza mambo ya Mungu kwa maana ANATUFUNDISHA ili tupate FAIDA. (Isaya 48:17-19). Ukiona kwenye TV (series, movies, nk.) na kusoma NOVEL na MAGAZETI unachangamka ila hata page 3 tu za mafundisho ya Neno la Mungu unaona ni MZIGO, ujue uko karibu na HASARA kama HUJAPATA tayari.

Nawatakia HERI ya MWAKA MPYA 2014.

Frank Philip

No comments:

Post a Comment