Monday, December 23, 2013

KILIO CHA MWENYE HAKI!!!



Leo nataka niseme juu ya KILIO. Kuna tofauti ya kulia kwa machozi ya nje na kulia kwa machozi ya ndani. Mtu anapotendewa kitu na ndani yake akasikia KUNYANYASIKA na akasikia uchungu sana, mara nyingi anatoa machozi ya nje (atalia). Lakini sio kila mara mtu atalia kwa machozi, ila kuna ule UCHUNGU wa ndani ambao watu mbalimbali wamekua nao na wameenda mbele za Mungu kwa maombi au hata wametamka tu maneno na Mungu AMESIKIA (“nipo pamoja nanyi katika mipango yenu, kabla ya kuomba mimi Bwana nitasikia na mkiwa katika kunena mimi Bwana nitajibu”). Chunga hii kitu, Mungu anasikia KILIO kuliko unavyodhani. Na mara nyingi sana hiki KILIO hata kama mtu sio mlokole nakwambia UKIMDHULUMU, UKIMNYANYASA, UKIMTENDA JEURI mtu na akalia kwa UCHUNGU mbele za Mungu hata kama hakumwambia mtu au hata kama hajui kama Mungu anasika, nakwambia Mungu husikia VILIO.

Wakati Mungu anamtokea Musa na anamtuma Misri kuwakomboa wana wa Israel kutoka UTUMWANI, Mungu alisema “nimesikia kilio chao nami nimeshuka kuwakomboa”. Mungu hakusikia maombi bali KILIO! Sasa ninataka uone huu mfumo vizuri. Pale Misri wana wa Israel walikua watumwa, na juu yao kulikua na VIONGOZI na WASIMAMIZI na kule juu kabisa alikuwepo Mfalme Farao. Kiutawala hawa watumwa walikua chini kabisa, ila walikua WANA wa MUNGU aliye hai. Kumbuka “hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu na ile iliyopo imeamriwa na Mungu”. Kwa lugha ya kawaida BOSS mkubwa sana katika “utawala wowote” hapa duniani ni Mungu. Sasa kama mtu mwenye HAKI, amefika mahali pa gumu sana na amelia kwa MATESO mbalimbali, akiwa hajui huu mfumo bado BOSS mkubwa hushuka hapo na kurekebisha mambo, haleluya! Kwa wale wanajua hii SIRI na kusimama katika nafasi na zamu zao vizuri, HAWATAMSUJUDU boss wao wa duniani na kufanya NGONO, nk., na kumkosea Mungu kwa sababu ya kulinda MASLAHI yao ya kikazi. Watapambana kwa “NIA ya kushinda UOVU na KUTII kwao kutakapotimia MAMLAKA yao katika ulimwengu wa roho dhidi ya wakuu wa giza na majeshi ya pepo wa baya ITAONGEZEKA sana”. Na KILIO chao Mungu atasikia na ATASHUKA kuwaokoa. Kumbuka, Mungu ndio boss mkubwa pale juu ila maandiko yanatuonya TUTII mamlaka iliyo kuu. Na usithubutu kumwambia kiongozi wako kuwa wewe sio boss ila boss ni Mungu. Jua hilo moyoni na mtizame Mungu kama Mkuu wako wa kazi na chapa kazi kwa moyo, acha uvivu.

Nebkadneza mfalme wa Babeli alikwenda kula majani miaka/misimu 7 kwa kosa la kujisifia kwamba “huu mji ni mkono wangu umejenga?” Akatizama mafanikio ya Ufalme (kampuni yake) akajiinua ndani ya moyo wake! Mungu akasema sasa utajua kwamba mimi natawala pamoja na wanadamu, sio wewe Nebkadneza, ni Mimi! Hii siri watu “wachache” wanaijua na wamehusika kuwapiga “transfer” (uhamisho) mabosi wao kwa sabababu wameleta shida kwenye KAMPUNI na jina la Mungu linatukanwa au watu wamenyanyaswa. Transfer inaweza kuwa kulala, kushushwa cheo (kula majani), kuhama kituo cha kazi, nk. Ila vita vyetu sio juu ya DAMU na NYAMA. Ni katika roho, na tunapata NGUVU tukiwa na NIA thabiti ya kupinga UOVU wote na KUTII kwetu kutakapotimilika (2Kor. 10:4-6). CHUNGA sana usije ukafanya mambo kwa HUSUDA, WIVU au MASHINDANO, utashindwa. Mamlaka ya Mungu haifanyi kazi hapo. LAZIMA usimame katika KWELI na HAKI na sio maslahi binafsi. Usikubali kumkosea Mungu kwa kisingizio eti “sasa huyu ni MHESHIMIWA na mimi ningefanya je?”, mwite Yesu hapo akuokoe na KILA (hata kama sio mlokole) atakayeliitia jina la BWANA ataokoka katika hali anayopitia. NEEMA ya BWANA izidi KWENU. AMEN

Frank Philip.

Sunday, December 22, 2013

KAMA UNATAKA MUNGU AONEKANE NA WATU JIFUNZE HII SIRI



Kipimo cha UDHIHIRISHO (MANIFESTATION) wa Mungu kwenye HADHIRA (PUBLIC) ni MUDA, BIDII na HALI ya MOYO wako UKIJIHUDHURISHA mbele Zake mkiwa wenyewe wewe na Mungu pekeyenu (SIRINI).

Kama UKIJIHUDHURISHA mbele za Mungu wako kwa BIDII na kwa UELEKEVU mahali pa SIRI, basi Mungu ATAJIDHIHIRISHA mbele ya WATU hadharani.

Ukitaka Mungu aji-present kwa watu basi jifunze kuji-present kwa Mungu.

Ni aheri ukose MUDA wa kuandaa PRESENTATION kwa watu na sio MUDA wa kuji-present kwa Mungu, kwa maana unaweza ku-present kitu chochote mbele za watu ILA HUWEZI kum-present Mungu! Ndio maana kazi ya Mitume ilikua KUHUBIRI na KAZI ya Mungu likua KULITHIBITISHA hilo Neno kwa ISHARA na MAAJABU.

Kazi ya Musa ilikua kuji-present kwa Mungu na kupata maelekezo na KAZI ya Mungu ilikua KUTENDA miujiza (kuji-present) mbele za Farao!

Frank Philip.

Wednesday, December 18, 2013

(MAOMBI YENYE NGUVU).....SEHEMU ya II


Katika maisha yetu ya kila siku tumetamani MAMBO mengi mbalimbali yatokee. Mengi ya haya MAMBO yako nje ya uwezo wetu na IMETUPASA kuhitaji msaada wa Mungu au watu wengine. Mara nyingi utagundua ni vigumu sana KUTEGEMEA misaada ya watu KUTIMIZA mahitaji yetu ya kila siku. Njia rahisi ni kujua jinsi ya kujipanga vizuri na Baba yako wa Mbinguni na kwa kupitia Yeye, anaweza kuinua watu mbalimbali kuja kuingilia kati hali unazopitia na kukusaidia. Ikishindikana kabisa, Mungu anaweza kuinua kunguru, mawe au Malaika kuja kukupigania, na hii imetokea kwa wengi hata kwako pia inawezekana.

Kusudi la somo hili fupi ni kutaka kuhusianisha USHINDI wako na (i) NAFASI yako katika Kristo na KUZAA kwako MATUNDA, na (ii). KIWANGO chako cha MAOMBI na pia ujue (iii). VIKWAZO vya Majibu ya maombi yako, (iv). Kutofautisha imani ya KUOMBA na KUPOKEA, na (v). Ujue jinsi ya KUJITEGEMEA kimaombi.

i. NAFASI yako katika Kristo
Mambo kadhaa ni ya LAZIMA: (a) kukaa ndani ya Yesu, (b). Neno kukaa ndani yako, na (c). Omba lolote utapewa. Yesu alitufananisha na yeye akiwa mzabibu, akasema“ sisi ni matawi ya mzabibu na yeye ni Mzabibu. pasipo yeye sisi hatuwezi jambo lolote”. Pamoja na kwamba Yesu alikuwa anazungumzia KUZAA matunda, utagundua pia mistari iliyofuata alisema juu ya MAOMBI. Kwa upande mwingine kuna uhusianao kati ya KUZAA matunda na KUJIBIWA maombi yako. (Yohana 15:1-6).

ii. KIWANGO cha maombi
Yesu alipowatuma wanafunzi wake kwenye HUDUMA mambo mengine yalikuwa magumu, japo wametumwa na Bwana! Walipomuuliza kwanini mambo mengine yanagoma? Yesu alijibu “mambo mengine hayawezekani bila KUFUNGA na KUOMBA”. Hapa tunapata picha kwamba kuna kiwango fulani cha maombi kinaweza kukuvusha hadi hatua fulani. Ukifikia hiyo hatua inahitaji GIA nyingine ya maombi ya kiwango cha juu zaidi ili uvuke kwenda kwenye hatua ya juu zaidi.

Pamoja na BIDII (diligence) na KUDUMU (persistance), haya mambo mawili ni ya muhimu sana KUPIMA kiwango cha USHINDI wako katika yale unayoyaombea. Kuna wakati itakupasa kuongeza NGUVU/KIASI cha kuomba ili kuvuka mahali ulipo. Hata kama wewe ni TAWI na UKO ndani ya Yesu vizuri na Neno (imani) limejaa ndani. (Luka 18)

iii. VIKWAZO vya MAJIBU ya Maombi yako
Kuna uhusiano mkubwa sana wa KUPOKEA majibu ya MAOMBI na HALI ya MUOMBAJI mwenyewe pamoja na KUTIMIZA viwango vingine kama (i) na (ii) hapo juu. Kila mtu anajua kwamba tukiomba sio mara zote mambo hutokea wakati huo-huo. Kuna kipindi cha KUSUBIRI na wakati mwingine kinakuwa kirefu. Ili uweze KUPOKEA majibu yako angalia usikate tamaa kwa maana “Mtavuna kwa wakati msipozimia roho.” Huhitaji IMANI kubwa kupokea MAJIBU ya Maombi yako. “Imani kidogo sana kama chembe ya haradali tu, inaweza kuhamisha milima na kufanya mambo makubwa sana maishani mwako ila usipokuwa na SHAKA juu ya yale mambo uombayo”. MASHAKA ni KIKWAZO kikubwa cha kupokea uombayo hata kama una IMANI. Kwa lugha nyepesi, mashaka ni sumu ya IMANI yako. Adui anajua ukiomba kwa imani utapokea, sasa akishindwa kukuzuia usiombe, basi ataleta MASHAKA katika yale uyaombayo ili USIPOKEE. Ukiwa makini utamsikia katika “mawazo yako” akikukukatisha tamaa na saa nyingine akikuzomea kabisa. Pambana na hayo mawazo maana ni vita inayoweza kuathiri IMANI yako na majibu ya maombi yako. (2 Wakorinto 10:1-6)

iv. JUA kutofautisha IMANI ya KUOMBA na IMANI ya KUPOKEA
Watu wengi sana wana IMANI ya KUOMBA ila wachache wana IMANI ya KUPOKEA. Ukiwauliza watu juu ya maombi kwa kweli watakuambia Mungu anajibu ila ukichunguza WANACHOONA ndani ya MIOYO yao ni KUSHINDWA zaidi kuliko KUSHINDA. Matokeo yake hawawezi KUPOKEA majibu kwa maana hawana IMANI ya KUPOKELEA.

Nitakupa mfano. Pamoja na kwamba Yesu ni mponyaji na Muumbaji wa Ulimwengu, utasikia mahali anasema “imani yako imekuponya”. Ina maana imani ya KUPOKEA ni ya MPOKEAJI na sio imani ya Yesu japo kuna mahali ALIWAHURUMIA tu watu akafanya mambo kabla hata hajaombwa na mtu (Luka 7:12,13). Kati ya maeneo ambayo Yesu hakufanya miujiza ni kule mitaa ya nyumbani kwao, SABABU sio uhaba wa IMANI ya Yesu ila IMANI ya WAPOKEAJI haikwepo. Yesu hakufanya kitu japo wengi walikuwa na shida zao nyingi na aliwahurumia! Ndipo akasema “nabii hakubaliki kwa watu wake.”

v. EPUKA MAOMBI TEGEMEZI
Kuna kundi la watu wamefanya baadhi ya watumishi kama TIKETI ya kupokelea majibu ya MAOMBI yao. Sawa, kuna kiwango cha NEEMA juu ya watumishi wa Mungu kinachoweza kukuvusha mahali, lakini nakwambia kuna wakati hata YESU “alipoitizama imani ya watu, ndipo alipotenda jambo” pengine aliacha kwa sababu ya KUTOKUAMINI kwao! UELEKEVU wa MOYO wako kwa Yesu utakusaidia sana katika KUPOKEA majibu ya maombi yako.


Sasa tunakumbushwa siku zote kuomba kwa imani na kuambiwa kwamba “kuomba kwake mwenye HAKI kwa faa sana akiomba kwa bidii”. Jifunze na uchukue MAZOEZI ya kutumia IMANI yako kwa maana imani ina tabia ya KUKUA au KUPUNGUA. Kumbuka KUKUZA imani ya KUPOKEA majibu ya maombi yako kwa maana hiyo ndiyo inayokwamisha wengi. Kumbuka adui mkubwa wa imani ya KUPOKEA anaitwa MASHAKA.

Dawa ya kupambana na MASHAKA ni kufanya MAZOEZI ya KUOMBA wewe mwenyewe na KUPUNGUZA utegemezi wa WATUMSHI wa Mungu. Sisemi ni vibaya kuombewa, ninachotaka kusisitiza ni wewe kujijengea UWEZO wa kusimama kwa MIGUU yako MIWILI kumwamini Mungu kwamba UNAWEZA kuomba na KUOPOKEA mwenyewe. Kumbuka wewe ni TAWI la Mzabibu na mtumishi pia ni tawi tu, anayejibu maombi ni MZABIBU (Yesu). Ukiweza kuepuka utegemezi kwa MATAWI mengine utagundua UMEVUKA hatua nyingine ya IMANI na KUMPENDEZA Mungu pia kwa sababu “haiwezekani kumpendeza Mungu pasipo imani”. Wengi sana tunaweza kumshangaa Petro jinsi alivyoweza kutembea kidogo juu ya maji na ALIPOONA upepo, akazama! Hiyo ndio kazi ya MASHAKA. Nadhani kama Petro angefanya tena mazoezi kwa mara nyingine, angekuwa hahitaji tena Mtumbwi kwenda ng’ambo! Kwanini? Alikuwa na IMANI ya kutosha KUTEMBEA juu ya maji ila MASHAKA yalikuwa kikwazo.

Nitakupa mfano. Nguvu ya DAUDI na UJASIRI aliokuwa nao wakati anamkabili Goliath, haikuwa kwa sababu tu alijuwa uweza wa Jina la Bwana wa Majeshi, ila “kama alivyofanya MAZOEZI ya kupambana na DUBU na SIMBA”, alijuwa kwa jinsi ILE ILE, BWANA atampigania kwa Goliathi. Hakubakia tu KUAMINI moyoni, DAUDI alimtangazia Goliath (adui) kwa SAUTI ya juu, mambo aliyoamini. Mara nyingi sana wakati UNAOMBA, adui akileta SAUTI ndani yako za kukutia mashaka, kumbuka KUMTANGAZIA kwa SAUTI juu ya USHINDI wako. Kwa njia hii utaweza kushinda MASHAKA. Msomee adui Neno, mwambie “imeandikwa”, kisha taja Neno (imani) katika biblia unalosimamia katika hayo maombi.

Uzoefu wa kutumia IMANI yako unakupa nguvu ya kuvuka hatua nyingine ya KUPOKEA mambo uombayo katika kiwango cha juu zaidi. Ukiwa unamtegemea MTUMISHI fulani tu, MOYO wako unaanza kuwa dhaifu na unaona PASIPO kujua unahamisha UELEKEVU wako kutoka kwa Mungu na kuuweka kwa huyu MTUMISHI. Hali hii imekuwa mtego mkubwa kwa watu wengi sana, wamehamisha MACHO yao kwa YESU na wengine wamefikia mahali pa kuona MTU mwingine anahusika na matatizo yao ndio maana wakati ule dada zake Lazaro walimlaumu Yesu (mtumishi) kwa kusema “ungekuwepo hapa kaka yetu asingekufa”!

Mungu atusaidie kuongeza IMANI ya KUPOKEA majibu ya maombi yetu.

Frank Philip.

Saturday, December 14, 2013

SABABU za KUKESHA!!!


Bwana Yesu alizungumza kwa mifano mingi akisisitiza UMUHIMU wa watu wake KUKESHA. Maana halisi ya KUKESHA ni kuwa macho hasa wakati wa USIKU ambapo watu kwa kwaida hulala. Katika maisha yetu kuna VIPINDI vya mchana ambapo kuna mwanga na tunaona. Pia kuna vipindi vya USIKU, kuna GIZA na hatuoni kitu kwa sababu ya giza. Mara nyingi watu wanakuwa SALAMA katika VIPINDI vya giza kuliko vipindi vya MCHANA kwa sababu wanachukuwa TAHADHARI na kujilinda. Lakini pia MAANDALIZI na MAFANIKIO ya ULINZI wako yanafanyika wakati wa MCHANA.

Vipindi vya MCHANA vina sifa nyingi. Mojawapo ni MWANGA. Kwa sababu UNAONA vyema, basi unakuwa na AMANI na UHAKIKA kwa sababu unaona VITU kwa jinsi ya MWILINI. Sasa tukumbuke tumeumbwa ili KUISHI katika ULIMWENGU wa MWILI na ULIMWENGU wa ROHO. Katika vipindi hivi tunaambiwa “Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafla, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.” (1 Thesalonike 5:1-7). Ukifuatilia mistari hii utagundua watu wa Mungu wameitwa ni wana wa MCHANA au wana wa NURU! Kwa lugha nyingine kundi la pili linaitwa WANA wa USIKU! Sasa, pamoja na kwamba mistari hii ilikuwa inakumbusha KURUDI kwa Yesu kulichukuwa Kanisa, nataka tujifunze hii TABIA ya Mungu ya KUKESHA.

Sehemu nyingine Mungu anajiita MLINZI wa Israel, Daudi alijuwa tabia ya Mungu ya KUKESHA na akasema “Msaada wangu u katika Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi. Asiuache mguu wako usogezwe; Asisinzie akulindaye; Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.” (Zab. 121:1-4). Hii tabia ya KUKESHA ni ya MUHIMU pia kwa WANA wa NURU ndio maana Yesu amesisitiza sana “kukesha katika kuomba” na pia akasema “atarudi kama MWIVI ajavyo usiku” akitutaka tuwe MACHO wakati WOTE. Pamoja na GIZA la dunia hii, Bwana anasema “tusiwe kama wale wanawali wapumbavu, waliochukua taa zao bila MAFUTA”, huko usiku wakati watu wamelala, ghafla! Bwana Harusi anakuja!

Kuna sababu nyingi za KUKESHA. (i) Tuweze kushinda/kutokuanguka majaribuni. (ii) Tuwe salama adui anapokuja kushambulia. (iii) Kujua wakati wa KUJILIWA na Bwana. (iv) Tusibaki Yesu akija kuchukua Kanisa lake. Sifa za WAKESHAJI utaziona hapa, “Miongoni mwao hakuna achokaye wala kukwaa; Hakuna asinziaye wala kulala usingizi; Wala mshipi wa viuno vyao hautalegea. Wala ukanda wa viatu vyao hautakatika; Mishale yao ni mikali, na pinde zao zote zimepindika; Kwato za farasi zao zitahesabika kama gumegume; Na gurudumu zao kama kisulisuli;” (Isaya 5:27,28). Nitazungumzia zaidi KUJILIWA. Yesu alipoutizama Yerusalemu alilia. Akasema “laiti ungejua yakupasayo amani”, Wakati Yesu (Baraka za Mungu) zinakuja, Israel hawakujua na kupokea kwa shukurani, na pia wakati ADUI anakuja kuharibu, hawakuwa na HABARI! Akalia. Maisha yetu tumejisahau sana na kuona tu mambo yataenda kama JANA! Tumepoa au kupunguza ile kasi ya kumtafuta Mungu na tunaishi kama MUNGU hayupo! Taratibu tunapoteza NURU na kuanza kutembea GIZANI. Usipoangalia Ghafla! Uharibifu unakuja, kwa maana ADUI anakuwinda na anasubiri GIZA akushambulie! “Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi. Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku. Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.” (1 Thesalonike 5).

Sio kila mara ukiona MWANGA (NURU) kwenye ulimwengu wa MWILI pia unaona MWANGA kwenye Ulimwengu wa roho. Ngoja tujifunze kwa Ayubu. “Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure? Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi. (Ayubu 1:9,10). Huu uliku wa ni wakati wa MCHANA (NURU) kwa Ayubu. Wakati Baraka ziko kila upande, mali, watoto, na mafanikio ya kila namna. Huku unaouna mkono wa Bwana (ukingo) unakupigania, nk. Ghafla! Giza nene linatanda! Sasa sio watu wengi sana wanapona hapa. ILA wale ambao WANAKESHA “watayaona mabaya yakija” (1 Thesalonike 5), na Mungu wao atawapa DAWA ya KUSHINDA. Kwa sababu wako NURUNI, MLANGO wa KUTOKA wakati wa KUJARIBIWA kwao watauona.

Mara nyingi sana watu katika maisha ya kawaida hawajali sana kwa sababu BANK kumenona, wanajua hata wakifukuzwa kazi LEO hawafi njaa. VITEGA uchumi vimesimama sawia. Karibia kila kitu kimekatiwa BIMA. Wanaweza kupata MATIBABU mahali popote duniani. Mambo ni SAFI, hata wakitafuta kwamba SHIDA inaweza kutokezea wapi hawaoni. Huwezi kuona UMUHIMU wa kukesha na KUDUMU kumtegemea Mungu kama huna macho ya rohoni na UELEKEVU kwa Bwana kama Ayubu. Lakini kwa wale ambao wamepitia majanga wanajua nasema nini. Kuna habari MBAYA hata sipendi kusikia licha ya kusimulia. Utakuta watu wameokoka tu vizuri, wamebarikiwa kuingia kwenye NDOA. Wanakuwa na mipango mingi ya maisha na KAZI/BIASHARA zao nzuri ziko sawa. Ghafla! Wasipotarajia, wameenda wote kazini na kabla ya jioni mmoja ametwaliwa! Ghafla tu! Status inabadilika, mmoja anaitwa mjane. Adui kashambulia. Wengine katika hali isiyotarajiwa, watoto wameenda shule, ghafla jioni hawarudi! Wanapata taarifa waende chumba cha kuhifadhia maiti kukagua! Hizi ni habari mbaya sana. Lakini haya ndio yalikuwa yanamtokea Ayubu wakati wa GIZA ulipoanza. Anajigundua hana WATOTO hata mmoja, wamekufa wote! Hana MALI halafu ni mgonjwa hajiwezi hapo chini. Mke wake naye analeta mambo magumu ya kumchanganya zaidi. Huu ni wakati wa GIZA.

Kusudi la somo hili ni kukumbusha habari ya KUKESHA. Katika kukesha kuna kujaa NGUVU na kujiandaa kupambana (Isaya 5). Nguvu za kukuwezesha kuvuka kwenye GIZA hupatikana wakati wa MCHANA. Maisha ya Ayubu kabla ya JARIBU ndio yalimwezesha KUSHINDA wakati wa jaribu. Watu wengi sana wanasubiri MAJANGA (GIZA) ndio wanaanza KUFUNGA na KUOMBA kwa BIDII na KUKEMEA kwa NGUVU. Sasa kweli wanakemea, ila nguvu iko wapi? “Ukizimia siku ya taabu, Nguvu zako ni chache.” (Mithali 24:10). “Wamtumainio Bwana ni kama MLIMA Sayuni, hawatatikisika kamwe” lakini pia Isaya anasema “bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.” (Isaya 40:31). KUSUBIRI kunahusianishwa na tabia ya KUKESHA.

Yesu anaposema “ni rahisi ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kuingia Ufamle wa Mungu” aliona hii shida KUFANYA mapenzi ya Mungu wakati watu wamezungukwa na kila kitu. Ndio maana alipomuuliza yule kijana tajiri habari za AMRI za Mungu, na kijana anasema ameshika ZOTE, maandiko yanasema “Yesu akampenda”. Kwanini? Sio rahisi kukaa katika Amri za Mungu wakati HELA inapiga kelele. Ukifanikiwa kumpendeza Mungu wakati una KILA kitu lazima uwe KIVUTIO kwa Yesu. Sasa, Angalia maisha yako vizuri. Pale mahali ulikuwa una SHIDA, huna hela na hujui unavukaje, ULIMTAFUTA Mungu kwa BIDII na kukaa mbali na DHAMBI. Leo Mungu amekuvusha, umemaliza shule salama, umepata kazi, nafasi na pesa, Ghafla! Unaanza kuwaza KUTENDA dhambi! Ukiwa kwenye SHIDA kwako ilikuwa MCHANA, sasa Mungu amekubariki na baraka za Mungu badala ya kuongeza NURU, zimekuwa GIZA! Na chukizo kwa Mungu. Je! Unataka Mungu akurudishe kule kwenye DHIKI ili taa yako iwake? Wakati unadhani ni “amani amani” angalia uharibifu uko njiani. Neno hili linakukumbusha UAMKE na KUCHANGAMKA, rudi kwenye MKESHA na kuishi kwa KIASI, huku ukimsubiri Bwana. Kuna faida gani “kuupata ulimwengu wote na kupoteza nafsi yako?” Jijibu mwenyewe na uchukue HATUA. Mungu akusaidie.

Basi Mungu atuwezeshe kukaa katika KIASI na KUKESHA kwa Jina la Yesu. AMEN

Frank Philip.

Friday, December 13, 2013

KAZI YA UVUVI [UPDATED] !!!


Kazi ya UVUVI ni moja ya kazi ambazo zinahitaji uzoefu lakini pia Imani. Umewahi kujiuliza mvuvi anaposhusha nyavu zake huko chini kwenye maji ambapo haoni kitu ila anasubiri kwa IMANI akijua samaki wataingia?

Petro alipoambiwa anabadilishiwa kazi kutoka kuvua SAMAKI kwenda kuvua WATU ilikau inahitaji shule zaidi kidogo ili aelewe somo. Siku moja Petro akaenda kwa UZOEFU, kumbuka sio ZIWA/BAHARI au maeneo asiyoyajua, anajua sana na ana uzoefu nayo. Si akakesha sasa usiku kucha na hakupata kitu! Yesu akaja, akamwambia “Petro shusha nyavu” na akampa maelekezo ya ziada. Petro akajiuliza, “nimehangaika usiku kucha ila sikukamata kitu na sasa unasema nishushe nyavu?”, akapiga moyo konde na kusema, “kwa Neno lako nitashusha”. Hao samaki aliokamata hakuweza kuvuta nyavu maana ni wengi hadi nyavu kuchanika! Akasema “ondoka kwangu mimi mwenye dhambi”! Kwanini? [kufanya kazi ya Mungu bila mapenzi yake ni kosa na itakugharmu].


Sikiliza. Watumishi wengi sana wa Mungu wanahangaikal na KINA na UZOEFU wa nondo (mafundisho, nyenzo, nk.) wanazotumia na USTADI wa kupiga MAKASIA. Bila KUSUDI la Mungu utakesha hapo nakutahadharisha. Sio katika HUDUMA tu ila hata katika michakato ya maisha, biashara, nk. Hakikisha unashusha NYAVU mahali ambapo unajua YESU amekuongoza. Huwezi kosa SAMAKI asilani. Uzoefu wako na UJUAJI vitakuponza tafuta KUSUDI la Mungu katika maisha yako na utaona MATUNDA yakimimnika maishani mwako kama MVUA. Mafanikio ya Petro hayakutegemea KINA cha maji, AINA ya nyavu, MTUMBI, UREFU wa MUDA, wala UZOEFU wake! Ila NENO la Yesu! Ukipata Neno la wakati huo katika MUKTADHA (context) na MAUDHUI (content) na MUDA (timely), mafaniko yako katika HUDUMA, BIASHARA, KAZI, SHULE, nk., yatakua makubwa kuliko kujitahidi kwa NGUVU zako mwenyewe na AKILI zako. Jifunze kumshirikisha Yesu nawe utaona HATUA atakazokufikisha.

Kumbuka. Mungu hulituma Neno lake “kama mvua ishukavyo kutoka juu kuangukia ardhi”, na LITATIMIZA makusudi yake, halitarudi bure. Ukijua Yesu anasema nini juu ya UVUVI wako, sema kama Petro “kwa Neno lako nitashusha nyavu” halafu tukikutana utanipa ushuhuda. Barikiwa.

Frank Philip

Thursday, December 12, 2013

JUA NGUVU YA NIA YAKO!!!


Katika mambo ya muhimu sana kwa maisha ya IMANI, moja wapo ni kujua NIA yako katika mambo fulani ya kimwili na kiroho. Kwa lugha nyepesi ni muhimu kujua MOYO wako “unasema nini juu ya jambo fulani” (nimetumia KUSEMA kwa maana Moyo unatoa sauti ya yale uwazayo mbele za Mungu). Au kwa lugha nyingine ni vizuri kujua “MTIZAMO wako juu ya mambo fulani” (Kuna picha/kitu halisi kinajengwa ndani yako na mawazo yako na ndicho Mungu anachokiona).

Sababu ya msingi ya kujua NIA (makusudi ya Moyo) yako ni kupima kiwango cha MUNGU kuhusika na hayo mambo UWAZAYO/UNAYOHITAJI ambayo mengi yanapita MOYONI mwako kama MAWAZO tu. Majibu ya maombi yako hayaji kwa yale mambo ambayo ULIMI wako ulitamka wakati wa maombi, bali yale mambo ambayo NIA (makusudi ya moyo) yako imetamka wakati wa kuomba. Sasa unaweza ukafikiri nataka kusema nini hapa ila ukitafakari kwa makini utagundua kwamba “unaweza kuomba au kunena jambo tofauti na unavyo NIA ndani yako (unavyo sikia/ona hilo jambo NDANI yako)”. Sikia, “Kwa MOYO mtu huamini hata akapata HAKI”, ticket ya kupokea inaitwa IMANI, na hukaa moyoni. Moyo wako ukinena (NIA) kwa imani UNAPOKEA majibu ya maombi yako! “Kinywa kinapitisha tu yaujazayo moyo wako”!

NIA yako ikisema KITU tofauti na ULIMI wako unachokisema, katika kuchagua kati ya haya MAWILI, Mungu anasikiliza NIA (makusudi ya moyo) yako na sio ULIMI (mambo yatokeayo akilini mwako) wako! Ndio maana Suleiman alisema “Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana.” (Mithali 16:1). Haijalishi ULIMI wako umekiri sana mangapi, je! Nia yako imejipanga sawasawa na KUSUDI la Bwana? Ukitaka MAJIBU mazuri, maandalio ya MOY O ni wewe unafanya sio Mungu, JAWABU la ULIMI kwa uombapo ni kazi ya Mungu kujibu.

Kutokana na UMUHIMU wa NIA (makusudi ya moyo) ndani ya mtu ndio maana “Mungu anachunguza moyo na kujaribu viuno”. Na katika vitu 6, naam 7 achukiavyo Mungu mojawapo ni “moyo uwazao mabaya” (Mithali 6:18). Sasa sisi tunapambana na watu kwa MATENDO au MANENO yao lakini kwa MUNGU hata ULIMI usiposema, MOYO unasema na Mungu anasikia na KUONA. Yesu akasisitiza, “sio alacho mtu hunajisi ila kimtokacho”, kwa maana kinatoka ndani ya MOYO na NIA yako inasema moyo ULICHOKUSUDIA kufanya. Kabla dhambi haijafanyika kwa jinsi ya mwili, ilianza kufanyika ndani ya moyo wako kisha UNAITIMIZA kwa MAKUSUDI ya MOYO wako (NIA).

Jifunze kudhibiti NIA yako kwa sababu hapo ndipo penye NGUVU ya kushinda au kushindwa kwako. Kama unataka kufanikwa zingatia “kulinda sana moyo wako kuliko vyote ulindavyo”. Watu wengi sana wanasahau kwamba MAWAZO ya mioyo yao yanapiga KELELE kwa SAUTI japo ULIMI haujasema kitu! Kwa Mungu hayo mawazo yanapita kama PICHA/SANAMU ndio maana Mungu anasema “umechukua vinyago na kuvitia moyoni”, yaani kule ndani yako Mungu anaweza kuona OBJECTS au PICHA japo wewe UNAWAZA tu. Yesu akasema “amwangaliaye mwanamke kwa kumtamni MOYONI mwake amezini”, sasa kila mtu anajua tamaa ni kama WAZO tu ndani ya mtu ila Mungu akiangalia kama umefuga hayo mawazo, Yeye anaona KITENDO/SAUTI/PICHA/SANAMU! Ndio maana Mungu anasema “anachukia MOYO uwazayo mabaya” kwa sabubu kwake ni VITU HALISI kuliko sisi tunavyofikiri na mara nyingi tunapuuzia tu.

Mungu alipomtokea Sulemain na kumwambia aombe kitu chochote, NDANI ya Sulemani kulikuwa na MENGI ila aliomba KUSUDI la Mungu juu ya KAZI aliyoitwa kufanya ili AMPENDEZE Mungu. Jambo hili LIKAMPENDEZA Mungu. Nataka uone kitu cha tofauti hapa. Usije ukafikiri Sulemani alikuwa na AKILI sana ndio maana ALISEMA hivyo. KUMBUKA, ilikuwa ni NDOTO tu! (1 Wafalme 3:8). Kila mtu anajua kwamba tukilala hatutumii AKILI kama tukiwa macho, sasa Sulemani aliwezaje KUOMBA kitu sahihi kwenye NDOTO? Inamaana MOYO wa Suleiman ulikuwa UKITAMANI kumpendeza Mungu (alikuwa na NIA) ambayo Mungu alipomtembelea japo ULIMI wake haukunena, NIA iliyoko ndani yake ILINENA na Mungu akajibu.

Ukisoma sehemu nyingine Bwana anasema “niko pamoja nanyi katika mipango yenu, KABLA ya kuomba mimi Bwana nitajibu, na mkiwa katika KUNENA nitasikia”! Sasa watu watakubaliana na mimi kwamba kila mmoja wetu huwa ana mipango ndani ya MOYO. Ukiwa na NIA (makusudi ya moyo) safi mbele za Mungu, hiyo MIPANGO yako katika MAWAZO yako, Mungu anasema NINASIKIA! Kabla HUJAOMBA, Mungu anajibu! Ukisoma kitabu cha Ayubu utaelewa vizuri NGUVU ya mawazo yako. Tunaambiwa Ayubu “hakumwazia Mungu kwa upumbavu”. Hili ni jambo KUBWA na Ibilisi amelificha kwa watu wengi ukiangalia ndani yao ni MAWAZO machafu tu na kuwaza vitu vya AIBU na wao hawajui kwamba mambo mawili yanatokea: i. Moyo wako unakua chukizo kwa Bwana ii. Unadhoofisha kiwango cha kupokea majibu ya maombi yako kwa maana MOYO wako unanena tofauti na ULIMI wako. Umepoteza UELEKEVU! “Na macho ya Mungu yanakimbia-kimbia diniani kote, anatafuta huo uelekevu ndani yako ili ajionyeshe mwenye NGUVU”

Petro akasema “kwa hiyo VIFUNGENI VIUNO VYA NIA ZENU, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo. Kama watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu” (1Petro1:12,13). Hapa napata picha kwamba tunaweza KUAMUA kushughulika na NIA zetu na kizidhibiti, ndio maana tunaambiwa TUZIFUNGE NIA zotu viuno na kua na kiasi!

Kuna maswali mengi huwa najiluza. Hivi Mungu akiniangalia huku ndani ANAONA nini? Watu wengi sana utawakuta wamepiga MAGOTI kwenye IBADA kanisani/sehemu mbalimbali, lakini ndani ya MIOYO yao kwa kweli WAMESIMAMA. Jiulize tu, kwamba kweli kuna UWIANO (synchronization) kati ya USEMAYO, UTENDAYO na UWAZAYO? Watu hawatuoni lakini nakwambia kuna watu MIOYO yao inavurumisha matusi kwa nguvu kama wafanyavyo wavuta bangi. Sawa, watu hawasikii lakini nakuhakikishia leo Mungu wako anasikia SAUTI! Basi AMUA leo, katika dunia hii iliyojaa UOVU na HARUFU ya UVUNDO inayopanda kwa Mungu kila siku, wewe uwe MANUKATO na KITU cha kupendeza Mungu anapo CHUNGUZA moyo wako. Jifunze KUMBARIKI MUNGU kwa MAWAZO ya MOYO wako. Ukifanikiwa hili Mungu atajibu HAJA ya MOYO wako kabla hujaomba kwa sababu NIA yako husema kwa SAUTI mbele za Mungu.

Ukitaka kujua UMEFANANAJE mbele za Mungu, angalia NAFSINI mwako, kile kitu unachokiona ndani yako NDIVYO ULIVYO mbele za Mungu, kwa maana imeandikwa "mtu aonavyo nafsini mwake ndivyo alivyo".

Roho Mtakatifu tusaidie. AMEN.

Frank Philip.

Monday, December 9, 2013

MAOMBI YENYE NGUVU!!!


Kama kuna kitu unahitaji kujua kama Mkiristo ni kuomba VIZURI. Wanafunzi wa Yesu walimwomba Bwana awafundishe kuomba kwa maana waliona wanafunzi wa Yohana wanavyoomba wakajua lazima kuna namna ya kuomba na sio kufurumuka tu na maneno bila utaratibu (Luka 11).

Kama kuna swali gumu nilikuwa najiuliza ni hili la kuomba kwa muda mrefu. Yesu anasema “KESHENI mkiomba msiingie majaribuni”, sehemu nyingine anauliza “hamkuweza kukesha nami hata saa moja tu?”. Katika Agano la Kale utaona neno “WALINZI” limetumika. Bwana anasema “Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha Bwana, msiwe na kimya” (Isaya 62:6). Sasa kwa WAOMBAJI watajua hii lugha ya “KUMKUMBUSHA” Bwana maana yake ni nini. Unapoomba sio kwamba Bwana hajui, unamkumbusha tu, ndio maana “Roho hutusaidia katika udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba kama itupasavyo”. Sio tu kwamba hatujui kuomba ila hata cha kuomba mara nyingi hatujui hadi Roho atusaidie. Kumbuka, unapoomba hutakiwi kukaa kimya hadi utakapoona majibu ya maombi yako. Hii TABIA ya KUDUMU/KUKESHA katika maombi imejirudia tena wakati Yesu anafundisha wanafunzi wake FAIDA za kuomba BILA KUKOMA. Yesu “Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa. Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu. Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu. Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu, lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima. Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu. Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao? Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?” (Luka 18:1-8). Nilinachotaka uone hapa ni aina ya UOMBAJI unaotakiwa na jinsi unapaswa kujipanga na kuwa na nguvu za kuomba kwa muda mrefu. Nitakupa moja ya SIRI muhimu za kukusadia kuwa na nguvu za kukusukuma angalau muda zaidi kidogo katika maombi.

Kuna mambo mawili nataka uone. La kwanza ni BIDII na la pili ni MUDA. “Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa BIDII. Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa BIDII mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita.”(Yakobo 5:15,16). Ukiona mtu “anajifanya” eti anatamka neno “moja tu” na mambo yanatokea, anataka kuonyesha kwamba yeye yuko juu sana na karibu sana na Mungu na miujiza ni kama tu switch ya umeme, ON/OFF matatizo kwisha! Huwa najiuliza swali hili, je! Huyu jamaa huwa anakesha na kuomba sana na sasa anamalizia tu kile alichokuwa ameomba/anomba kwa muda mrefu? Na kama sio mwombaji, je! Hii nguvu ya ON/OFF na huku ameshika kiuno imetoka wapi? Naishia hapo. Usifike mahali ukaona watumishi wa Mungu wanatumika kwa mtindo ambao hujawahi kuona ukakimbilia kusema ni PEPO. Utaingia kwenye matata MAKUBWA kama ni Mungu kweli anawatumia. Lakini pia UJUE sio kila atendaye MIUJIZA anatoka kwa Mungu.


Biblia inasema Eliya aliomba kwa BIDII! Sasa wewe unasema hapa ni kuamuru tu mambo kama ON/OFF na huna TABIA ya kukesha kwenye maombi! Kumbuka Yesu aliamuru mambo kwa mtindo huu, just ON/OFF mambo yanatokea, wanafunzi wake wakajitahidi kuiga, “IKAGOMA”! Wakamwendea wakamuuliza “mbona sisi inagoma?” Yesu akasema “mambo mengine hayawezekani ila kwa KUFUNGA na KUOMBA”. Tunasoma kwenye maandiko kwamba Yesu alikesha milimani akiomba na asubuhi anaingia hekaluni kuhudumu. Anasema “sifanyi kitu ambacho sikumwona Baba yangu akifanya!” Swali je! Aliona saa ngapi? Kama Yesu ALIFUNGA na KUOMBA, halafu wewe HUTAKI kujifunza tabia hii na unataka tu usimame kama “AFANDE” na kutoa tu ishara kwa mkono mambo yanatokea, watu wanarushwa huku na kule. Jua unakaribia MAHALI pa GUMU.

Hatua SABA za maombi zitakusaidia kuomba kwa MUDA mrefu. Kumbuka siku zote MAOMBI hayaendi bila NENO. Ukitaka kufanikiwa kuomba ni LAZIMA uwe msomaji wa NENO pia. Jipe angalau milango (chapters) 2 kwa siku. Asubuhi na jioni au muda wa kusubiri (ukiwa kwenye gari, bank, nk.) Hizi hatua SABA sio ubunifu wangu ila ni SALA ya BWANA.

Hatua ya kwanza: Liitie Jina la Bwana wa Majeshi.
Yesu alisema “mkiomba neno LOLOTE kwa Jina langu nitafanya”. Pamoja na kwamba Daudi alimkabili Goliath kwa kombeo, fimbo na jiwe, alitumia “Jina la Bwana”. Hiyo ndio siri ya ushindi wake. Sehemu nyingine Daudi akasema “hawa wanataja magari na farasi lakini mimi nitalitaja jina la Bwana Mungu wangu”. NGUVU zako za kuomba na MAFANIKIO ya uombayo yapo katika Jina la Yesu.

Sasa, unaposimama na kuanza “Baba yetu/yangu uliye Mbinguni. JINA lako LITUKUZWE”. Jiulize, litukuzwe na nani? Kama ni wewe basi anza kulitukuza jina la Bwana. Usikurupuke na kuanza tu kukemea pepo bila utaratibu hapo, No! Mtukuze Mungu kwanza. Kukemea ni hatua ya 6 huko mwisho wakati umeshajaa NGUVU. Yesu akasema “huwezi kuchukua vitu vya mwenye nguvu mpaka umemfunga kwanza”. Sasa unamfungaje mwenye nguvu wakati huna NGUVU?

Watu wanajiuliza sasa nitamtukuzaje Mungu? Sikiliza. Wana wa Israel walipovuka mto Yordani na maji yakatindika mbele yao, waliambiwa waokote mawe 12 hapo mtoni wayaweke iwe ukumbusho huko mbele kwamba “Mungu alifanya matendo makuu”. Mungu anapenda hiki kitu. Taja “matendo makuu ya Mungu” yoyote unayoyajua huko kwenye Biblia, mshangilie na kumshukuru kwa sababu ya UWEZA na NGUVU zake. Unavyozidi KUZAMA katika kutafakari na KUTAJA matendo makuu ya Mungu, taratibu utagundua kuna kitu kinatokea, unaanza kujaa CHARGE! Unavyozidi kutaja na kumtukuza Mungu, NGUVU inaongezeka na unaanza kuwa mwepesi ghafla. Hii hatua ukipita vizuri, inakupa NGUVU ya kusogea hatua ya 2.

Hatua ya pili: Ita Ufalme wa Mungu.
Hakuna ufalme usio na mfalme! Ndani ya MFALME kuna MAMLAKA na NGUVU. Sasa unapoita Ufalme wa Mungu uje, kimsingi umeagiza MAMLAKA za Mbinguni zishuke kukuhudumia wewe na mambo unayoyaombea. Ndani ya ufalme wa Mungu kuna KILA kitu unachokitaka. Mahitaji yako yote yanapatikana humo. Lakini jipange na MOYO wako vizuri maana ukiomba vitu kwa tamaa yako hupati kitu (fuatilia somo kwenye “Mafundisho ya Neno la Mungu LIKE page” lenye kichwa “Jinsi ya kumwona Mungu akijidhihirisha kwako”). Jifunze kwamba NENO la Mfalme ndio NENO la MWISHO. Huwezi kumfundisha Mfalme chakufanya kama hataki. Wewe UNAMSIHI kwamba MAPENZI yake yatimizwe . Ukifika hapo unaingia hatua ya 3.

Hatua ya 3: Jua Mapenzi ya Mungu kwa unachokiombea.
Mapenzi ya Mungu yapo katika NENO la Mungu. Huwezi kupokea kama unaomba pasipo IMANI. Na tunajua kwamba “imani huja kwa kusikia, na kusikia huja kwa NENO la Kristo”. Sasa ukiwa na Neno la Mungu juu ya “hicho” unachoombea, jua una mtaji wa IMANI. Sasa kumbuka. Unapoenda mbele za Mungu uwe kama yule mama mjane ambaye alienda BILA KUCHOKA, “akirudi-rudi kudai haki yake” (Luka 18). Ukijua AHADI zako na NENO juu ya kitu unachoomba, kaa hapo usiondoke, omba na dai ahadi yako kwa UPOLE na UNYEYEKEVU mbele za Bwana, tena bila kuchoka (usipayuke kama mtu asiye na imani). Ukirudi-rudi hadi upokee kumbuka siku zote, “Mungu huliangalia Neno lake akalitimize, na Yeye hulituma Neno kama mvua ishukavyo juu ya Nchi, Litaenda (halikosi shabaha) kwa YALE mambo aliyoliagiza na halitamrudia bure”. Hakuna faida kama unajua KITU unachoomba kipo kwenye MAANDIKO. Hapo ndio nguvu na mafanikio yako yalipo. Kama una jambo “nyeti” unataka Mungu akutendee, hakikisha unachukua kalamu na karatasi na unatafuta mistari ya KUSIMAMIA. Imani ya KUPOKEA uombacho imejikita katika UFUNUO wa hilo Neno.

Hatua ya nne: Omba mahitaji yako.
Maombi ya unachokihitaji yamejengwa kwenye hatua ya 3 hapo juu. Unapoomba RIZIKI au mahitaji mbalimbali ya mwilini na rohoni, kwako au kwa mtu mwingine, yote yamejikita katika MAPENZI ya Mungu ambayo unayapata katika Neno. Neno hilo hilo linakupa imani ya kupokea majibu ya maombi yako. Sasa kumbuka siku zote kwamba majibu ya maombi yetu yako ya aina mbili tu. NDIO au HAPANA! Jifunze kwamba hata HAPANA imo katika mapenzi ya Mungu pia. Mungu anakuwazia mema siku zote, hakunyimi kitu bila SABABU. Na imetupasa kumshukuru Mungu katika Mambo yote. Kama tumepokea au hatujapokea yote ni mapenzi ya Mungu kwetu. Ukisikia mtu anakuhakikishia kwamba “LAZIMA” jambo fulani litatokea kwa MUDA anaotaka yeye, jiulize swali hili, Je! Mungu alimhakikishia hilo jambo kwa namna hiyo? Na kama hajahakikishiwa na Mungu, jiulize tena swali hili, je! Ukiri tu ushindi NJE ya MAPENZI ya Mungu ili “kumpinda” Mungu afuate matakwa yako? Ukijua majibu, jifunze UMUHIMU wa kujipanga kwenye mapenzi ya Mungu na KUMSHUKURU kwa KILA jambo.

Hatua ya tano: Toba.
Hii hatua huwa inakuwa ya tano kama tu wewe unadumu katika maombi muda wote, ila mara nyingi sana inakuwa ya kwanza pia. Mungu ni mtakatifu, “ujasiri wa kukariba Kiti cha rehema tunaupata katika Damu ya Yesu tu” mara nyingi sana ukianza kuomba unaweza KUSUKUMWA kujitakasa. Sizungumzii hii hatua ya kujitakasa ambayo inaweza kutokea mwanzo wa maombi. Nazungumzia hii hata ya 5 ambayo sasa unazama kwenye TOBA kwa UPANA wake. Hii hatua ukiifaya vizuri itakuwa ni UFUNGUO wa matatizo mengi sana na KIPOKELEO cha maombi yako. Yesu anaagiza “kila tusimamapo kusali tusamehe ili na sisi tusamehewe”. “Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu. Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu. Lakini kama ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.]” (Marko11:24-26). Ili uweze KUPOKEA jifunze KUACHILIA watu waliokukosea/wadeni wako! Nakwambia jitahidi KUSAKA “huko” ndani yako KILA mtu ambaye ukimuwaza moyoni unasikia UCHUNGU na ukimpata, MSAMEHE na KUOMBA kwa ajili yake hadi upate UHURU. Kama bado una FUNDO ukimuwaza huyo mtu jua BADO hujavuka hapo hatua ya tano. Watu wengi sana wameshindwa “kupokea wanayoamini” (Marko 11) kwa sababu wameshindwa kuvuka hatua ya tano! Omba NEEMA ya KUSAMEHE kama inakuwa Ngumu na Yesu atakusaidia kumsamehe Mtu. Kama Yesu aliweza kuwasamehe WALIOMSULUBISHA katikati ya mijeledi, misumari, taji ya miba na kuangikwa msalabani huku anatukanwa na kutemewa mate, wakati yote yanaendelea ANAWASAMEHE na kumwomba Baba awasamehe! Yaani anapigwa, ila yeye yuko kwenye maombi! Huyu Yesu anaweza kukupa NEEMA hii ya KUSAMEHE mwenzako kwa faida yako WEWE mwenyewe KUVUKA hatua nyingine.

Hatua ya sita: Shughulika na ADUI.
Watu wengi sana wamejifunza njia moja tu ya kushughulika na Ibilisi. Kila mmoja yuko busy KUKEMEA kwa Jina la Yesu! Sawa, ni muhimu lakini nataka ujifunze Neno hili. Yesu alimwona Petro jinsi anakavyo mkana kabla hajamkana! Hakikumsumbua Yesu kwa sababu “huko” katika MAOMBI yake alikwisha omba kwamba “imani ya Petro isitindike wakati Ibilisi anampepeta kama ngano”. Yesu hakumkemea Ibilisi “asimpepete Petro ila aliomba Petro ASIANGUKE kwenye hilo JARIBU na akisimama awasaidie wenzake”. Majaribu ni package (kivunge/kifurushi) sio kitu kimoja. Sasa ukiwa na utaalamu wa kukemea kuna kitu kwenye hicho kifurushi kitakuwia kigumu. Kifurushi cha jaribu kina mambo makubwa matatu. Kwanza, jambo/kitu utakachojaribiwa nacho. Pili, kitakachotokea wakati unakutana na hicho “kitu” (kupepetwa kama ngano) na tatu, kusudi la jaribu. Ufanye nini baada ya jaribu (simama na imarisha wenzako). Hakuna mwanadamu atakemea MAJARIBU yasije maana majaribu yamo katika mapenzi ya Mungu. Unapaswa kutambua mambo haya matatu kwa makini sana: jaribu (kitu kinachokujaribu), namna ya kujaribiwa, na kusudi la jaribu. Sasa ukikazana tu na kukema huwezi kufanikiwa kila kitu kwa maana katika hilo jaribu, japo ni Ibilisi anakujaribu lakini ni Roho Mtakatifu katoa kibali kwa KIPIMO! Na huwezi kumkemea Roho Mtakatifu kwa maana ndani ya hilo JARIBU kuna KUSUDI la Mungu!

Kumbuka aliyempeleka Yesu Nyikani kujaribiwa hakuwa Ibilisi. Alipelekwa na Roho Mtakatifu! Sasa nataka ujifunze KUOMBA na sio KUKEMEA tu! Omba Mungu kwamba “usianguke majaribuni na uokolewe na yule Mwovu”. Jifunze kumshinda Ibilisi kwa Maombi sio kumkemea tu. Mara nyingi sana ukikuta mambo magumu na unawekwa kwenye “kona” badala ya kukemea pia unamwambia Ibilisi “imeandikwa”, halafu unamsomea msitari wa Biblia na Ibilisi anaachilia mara moja! Kumbuka “nao wakamshinda kwa Damu ya Mwana-kondoo na NENO la ushuhuda wao”, Neno lina nguvu ya kumshinda Ibilisi. Kwanini? Yesu ni Neno! Na tumehakikishiwa kwamba ni “aheri dunia iondoshwe kuliko yodi moja ya andiko kuondoshwa”. Sasa unaweza kuona kwamba hakuna UJANJA ibilisi anaweza kufanya kushindana na Neno la Mungu. Kwa mfano ni rahisi Ibilisi kuangamiza dunia ila sio Neno la Mungu! [japo dunia inalindwa na hakuna uharibifu wa kuangamiza dunia yote ambao utatokea kama Mungu hajaruhusu. Kumbuka agano la upinde wa mvua, nk. hii dunia imewekwa akiba..]

Hatua ya saba: Rudisha Utukufu kwa Mungu.
Hii hatua ni ya muhimu sana kama hatua nyingine zilizotangulia. “kwa kuwa wako ni Ufalme, na nguvu, na Utukufu hata milele Amen!”. Ulianza na “Jina lako Litukuzwe” na kuita “Ufalme wa Mungu uje”, sasa ukishahudumiwa na Mfalme na kuamini kwamba KILA ulichoomba kimesikika kwa Mfalme sasa lazima utoe HESHIMA kwa Mfalme! Unamalizia kwa kusema “kwa kuwa wako ni Ufalme, na nguvu, na Utukufu hata milele Amen!” Kumbuka kumshukuru Mungu kabla ya kupokea uliyoomba kwa sababu “imani ni hakika ya mambo YATARAJIWAYO na ni BAYANA ya mambo yasiyoonekana”. Mambo yatarajiwayo maana yake hujayapata ila UNAJUA yanakuja. Haya mambo yakiwa BAYANA unapata ujasiri wa KUKIRI kwa maana una UDHIHIRISHO wa NDANI kwamba umepokea ulichoomba. Usiiishie hapo, rudi-rudi kama yule mama mjane, kukumbusha hadi uhitimishe maombi yako kwa kuona sasa kwa jinsi ya mwilini jambo limetokea.

HITIMISHO

Kama utakuwa umefuata hizi hatua saba, na kujimimina utagundua kumbe saa nzima imeisha na unataka kuendelea kuomba. Fanya mazoezi halafu unipe ushuhuda. Najua hutaanza kupiga masaa tu kwa mara moja, ila angalau utavuka hatua kwa hatua.

Jambo la muhimu sana la kujifunza katika maombi ni juu ya MAHALI na MUDA. Watu wengi sana wamesindwa kuomba kwa sababu ya kufungwa na MAHALI na/au MUDA. Ukijifunza kuomba kila mahali, ukitembea, ukipika, ukifua, ukiwa darasani, ukiwa safarini, nk., utagundua unaweza kuombea mambo mengi sana kwa siku na kurudi-rudi kwa Mungu mara kadhaa “kumkumbusha jambo” kwa sababu huhitaji kujifungia mahali. Kama unaweza kuomba kwa “kunena” ni nzuri sana hasa unapokuwa katika michakato ambayo inachukua attention yako. Mtume Paulo anatufundisha kwamba tutumie mbinu zote mbili. Kuomba kwa lugha na kwa akili pia. “usikae kimya usiku wala mchana” (Isaya 62) usifungwe na muda.

Ukisikia unasukumwa KUFUNGA, fanya hivyo kwa kipimo cha mambo unayojihusisha nayo kama umetingwa na KAZI au aina ya MAJUKUMU yanahitaji sana nguvu za mwili. Ikiwezekana jipe siku malumu katikati ya wiki na kama kazi yako inahitaji nguvu nyingi za mwili jaribu kufanya maombi ya namna hii wakati wa mapumziko ya wiki, nk. Kila mtu afanye kama Roho Mtakatifu atakavyomongoza.

Neema ya Bwana wetu Yesu na izidi kwenu mnapojifunza na KUYATENDA haya. AMEN.

Frank Philip.