Showing posts with label Men. Show all posts
Showing posts with label Men. Show all posts

Thursday, December 26, 2013

NDOA YA YUSUFU NA MARIA!!!


Nimetamani sana tujifuze jambo katika ndoa ya Yusufu na Maria. Nimechukua mfano huu kama ndoa/uhusiano wowote wa mwanaume na mwanamke ambao lengo lake ni kuishi kama mke na mume.

Kuna mambo kadhaa najifunza kwa maisha ya binafsi ya Yusufu na Maria. Yusufu alikuwa mtu wa haki, mtu mwenye heshima yake na jina jema katika jamii iliyomzunguka. Aliukuwa na kazi yake ya useremala ambayo yamkini ilimwingizia kipato. Kwa upande mwingine hatuambiwi Maria alikuwa anajishughulisha na nini ila alikuwa BIKIRA, ikimaanisha alikuwa msichana aliyejitunza na kuishi maisha masafi. Hawa wawili walikuwa wachumba na walidumu katika UHUSIANO huo katika USAFI wote. Kuna mambo manne (4) nataka tuone hapa. (Luka 1)

i. Kipindi cha Giza

Wakati maisha yanaendelea, ghafla! Malaika analeta habari kwa Maria kwamba atapata mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu na atazaa mtoto wa kiume. Kwa Maria ilikuwa ni habari ngumu ila alikubali kama MTUMWA kwa Bwana wake kwa sababu alijua ni mapenzi ya Mungu. Sasa nisikilize vizuri, wakati Malaika Gabriel analeta habari kwa Maria kwamba AMEBARIKIWA, tena amebarikiwa kuliko wanawake wote, na kwamba mtoto atakayezaliwa atarithi kwenye kiti cha mfalme “Daudi”, Maria anasikai raha hadi anaenda kwa ndugu yake Elizabeth [mama yake Yohana mbatizaji], anamshangilia Mungu kwa wimbo na wanajazwa Roho Mtakatifu pale na Yohana naye anashangilia kwa kucheza akiwa huko tumboni kwa mama yake. Sasa nataka uone kitu ambacho mimi nakiona. Wakati Maria anaitwa AMEBARIKIWA kuliko wanawake wote, kwa Yusufu ilikuwa sio Baraka ila ni balaa tupu. Kwa maana binti aliyemwamini kabisa sasa ni mjamzito katika mazingira ambayo hayaelewi, wala hajawahi kusikia kitu cha sampuli hii kimetokea wapi (all was new experience), hakuna mahali pa kurejea (reference) na wala hakuna mtu anaweza kumshauri kwa maana katika ELIMU ya dunia wakati huo hakuna mahali kitu kama hicho kimeandikwa/kimetokea. Watu hawajui nini kinaendelea. [Angalizo: Sio kila jambo kwenye ndoa/uhusiano wako utapata mjuzi wa kukusaidia, jifunze kujipanga na Mungu kwa mambo ya ndoa yako]

Katika hali hii ya GIZA, Yusufu akaamua KUMWACHA Maria kwa siri! Hii ni hali ya kuchanganyikiwa ambayo wengi wanafika katika mazingira magumu katika mahusiano yao. Ghafla tu unaona hiki “kitu” ni kigumu na unaona hakuna njia tena na unajiambia “basi bwana kama ndio hivi basi mimi naacha” au “mimi nimefanya sehemu yangu ila mwenzangu amenisaliti, naachia ngazi”, au “kwani mimi ndio wa kwanza kuachika”, “kwa vile ameenda kupata mimba huko basi na mimi sioni tena haja ya kujitunza”, “kwanza nina kazi yangu na simtegemei, potelea mbali maisha yataendelea”, nk. Ni hali ya kukata tamaa. Hiki ni kipindi cha giza. Na mwili unataka kuleta majibu ya haraka (instant solutions), kukimbia na kupotelea mbali. Lakini Malaika anakuja kusema na Yusufu na kuugeuza Moyo wake. Sijui kama Yusufu alikuwa mwombaji ila tunaambiwa Mungu alisema naye, akasikia na KURUDISHA moyo nyuma. Usipo jifunza kukaa katika MAOMBI ni vigumu kuvuka hii ngazi. Hapa ni kipindi cha KUNGOJA maana unajisikia huku ndani kwamba BADO hujapata/hujafika mahali unataka. Kumbuka “wamngojao Bwana watapata NGUVU mpya”. Unahitaji Nguvu mpya kila siku kuvuka hapa. Utagundua ule “upendo wa zamani umepoa”, sasa unahitaji NGUVU mpya. Muombe Mungu akupe nguvu mpya.

ii. Kutembea katika Baraka

Mara nyingi watu wamefikiria Baraka za Mungu kwa upande mmoja tu wa kuwa na hela, majumba, magari au kufanikiwa katika mambo ya mwilini na kusahau upande mwingine. Utasikia watu wanasema “count your blessings” (“hesabu Baraka zako”). Sasa unajua huwezi kuhesabu KITU ambacho hukijui na wala hukioni. Nakwambia Leo kuna Baraka nyingi sana Mungu anatubariki na hatuwezi kuziona wala kuzihesabu kwa maana ziko kwa jinsi ya ROHONI na kwa sababu huzioni hujui kwamba UMEBARIKIWA na unabaki ukilalamika na kunung’unika kwa sababu ulishamwekea Mungu vigezo na vitu fulani kwamba “hiki kisipotokea basi sijabarikiwa bado”. Kama mambo yako “hivi” basi bado hakijaeleweka, nk. Maria alichukuwa tu kama Malaika alivyosema na “akayatia moyoni mwake” huku akijua kwamba AMEBARIKIWA kuliko wanawake wote. Kwanini aliweka moyoni mwake? Kwa maana hakuna mtu wa kawaida anaweza kuelewa hii lugha ya kupata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Akajua ni Mungu na hakuna haja ya kutoa maelezo ya ziada au kuuliza watu au kupeleka umbea. Akakaa mimya.

Hebu mfikirie Yusufu. Wakati anajua kabisa hii mimba sio yangu ila anamhudumia Maria. Wanaenda huko mbali mji mwingine kuhesabiwa na mama hajiwezi mimba ni kubwa. Yamkini huko njiani Yusufu alitembea kwa mguu wakati mkewe mjamzito yuko juu ya punda na yeye anakokota huku mbele, ila mimba sio yake! Yule mama anajifungua hapo, Yusufu anamsaidia, ila mimba sio yake! Ni mambo magumu kuelewa ila Yusufu alikaza USO kufanya MAPENZI ya Mungu kama Malaika alivyosema. Hapo hampendezi Maria, ila Mungu, kwa maana yeye alichagua kitu cha kumfanyia Maria tayari, yaani KUMWACHA kwa SIRI! Sasa huu mpango wa kubaki ni mpango mpya ambao anaambiwa na Malaika na anaamua kuutimiza mpango huu japo haelewi vizuri. Mimba sio yake! Na sio hivyo tu, hajawahi kumgusa kabisa huyu mama! Analea mimba miezi 9, akijua kabisa sio yeye!

Kumbuka sio kila kitu Mungu atafanya juu ya maisha yako UTAELEWA. Baraka nyingi sana tunapata sio BINAFSI. Mungu amelenga KUWABARIKI wengi kupitia BARAKA alizokupa. Katika kubariki wengi LAZIMA kuna UDHIA. Ndio maana Yesu alisema “hakuna mtu aliyeacha ndugu, wazazi, shamba, nk. na kumfuata asipate hivyo “vitu” mara 100 hapa duniani ila na UDHIA pia”. Watu wengi sana wanapenda BARAKA ila BINAFSI, wanasahau kwamba Mungu akishusha Baraka mara nyingi sana hulenga wengi sana kwa Baraka hiyo hiyo, na imekuwa udhia. Kwa maana sio UPENDAVYO wewe ila sasa ni kama WAPENDAVYO wengine pia kupitia Baraka hiyo hiyo. Hebu fikiri wewe ni Maria (mama wa Yesu), unaitwa MBARIKIWA kuliko wanawake wote, ila kijana hakai nyumbani, anapita mitaani KUHUBIRI vitu hata huelewi, ukimuuliza anasema anafanya MAPENZI ya Baba yake! Huku Yusufu naye haelewi pia. Ghafla! Watu wanajaa kila mahali hata hakuna muda wa kula na kuongea kama familia! Huwezi tena kusema huyu ni MWANANGU kwa maana hata yeye anasema “hawa wa hekaluni ndio mama na ndugu zangu”. Kijana anasema lugha ngumu-ngumu tu kila saa! Huku mtaani wanasema kachanganyikiwa (karukwa na akili) na wengine wanasema kijana ana pepo! Hebu fikiri hii ndio ile kitu Mungu anasema ni BARAKA!

iii. Machozi kwenye Baraka Yako

Bila shaka Maria na Yusufu walikuwa na vipindi vigumu na Yesu, japo waliitwa WABARIKIWA. Ghafla wanaambiwa wahame nchi kwa maana Herode anataka kumuua mtoto! Wanakimbilia Misri, sijui walikuwa na usafiri gani ila najua haikuwa rahisi. Hebu fikiri ghafla! unajikuta unaanza kupiga mahesabu ya kuacha kazi yako kama Yusufu kwa sababu ya hii BARAKA iliyokuja kwenye familia. Hebu fikiri wale wateja wake ambao alikuwa anawatengenezea furniture, anawaagaje? Hebu fikiri wale ndugu zake sasa hapo mtaani anawaagaje? Eti, anahama nchi! Maana sio tu hawamwelewi, ila wanamwona kachanganyikiwa pia. Hii ni BARAKA imeingia katika familia na watu wanaanza kuhangaika. Sasa ukifika mahali pa kukata tamaa jua UNAHARIBU ile Baraka ya Mungu kwa maana sasa inakuja kwa MTINDO ambao haujautarajia. Nakwambia kila mtu atakuelewa ukiamua kuitupilia mbali hiyo BARAKA isipokuwa Mungu. Lakini nakwambia ni aheri KILA mtu asikuelewe ila Mungu akuelewe inapofika kufanya MAPENZI yake.

Ndoa nyingi sana ni BARAKA katika maisha ya watu na pia Mungu amelenga hizi ndoa ziweze kuwa BARAKA kwa watu wengine. Utakuta hapo katikati kumetokea MAMBO magumu na watu wamesamabaratika na KUTOKA nje ya kusudi la Mungu. Sawa watu watakuelewe kwa maana kwa kweli “huyu jamaa” amekuwa kama kichaa kabisa, ila kusudi la Mungu ni nini? Nakwambia kuna BARAKA ambayo Mungu alitarajia watu wengine waipate kupitia NDOA yako ila sasa Ibilisi ameisambaratisha na amefuta BARAKA kubwa ambayo wengi wangeipata kupitia NDOA yako! Sio kila KUACHANA ni suluhisho hata kama mazingira yote ya KISHERIA na KIJAMII yamekaa sawasawa na kila mtu anakuunga mkono. Kumbuka Yusufu angeweza kumwacha Maria mapema tu akiwa kama mtu wa HAKI, ila alikaza uso kutimiza Mapenzi ya Mungu. Je! Unajua mapenzi ya Mungu kwa NDOA yako? Je! Kila mmoja anajua WITO wake na mlichoitiwa kufanya shambani mwa Bwana? LAZIMA kipo. Hebu fikiri hii MISUKOSUKO yote ya NDOA ya Yusufu na Maria halafu hawajui WITO wao ingekuaje? Mkijua kila mmoja alichoitiwa mtapona kwa urahisi zaidi katika VITA vya adui.

iv. Mahali pa Ushindi

Wakati Maria na Yusufu wanapita nyakati mbalimbali ngumu na BARAKA ya mtoto Yesu, inafika takriban miaka 30 ambapo sasa KIJANA anakomaa kuwa mtu mzima. Mara kijana anakuja na agenda za KUFA kwa ajili ya ULIMWENGU! Maria haelewi wakati kijana anasema “mkila mwili wangu na kunywa damu yangu mnauzima wa milele”! Pamoja na kupita hivi vipindi vizito sasa kijana anataka KUFA! Eti yeye ni kondoo wa SADAKA. Matarajio ya Maria alijua siku moja yeye atakuwa mama wa MFALME, mtu tajiri mtaani na watu wote, wakubwa kwa wadogo wanamwamkia na kumheshimu. Maria anapiga picha ya KIONGOZI mkubwa kwa jinsi ya mwili lakini KIJANA anakuja na AGENDA za kusulubiwa sasa. Yamkini nguvu ya kushinda mambo yote magumu ilikuwa kwenye matumaini kwamba SIKU MOJA huyu kijana atakuwa mfalme kwenye kiti cha Mfalme Daudi na hapa nitapumzika. Mambo yanakuja kinyume na matarajio yake japo anajua kuwa AMEBARIKIWA. Huyu mama anafuata kila hatua, anaona kijana anakamatwa, anapelekwa Golgotha kusulubiwa kama MHALIFU. Hebu fikiri hapo. Mama anamjua mwanae vizuri sana. Anajua ni mcha Mungu leo ghafla tu anasingiziwa vitu VIGUMU na sasa wamempiga vibaya damu inatiririka kila mahali na wanampeleka kumgongomelea MASALABANI. Mama analia Yesu anasema “USINILILIE mama, jililieni wenyewe!” Yesu alijua ili hii BARAKA ikamilike ni LAZIMA asulubiwe kwa maana yeye ni “Mwana-kondoo wa Mungu achukuaye dhambi za ulimwengu”. Hii ni Baraka kubwa ila haijakaa kwa namna watu wengi wataiona kama Baraka! Wengi wangelalamika na kuona ni BALAA kubwa kwenye familia! Kama unatarajia UZIMA wa Milele jifunze kusoma LUGHA za rohoni katika Baraka zako kwa maana nyingine zinakuja kwa mtindo ambao unaweza kukemea ukidhani ni Ibilisi au jaribu. (Luka 23)

Lengo la somo hili ni kutaka kukufungua macho juu ya mambo ambayo Mungu anafanya katika maisha yetu na tukumbuke kumshukuru hata kama hatuelewi kila kitu kwa maana “Mungu amekusudia mambo mema kwa ajili ya watoto wake kila siku”. Angalia usibebe roho ya KISASI kwa mambo yatakayokukuta katika MAHUSIANO kwa maana KILA uhusiano/ndoa itapita katika VIPINDI vigumu na vyepesi, vipindi vya huzuni na furaha, vicheko na vilio, nk. Angalia sana katika VIPINDI hivi usimkosee Mungu kwa sababu tu HUELEWEI mwenzako anafanya nini. Yamkini ameamua kukusaliti na wanawake/wanaume wengine na umejua. Kwa maana kama wewe ni mtu wa Mungu “hutakosa kuzijua HILA za Ibilisi na Mungu hatawaficha watu wake jambo”, na umefika mahali UMEJUA. Chunga USIMKOSEE Mungu kwa sababu mwenzako amemkosea Mungu. Uhusiano/NDOA ina mwisho ila uhusiano wako na Mungu hauna mwisho. Ukijua kwamba MATESO yako ni ya KITAMBO tu, usikubali KUPOTEZA hatma yako (mambo ya milele) kwa sababu ya mambo ya kitambo tu. Kaza uso wako kwa Mungu na kaa katika KUSUDI lake na WITO ulioitiwa ili ile BARAKA Mungu aliyoweka katika maisha yako ISIPOTELEE njiani. Tafakari yaliyo juu aliko Kristo kwa maana huku Duniani kuna ufisadi mwingi. Angalia MWISHO wa safari yako na ujitie moyo katika Bwana. Mambo yanayotokea kwenye uhusiano wako yasiujaze moyo wako hata ukakosa shukrani kwa Mungu wako.

Neema na Rehema zitokazo juu ziwahifadhi NIA zetu tangu sasa na hata milele. Bwana yu karibu.

Frank Philip.

Tuesday, March 19, 2013

#STRICTLY FOR MEN...>>>HOW TO ATTRACT A GOOD CHRISTIAN GIRL!!!

Shalom all men!
I am writing this to you because i know it is very important and sometime we don't have time and enough teaching about these stuffs in church or elsewhere,so take heed of them and God the father will surely help you in every step you make in life and this subject is very vital to single men!!

.......She's that pretty girl in your Youth Group or your church. She's really nice, and you like her a lot. Here's how to show her you like her to get her to like you back!!!

 STEPS TO GO THROUGH;

Be a guy who loves the Lord with his whole heart. Don't try to fake it, she will know. Often the thing she will find most attractive in a guy is a heart for God.

Talk to her! Yes, you've all heard this a million times, but it works! If you're in the same Youth Group, talk to her about the Bible study. Ask her if she's planning on going to the meeting next week, or if she's planning on going to the up coming worship night. That sort of thing. Those are great conversation starters!

She's a Christian girl. Chances are, she'll want a boy who will treat her like a real woman. Conduct yourself like a Christian should, by treating her with respect.

 .....Continue!

Friday, December 14, 2012

Here are Top 10 Traits Of A Real Man!!!


Shalom my readers!!!

I am so excited today to share with all men, what it takes to be a real man!!
This is very important to all people, women have to know so that somehow somewhere can help but my main concern is every man!!!
“A real man makes decisions and lives with the consequences” 

To build a great house, you need a strong foundation upon which to assemble all the other pretty things. To build a great man, you also need a solid foundation upon which to add all the other little things that set the real men apart from the stronzos. Let's not piss around, the stuff inside matters most.


Trait No. 1: A real man is strong

A real man doesn't cry, doesn't moan, doesn't complain, doesn't get sick, and doesn't need to go to the doctor every time he sneezes. A real man makes decisions and lives with the consequences. A real man accepts responsibility for his actions and his words. A real man is firm. If life is a rat, a real man will slap it and move on.

A real man is macho. A real man is tough. A real man doesn't show emotions. A real man is 
the backbone of his family and doesn't have time to be weak. If spiders scare you, you'll never be a real man.

Trait No. 2: A real man is focused

A real man knows the difference between what's important and what isn't. A real man doesn't waste time on stupidities that don't bring him any profit. Sure, there are things you can do as a hobby -- I like to shoot ducks -- but it must have a purpose. The purpose of my hobby is to improve my aim, and I don't have to tell you whether or not that's a useful thing in my line of work.

A real man focuses on power, money and family. He doesn't focus on sex. Sex comes as a result of having power, money and a wife.

Trait No. 3: A real man knows the importance of family


A real man will keep his family strong and pass on his ancestors' history and traditions. A real man knows that his children are God's gift and should be treated as such, even if he disciplines them from time to time.

A real man must also remember his other Family, his organization. In my world, both my family and my Family hold the same importance; I protect them both with all my might. If you have a Family, don't forget where your loyalties lie and who has your back when you need it.

Trait No. 4: A real man doesn't gossip

A real man follows omerta; he keeps his mouth shut. He shelters information and rations his words. A real man does not reveal more than he has to and doesn't engage in girlie talk about others. A real man doesn't discuss things he doesn't know about or people he has never met.

Trait No. 5: A real man's word is his bond

When a real man makes a promise, he keeps it. If he can't keep a promise, he doesn't give his word. A real man would rather die than break his word. A real man knows that his words are as powerful as his actions, and that they must be taken at face value. That is why he rations them (see above).

Trait No. 6: A real man strives to be a role model

A real man respects himself and others at all times, unless, of course, he has been disrespected. A real man sets an example for his disciples, and especially for his children. I never bring my work home, so my children only know me as their father and not as a waste management executive. You should do the same; a real man sets the tone for his children and keeps them from discovering that he has weaknesses.

Trait No. 7: A real man makes his own fortune

A real man doesn't settle for handouts or charity when it comes to his personal fortune. A real man isn't satisfied with papa's money. He spits on Lady Luck and decides his own destiny. A real man who inherits goods from his forefathers takes his inheritance and turns it into 10 times what it was.

Trait No. 8: A real man doesn't look like a woman

A real man doesn't have piercings and long hair, and he doesn't shave his chest. Manicures, however, are acceptable. Massages from female attendants are also tolerated. A real man knows that, outside of his barber, all his personal hygiene needs must be taken care of by a woman.

A real man has at least three suits (with a mandatory pinstriped one) that cost more than a roomful of escorts. A real man wears a suit/Smart at least three times a week. Any man who doesn't know how to tie a tie should hand in his class immediately.

Trait No. 9: A real man keeps his house in order

Have you ever been inside the boss’ house? There ain’t no pizza boxes sitting around, there ain’t no undershirts on the floor, and there sure as hell ain’t no unpaid bills being used as beer coasters. No ruler can rule over a territory if he isn’t already the master of his own home.

This means you lazy pinheads out there need to stop using machismo as an excuse to live like a bottom-feeder; keep your sty spotless, keep your documents in order and -- listen up on this one -- clean your freaking suits.

Trait No. 10: A real man can defend himself

You know what’s missing in the world today? Leaders who have had to fight their way to the top. No joking, look at the head of any business that’s circling the toilet bowl, and I’ll show you a boss whose parents' power and money kept him from ever learning things the hard way.

Every successful capo has been on the wrong end of a beatdown -- be it with words or be it with a set of A. Testonis. But those future capos got up again and again, until they knew how to stand their ground -- and that, my students, is when you can start to climb the ladder.

THANK YOU FRIENDS!!

THIS IS PER NORMAL DEGREE LEVEL, I MEAN I HAVE JUST TRIED TO EXPLAIN SOCIALLY AND NOT SPIRITUALLY,SO ONCE YOU ARE DONE WITH THIS HOMEWORK THEN START WORKING ON YOUR SPIRITUALITY STATUS!!!


YOU ARE VERY WELCOMED FOR COMMENTS!!!