Sunday, March 24, 2013

Kutoka Madhabahuni>>>...."MJUE SANA MUNGU ILI UWE NA AMANI NA MAFANIKIO"

MJUE SANA ILI UWE NA AMANI NDIVYO MEMA  YATAKAVYOKUJIA(01)

SHALOOOOOOM!!
NAWASALIMIA WOTE KATIKA JINA LA YESU KRISTO!
NINATUMAINI UNAENDELEA VIZURI NA MUNGU BADO NI MWEMA SANA MAISHANI MWAKO!
LEO JPILI YA TAR 24 APRIL 2013, NINAWALETEA NENO TOKA MADHABAHUNI MWA BLOG HII NA Mwalimu FREDY E.CHAVALA!
MISINGI YAKE INAJENGWA KATIKA MAANDIKO HAYA

Ayubu 22:21..."Mjue sana Mungu ili uwe na Amani ndivyo Mema yatakavyokujia."

UTANGULIZI;
#Neno hili liko wazi sana na yamkini umewahi kusoma hata maandiko haya mara nyingi sana,lakini ukijua undani wa maneno yake yamkini ukajengeka zaidi,
Neno "MJUE"- Lina misingi miwili M-JUE,M-inakuonyesha msisitizo wa Agizo, na JUA ni hali ya kujifunza ama kufahamu jambo kwa juhudi au kwa bidii, Kwa hiyo MJUE maana yake Tumia juhudi kufahamu zaidi kuhusu Mungu na maandiko hayakuishia hapo,bali yamesema "Mjue sana", maana yake mbali na msisitizo wa neno MJUE bado unasisitizwa SANA....
#Na zaidi maandiko yanasema..."ili uwe na  AMANI",maana yake Kwa kadri unavyomjua ndivyo unavyozidi kuwa na AMANI.....
#Na mwisho maandiko yanasema.."Ndivyo MEMA yatakavyokujia"... na hii inadhihirisha kuwa Ukiwa na Amani ndio unaweza kuona mafanikio/mema!

Kwa Ujumla andiko hili lina maana hii;
KWA KADRI UNAVYOJITAHIDI KUMJUA MUNGU>>>>NDIVYO UTAZIDI KUWA NA AMANI>>>>NA KWA KADRI UNAVYOZIDI KUWA NA AMANI,NDIVYO UTAZIDI KUFANIKIWA!!!

SHULE YA NENO;
Unaweza kuwa unajiuliza sasa kumjua Mungu ndio kufanyaje...Kumjua Mungu ni kufahamu Yeye ni nani kwako,kwanini amekuumba na anakutaka ufanye nini ukiwa duniani,zaidi anataka ufanye nini kwa wanadamu wenzako na Ulimwengu ufanye nini,na hapo utajifunza Vipao mbele vya Mungu,Amri na makatazo yote,ahadi,zawadi na malipo ya kila............

.......ITAENDELEA!!!


3 comments: