Wednesday, November 7, 2012

VIGEZO VYA UBORA/HESHIMA VYA MTUMISHI WA MUNGU HUSUSANI MWANA-SANAA (01)



VIGEZO VYA UBORA/HESHIMA VYA MTUMISHI WA MUNGU HUSUSANI MWANA-SANAA (01)

(Qualities of honor of a Christian Servant especially Christian Artist (Celebrity))
*****************************************************************************************

Shalom!!
Ninayo heshima kubwa sana kwenu na kwa Mungu na moyo wangu umejaa shukrani mno, ahsante kwa kupata muda wa kujifunza na kuyatafakari yale yafaayo kutafakariwa!!

Nimekuwa na maswali mengi sana kichwani mwangu na mara kadhaa niwewahi kuwahoji watu mbalimbali, kuwa….HIVI KWA MFANO UKIANDAA TUKIO FULANI MAHUSUSI NA UKATAMANI MMOJA WA WASANII(WA SANAA YEYOTE ILE) AWE MGENI RASMI, UTAMCHUKUA NANI? KWA NINI? NA KAMA UKIMPATA HUYO, NI KWA NINI HUYO NA SIO MWINGINE?

Bila shaka umeshtuka na kichwani mwako bado una haha na yamkini hata nadharia zako huziamini amini vile, lakini yote haya ni kwasababu gani?
Je hakuna msanii mwenye hadhi ya kuwa mgeni rasmi? Je wasanii au watu maarufu wanajua thamani yao? Je wanajua kujiweka sawasawa mbele ya jamii?
Nimeona nianzie hap oleo na nitaendelea kuzungumza mambo muhimu ya kuzingatia kwa mtumishi wa MUNGU anapokuwa maarufu au star kwa lugha ya leo!!

HATUA ZA MSINGI
Kipaji mtu hupewa na Bwana lakini maboresho ya kipaji huletwa na juhudi ya mwenye kipaji, yaani namaanisha huwezi kung’aa katika kipaji chako kama hujaweka juhudi za kutosha katika kipaji hicho, hivyo zifuatazo ni hatua za msingi kwa mtu yeyote;

a.     KUJITAMBUA

Kila mtu anapaswa kujitambua vema, yeye ni nani? Anataka nini katika maisha na anatamani kufika wapi? Zaidi nini makusudi ya Mungu kumleta hapa duniani!!(HILO SI SOMO PANA SANA LAKINI HAPO MBELENI TUTAKUJA KUCHAMBUA KWA KINA SANA)






b.     KUJIVUMBUA
Mtu akishajitambua sasa anakuwa na heshima ya kuwa mtu na sasa kuna uwezo ambao Mungu ameuweka ndani ya kila mtu kipekee na uwezo huo ndio unaotoa mwelekeo hata wa kusudi la maisha yako hapa duniani. Sasa unapaswa kupitia hatua hii ya kujivumbua, hapa mtu anajua kwa hakika yeye ana kipaji Fulani na hicho amepewa awe makini kwa manufaa yake na jamii nzima(PIA HAPA TUTAKUJA KUCHAMBUA KWA KINA SANA HAPO MBELENI)

c.      KUJIFUNDISHA

Neno kujifundisha limesimama kwa niaba ya maneno MAFUNZO, yaani ukishajivumbua sasa unajitaji elimu,utaalamu na ujuzi bora uliopangiliwa vema sana juu ya hicho kipaji chako, watu wengi sana wakishajivumbua kuwa wao ni wazuri katika jambo Fulani basi hawafanyi jambo lolote zaidi kuvimba kichwa na kuanza kuishi maisha ya maigizo na unakuta hata hawavumi kivile kwasababu hawajawekeza kwenye kujifunza(HAPO MBELENI TUTACHIMBA NDANI KABISA NA KTOA MIFANO HAI)

d.     KUJIJARIBU
Hii ni hatua ambayo mtu anaanza kujihudhurisha mbele ya kadamnasi na kujaribu kuonyesha kile anaweza kufanya na hapa ni kama elimu wa vitendo, kwa maana hapa mtu anakuwa bado havijui vingi lakini anafanya vile ajuavyo na kufungua masikio kwa ajili ya maoni na mafunzo zaidi, hapa wengi huruka na kudhani wameshakuwa watu maarufu na ndio maana unaweza kuona mtu anakuja kwa kasi sana kasha akapotelea matopeni!!!
N.B; HATUA HII HUENDA IKIBOREKA NA KUBOREKA KADRI  MTU ANAVYOJITAHIDI KUONGEZA JUHUDI KATIKA KUJARIBU NA KUJARIBU TENA(WAZUNGU WANASEMA…PRACTISE MAKES PERFECT)

e. KUJIHUDHURISHA RASMI SASA

Baada ya muda wa kutosha sasa unafika wakati wa kuwekwa wakfu na kuanza kufanya na kuishi kipaji chako, hapo unakuwa bidhaa na unakuwa mshauri na mwalimu wa wengine wanakuja katika njia moja au katika tasnia uliyoipitia, na wakati huu na wewe pia huendelea kukua na kama ukizingatia misingi ya kwanza basi wewe kwenye sanaa uko salama….







HUU ULUKUWA NI MSINGI TU WA UTANGULIZI NA….
TUTAENDELEA KUCHAMBUA KIDOGO KIDOGO, MPAKA HAPO NITAKAPOMALIZA KIINI CHA UJUMBE HUU!!

KARIBU SANA!!!
King Chavala
+255 713 883 797

.........TUTAENDELEA!!!

No comments:

Post a Comment