Wednesday, July 24, 2013

YOUTH PRAYER CAMP (3KAVU) KUFANYIKA BOKO TAFES CENTRE!!!

SHALOM!
NINAWASALIMIA KATIKA JINA LA YESU LIPITALO MAJINA YOTE!
NAAMINI MKO VIZURI NA MNAENDELEA VEMA NA MAISHA YENU YA KILA SIKU; KWA KADRI UNAVYOAHANGAIKA KUOGA,KUVAA,KULA NA KUSOMA KILA SIKU,IMEKUPASA KUTIA JUHUDI ZAIDI KATIKA KUIMARISHA KIROHO CHAKO KILICHO MSINGI WA KILA KINACHOONEKANA. NA NDIO MAANA KUNA MAHALI TUNAONA YOHANA AKIMWAMBIA GAYO.....MPENZI NAOMBA UFANIKIWA KAMA ROHO YAKO IFANIKIWAVYO.....HII INA MAANA MAFANIKIO YOTE YA NJE NI SAMBAMBA NA MAFANIKIO YA ROHO YAKO.

KWA KUTAMBUA UMUHIMU HUO WA KUONGEZA UKARIBU WAKO NA MUNGU KWA KUUTIISHA NA KUUTAABISHA MWILI HUU WENYE MAROROSO YASIYOKWISHA, HUDUMA YA VIJANA, THE BRIDGE ILIYO CHINI YA KANISA LA VICTORY CHRISTIAN CENTRE TABERNACLE (VCCT) IMEANDAA KAMBI MAALUM YA MAOMBI YA KUFUNGA KWA SIKU TATU KWA AJILI YA VIJANA WOTE WANAWIWA KUMTAFUTA MUNGU KWA BIDII.

KAMBI HIYO ITAANZA SIKU YA IJUMAA SAMBAMBA NA MAOMBI YA KUFUNGA KUANZIA IJUMAA(WENGINE WANAANZA ALHAMISI) MPAKA JUMAPILI AMBAPO TUTAFUNGUA PAMOJA BAADA YA IBAADA YA KWANZA KANISANI PALE VCCT, MBEZI BEACH A.

MAOMBI HAYA NI YA KUFUNGA KWA SIKU TATU KAVU MFULULIZO NA HAKUNA GHARAMA ZA KIINGILIO ZAIDI YA KULIPIA MALAZI AMBAYO NI TSH 5000/= KWA SIKU MOJA(HIVYO KILA MSHIRIKI ATADAIWA 10,000/= KWA CAMP HIYO).MAOMBI HAYA YATAFANYIKA KATIKA KITUO KINACHOITWA "BOKO TAFES CENTRE|

KWA WALE WANAOENDA TUTAKUTANA IJUMAA JIONI PALE VCC-VICTORIA TAYARI KWA AJILI YA SAFARI YA PAMOJA MAJIRA YA SAA MOJA NA NUSU JIONI.

MSISITIZO WA MAOMBI HAYA NI "KUFINYANGWA NA BWANA KWA UPYA" ILI UWEZE KUTEKA BARAKA ZAKO KWA NGUVU!!

MUHIMU KUBEBA BIBLIA,NOTEPAD,KALAMU,CHANDARUA,SHUKA,SABUNI,MSWAKI, SURUALI NA KANGA( KWA WASICHANA)MAFUTA NA NGUO ZA KUVAA JUMAPILI KANISANI (MAANA SAFARI ITAKUWA NI MOJAKWAMOJA TOKA CAMP MPAKA KANISANI)

KUTOKA UPANDE WOWOTW WA JIJI,BILA KUJALI KANISA WALA DHEHEBU LAKO, MRADI UNAMWAMINI MUNGU KUPITIA YESU KRISTO,BASI USISITE UNAKARIBISHWA SANA,KWA MAELEZO ZAIDI/KUJIANDIKISHA AU KUCHANGIA WANAENDA BASI WASILIANA NA WAANDAAJI KUPITIA;

0754 710 410/0713 883 797/0713 209056
IMETOLEWA NA THE BRIDGE YOUTH MINISTRIES,VCCT!

@IMEDHAMINIWA NA GOSPEL STANDARD BASE Blog.

Wednesday, July 17, 2013

HUYU NI"RAPHAEL JOACHIM LYELA" MTUMISHI AMBAYE ALIYEKAA MIEZI 11 TUMBONI NA KUISHI MTAANI KAMA CHOKORAA!!!

SHALOM WANDUGU!!
NINAWASALIMIA WOTE KATIKA JINA LA BWANA YESU KRISTO!
NINAAMINI KILA MMOJA YUKO POA NA ANAMTUKUZA KRISTO,HUSUSANI WEWE UNAYESOMA HAPA SASA HIVI!
LEO KIPEKEE NINAWALETEA HISTORIA YENYE USHUHUDA MZITO WA MAISHA YA MTUMISHI WA MUNGU AMBAYE BADO NI KIJANA INGAWA ni BABA na ANA WATOTO WENGI SANA TANZANIA NZIMA, HUYU NDIO MBEBA MAONO NA MUANZISHAJI WA HUDUMA IITWAYO "YKM-YOUTH KINGDOM MINISTRIES...Jesus Up!" 

Yamkini na wewe umewahi kupokea message nyingi sana toka katika huduma hii na yamkini umesaidika sana sana....Mtumishi huyu amekuwa anajighulisha sana na maisha na maendeleo ya vijana....yamkini umewahi kumuona chuoni au shuleni aukanisani kwako akihudumu ama umewahi kumsikia redioni akiongea au umewahi kusoma kitabu chake au umewahi kununua CD zake za mafundisho,basi binafsi nilipata fursa ya KUMHOJI KAKA HUYU MWENYE HISTORIA YA KIPEE YENYE KUOGOPESHA LAKINI INAYOTIA MOYO SANA MAANA SASA ANAMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII!

(Basi yafuatayo ndio mazungumzo yetu yalivyokuwa na maelezo yote yameandikwa kama mwenyewe alivyojieleza)

UTAMBULISHO RASMI;
Jina Kamili: Raphael Joachim Lyela

Familia;Nimemuoa Angela Godfrey Raphael
Asili;Mfipa Original toka Rukwa-Sumbawanga
Huyu ni Mtoto wa  3 kati ya 6 wa familia ya Mzee J.Lyela.



TUAMBIE HISTORIA YAKO FUPI YA KIELIMU;
".....Darasa la Kwanza Shule ya Msingi Mabatini-Mwanza, pia Mwimbi kule Sumbawanga vijijini nilikomalizia darasa la saba. Nilisoma O Level shule tatu tofauti, nilianza Kipoke Sec school kule Tukuyu nikasoma mpaka form two, nikahamishiwa Lutengano sec school nikasoma mpaka form three, sikumaliza form three yote kwasababu niliibiwa ada ya shule kwa kichupa cha dhahabu so nikaambiwa sitaki shule na hivyo nikaachia form three. 
Nikakaa mwaka mzima home, nilipoambiwa kurudi shule niligoma kurudia tena form three na kwahiyo sikumalizaga form three but nikaamua kusoma masomo ya jioni katika shule ya Iyunga Technical Sec ambako nilimalizia form four na kufeli kwa kupata division 111.24. 
Nikapangakiwa A Level Kigonsera High school, Songea kwa mchepuo wa HGL, nikasoma term moja, kasha nikahamia Sangu high school Mbeya nilikomalizia form six. Nilimaliza na kufeli kwa kupata div 1.8, nikaenda chuo kikuu Mzumbe nilipomaliza Bachalor ya Publick Admin-Human Resources Management."



HUYU KAKA KWA SASA NI MTAALAMU WA;Human Resources Management, NA ZAIDI NI Certified Facilitator
Anafanya Kazi KAMA:Partnership Facilitator,Human Resources Specialist na shirika la Compassion International Tanzania kwa mwaka wa tano tu mpaka sasa.

(Hapa nilimuuliza uzoefu au mambo mengineyo katika maisha yake,nae akafunguka kama hivi)


MAMBO MENGINEYO YA KIPEKEE KUMHUSU RAPHAEL;

".....Nilizaliwa baada ya miezi 11......mama alikufa nikiwa na miaka 10......niliishi mtaani kwasababu baba yangu alikuwa akinipiga sana toka nikiwa mdogo.
........nilianza kunywa gongo na kuvuta sigara na bangi, nilikuwa mwizi toka nikiwa mdogo.......nilishasafiri toka Mwanza mpaka Sumbawanga nikitafuta ndugu zangu bila kulipa nauli na kukaa njaa bila kula wala kunywa kwa siku kadhaa......nimeshauza mkaa na kuvua samaki ili nipate pesa za kujikimu......nilijifunza matusi toka nikiwa mdogo kutoka na jamii niliyokulia.......nimeshakuwa Mkatoliki, Mrastafari, Shahidi wa Yehova na pia Mbudha lakini mwisho nikakutana na Yesu nikiwa mwaka wa kwanza chuo kikuu pale Mzumbe........nimeshahudhuria makongamano mengi sana ya vijana ndani na nje ya Tanzania.........nilianza kuandika hadithi za kwenye magazeti nikiwa O level, nimeshaandika kitabu kimoja na vingi vinaandaliwa, ninaimba na nina nyimbo nyingi tu, ni mtunzi wa nyimbo, mwandishi wa vitabu, motivational speaker hasa kwa vijana"

MAONO NA NDOTO ZANGU;
 
".....Mwaka 2003 nilipata mawazo ya kuwasaidia vijana, nilianza kwa kuandika mawazo yangu kuhusu mahusiano kwenye karatasi na niliandika mawazo yangu ya kwanza yenye kichwa cha UTOPIAN PARADISE nikielezea maisha ya Furaha katika ulimwengu wa UTOPIA, mwaka 2007 nilianza huduma ya kutuma msg kwa vijana 24 kuwakumbusha umuhimu wa kuomba na kusogea karibu na Mungu wao,hi indo huduma ya Youth Kingdom Ministries iloiyopata shape mwaka 2012, YKM ni huduma inayowafikia vijana na njia ya kutuma msg kwa simu na mpaka sasa tunawafikia vijana zaidi ya 4000 kila zinapotumwa, YKM ina viongozi wa mkoa katika mikoa 15 mpaka sasa yaani DAR,MWANZA, MOROGORO, ARUSHA,LINDI,MTWARA,MARA, IRINGA, MBEYA,KILIMANJARO,KIGOMA,RUVUMA,DODOMA,SINGIDA,TABORA. Vijana ndio madhabahu yangu"
NILIMUULIZA SWALI,MPAKA SASA UMEATHIRIJE ULIMWENGU WAKO?
"....Mpaka sasa nimefikia vijana zaidi ya 4000 Tanzania nzima na Kenya pia, nina vijana zaidi ya mia moja waliojitoa kutumika katika huduma kwa simu zao toka maeneo mbali mbali, makazini, shuleni, vyuo, mtaani etc"


NI NINI UNACHOTAMANI KUKITIMILIZA MAISHANI MWAKO?

"....I want to die empty, kuachilia kila kilichowekwa na Mungu ndani yangu ili kutimiza kusudi la Mungu juu yangu, juu ya kizazi changu, juu ya taifa langu na juu ya familia yangu. Natamani kuona vijana wamesimama katika kanuni za Ufalme wa Mungu na kuleta mabadiliko yadumuyo katika kila eneo analopatikana Kijana. Natamani siku moja nipotelee kwenye biblia. Natamani nitumike kwa kiwango ambacho hata wakati wangu wa kulala utakapofika basi utukufu wa Mungu udhihirike kwa utukufu wa Omega. Sina chaguo linguine zaidi ya kumtumikia Mungu."

KIPEKEE NINAMPENDA SANA KAKA HUYU NA  TANGU NIMEMFAHAMU NINAJIVUNIA moyo wake,HAKIKA NI CHOMBO IMARA CHA BWANA!!
 
MAISHA YAKE YALICHANGAMSHA SANA NA KUNIKUMBUSHA MAISHA YANGU NILIYOPITIA NA MENGI YA MAMBO NI KAMA TUNASHARE....NA KWA SASA HUWA ANAANDIKA MASOMO MBALIMBALI KWA AJILI YA VIJANA KATIKA MADHABAHU HII KATIKA UKURASA UITWAO "Youth Platform"

Naamini umemfahamu mtumishi huyu vema,ama umemfahamu baba yako vema(kwa wewe ambaye ni mtoto) na zaidi naamini hautaacha kutembelea madhabahu ili ujifunze kila leo maana hapa kuna mengi sana ya kujifunza!!!

Na King Chavala-MC
Hotline; +255 713 883 797
*Jiunge uwe follower wa blog kisha utoe maoni yako au maswali yako!!!

....HERE IS THE BIOGRAPHY OF REV.EDMUND KIVUYE FROM BURUNDI AND STORY OF HIS MINISTRY IN AFRICA!!!

Shalom my reader!
Today i am presenting a very important minister of God from Burundi,Bishop Rev.Edmund Kivuye, whom is highly called "Apostle" or "Arcbishop" and much more but he just want to be adressed as Just a "Reverent" or "pastor" of

Eglise Vivante de Jésus Christ du Burundi



EXECUTIVE SUMMARY OF INTRODUCTION;
Edmond KIVUYE (born October 15, 1966) is the International Apostolic Leader of Eglise Vivante de Jesus Christ (Living Church of Jesus Christ)in Burundi, Rwanda, D.R.Congo, and Senegal. It is a non-denominational church, and one of the fastest growing church in Burundi with more than 8000 members in the city of Bujumbura, the capital city of Burundi.
Children doing dance during Children Conference
Pastor Edmond KIUVYE's sermon given at the Eglise Vivante  are broadcasted live every Sunday and Wednesday on the church website. His preachings are also broadcasted for 30 mins once a week on the national TV (RTNB). He is the only burundian Pastor on the Burundi National Television so far. He is also on a Christian television in burundi, everyday of the week and once a week on a secular television based in Burundi. The media outreach goes also on the national radio twice a week in Kirundi and Swahili. (National Radio heard in the whole country, also in Rwanda, D.R.Congo, and Tanzania) Pastor Edmond KIVUYE through the church he organizes annual conferences where people around the country and neighboring countries come and meet for 3 great days. Conferences like "Abagabo b'iteka" (Men of honor) Men conference. "Nyina Wanje" (Woman) Ladies conference. "Urwaruka rufise intumbero" (Youth with a purpose) Youth conference. "Banyene Ubwami" (Their's kingdom) Kids conference.
Pastor Faith ministering
Pastor Edmond Kivuye is also the International Director of African Revival Ministiries  A humanitarian organization, which has as goal to proclaim, teach, and demonstrate the Kingdom of God trough building hospitals, schools, orphanages, and many more to help people. The African Revival Ministries is located in Burundi, Rwanda, D.R.Congo, Senegal, and the UK.

LIFE HISTORY 
Rev.Edmund and Pastor Faith Kivuye


On October 15, 1966, Edmond KIVUYE was born in Ngagara, Bujumbura. Raised in a big family, and he was the first one to get saved and was honored to lead most of his brothers and sisters to the Lord.
Shortly after graduating in Mechanical Engineering (Heavy duty engines)in June 1987 he was called to go into ministry under the leadership of his uncle David NDARUHUTSE who was the founder of the African Revival Ministries and Eglise Vivante. These two worked together since the beginning of the ministry till when Pastor David NDARUHUTSE went to be with the Lord after a plane crush in the mountains of D.R.Congo in September 1997.

Before that the Lord led Pastor David NDARUHUTSE to pass on the mantle of leadership to Pastor Edmond KIVUYE. At the time, no one undesrtood what was happening, till after the plane crush. Then Pastor Edmond KIVUYE took over.
God Kept on blessing the ministry even though it was going trough problems, the church kept on growing almost every 2 months, so it was with the African Revival Ministries.

HIS FAMILY;

When he was 23 in 1989, he married Faith Kin Teustin. They have two children together (Henoc, and Anne). Pastor Faith Kivuye also helps his Husband in the ministry and God uses both of them in a mighty way around the world preaching the word of God.

ABOUT HIS MINISTRY;
Pastor Edmond's sermons are broadcast nationally through the church TV and Radio program "Igihe C'Impemburo" which means times of refreshment on the national radio and television. His sermons are helping people county wise and even in around the world trough Live streaming, DVDs, video's on YouTube, Facebook, and Twitter... 
Church Auditorium

Under the leadership of Pastor Edmond Kivuye, the Eglise vivante de Jesus Christ helps many people by paying their school fees when they no longer can afford it, feed the hungry, and helping them getting medical care. More of these good works are done through African Revival Ministries  still under Pastor Edmond leadership, where they have two schools in the capital city of Burundi, Bujumbura. One of them is the only english speaking school in the country which follows the oxford curriculum (King's School International). Still in the capital city ARM (African Revival Ministries) have two hospitals, one which is manly surgical and has the only X-ray which you can have the result right after they have taken you the X-ray picture.
In Burundi ARM has other project like one to help HIV positive people who are hopeless and cannot afford the medicine. In this center, they just don't give them, food and medicine, but they also encourage them with the world of God. ARM has a project which helps the pygmies in the country side. This tribe is one of the three but the least which is only 1% of the population. They teach them to read and write using the bible, ARM has also built a village for them and recently a clinic, so that they can be treated equally as other tribes.

After the war which took place in Burundi, many children were left without parents due the birth of CRIB (Children rescue in Burundi) orphanage. This orphanage have more than 300 children raised in a God fearing environment and also speaking English. In 2004 near the border on Burundi and DRCongo happened a genocide which took many Congolese refugees lives. At that time the first thing ARM did was to open an orphanage and taking all the children, because they did not have where to stay, the orphanage was called "New Hope Center", to give a new hope to those innocent children.
In Rwanda, ARM and Eglise Vivante helps people with HIV by giving them hope and encouraging them with the word of God. They do support them with medicine and food. They also helps different orphans by paying for their school fees. Eglise Vivante Have more than 50 different churches around Rwanda.
Praise Team

In DRCongo, ARM and Eglise Vivante does continue helping people mainly on the side of Uvira where a big population of "Banyamulenge" still living in the middle age of not having water, House, school, to get what to eat, women have to work for almost 3 weeks to get only a meal of 3 weeks. After seeing the need in that Region, Eglise Vivante and ARM under the leadership of Pastor Edmond Kivuye, they decided to build houses for the population, school, orphanages. With the help of some engineers from Canada, they were able to provide electricity in some houses using the great water falls that are around the mountain of Uvira. The Eglise Vivante and a number of church members bought machine so that women won't have to spend 3 weeks making ready a 5 day meal, but now they produce more for the family and also get time to rest and being with their families
In Senegal, ARM and Eglise Vivante are doing a great work knowing Senegal as a Muslim country, when people receives Christ as their savior, they are persecuted, so ARM established a refugee center for women, because women are persecuted to the point of being Killed. So that refugee center receives them and help them by giving them job... ARM do have another center for young boys called "Talibe" These young boys, are not sent to school by their parents so that they won't learn about the western education. They send them to the Muslim school to learn about the Koran, their teachers send them during the day to beg for money (without their parents knowing) and there is a certain amount they have to reach if they don't they are severely punished. ARM takes those young boys, first teach them about the word of God and put them in schools.


HOPE YOU ARE CHALLANGED BY THIS YOUNG SUSSESSFUL BURUNDIAN BISHOP COMPARED TO OTHER BISHOPS; IF HE IS AN OVERSEER OF 300 CHURCHES WITH A LOT OF OTHER COMMUNITY SERVICES PROVIDED TO THE COMMUNITY AND IN WHICH HIS EXCELLENCY THE PRESIDENT OF BURUNDI DO ATTEND SERVICES REGULARLY AND SOMETIME MINISTER TO THE CHURCH AT THE HEAD QUARTER.

PERSONALLY I KNEW THIS PASTOR WHEN HE CAME TO TANZANIA AND MINISTERED TO VICTORY CHRISTIAN CENTRE TABERNACLE FOR FOUR DAYS; HONESTLY I CAN TESTIFY THAT THIS MAN OF GOD IS LOADED WITH LIFE REALITY AND FUTURE ORIENTED PRINCIPLED SERMONS AND THAT IS WHAT HAS PUSHED ME TO FIND MORE INFORMATION ABOUT THIS MAN OF GOD!! IF REAL WISH TO HEAR ABOUT THIS MINISTER THEN JUST GOOGLE THE WILL GET HIM IN WEBSITES,TWITTER,BLOGS,YOUTUBE and to mention a few!!

MAY GOD ALMIGHTY BLESS YOU ALL!!!

Written by
King Chavala
(MC/Stand Up Comedian)
+255 713 883 797
*From different trusted sources of informations

SHEREHE ZA ISHARA NA MIUJIZA ZINAENDELEA PALE JIJINI TANGA!!


HABARI NJEMA KWA WAKAZI WA JIJI LA TANGA,PALE SHULE YA USAGARA
KUANZIA SAA TISA MPAKA KUMI NA MBILI JIONI KILA SIKU.
17-21 JULAI 2013


Sunday, July 14, 2013

Kutoka Madhabahuni;......."CHOCHOTE KILICHOKUMEZA AU KUMEZA VITU VYAKO,KINAENDA KUTAPIKA!!!!

SHALOM!!
NENO LA MUNGU KUTOKA MADHABAHUNI LEO LINATOKA KATIKA KANISA LA VICTORY CHRISTIAN CENTRE,MBEZI BEACH A,DSM....mahali ambapo Mtumishi wa Mungu Askofu Rev. EDMUND KIVUYE from BUJUMBURA,BURUNDI amekuwa na Kongamanoi la siku mbili mahali hapo na Somo hili limekuwa ni Hitimisho la Kongamano hilo.
NAAM KARIBU UJIFUNZE NENO TOKA MADHABAHUNI!!
******************************************************************************
SOMA BIBLIA
<<Yona 2:10.......Na Mungu akamwambia yule samaki,na samaki akamtapika Yona nje ya bahari!>>

Mtumishi alianza kwa kusema....Chochote kilichokumeza lazima kitakutapika!

"AMEN" ni neno dogo sana lakini ni ufunguo mkubwa sana wa utayari wako kupokea muujiza wako....ni sawa kabisa na Ufunguo mdogo sana unaweza kufungua mlango mkubwa sana,hivyo ni muhimu kutumia ufunguo huo AMEN kila mara maishani mwako.

Unapokaa kwenye kiti lazima ujue kuwa huo ni muujiza na hivyo ukikaa kanisani lazima utegemee miujiza na wewe mwenyewe ni muujiza;Ukiristo sio maisha ya mazoea lakini ni maisha ya ufunuo na ufumbuzi kila siku.

USHUHUDA;
Mchungaji alisema mwaka 1992 mke wake aliwahi kuumwa na alipopelekwa hospitali akapimwa na kuambiwa kuambiwa ana matatizo ya nyongo na ni lazima afanyiwe upasuaji ili apone,lakini mchungaji akasema hapana mke wangu hawezi kupata kisu....basi kulikuwa na na kongamano fulani huko Uingereza naam,mchungaji akaomba ampeleke mke wake huko,na dakatari akamruhusu Mchungaji aende nae.....na huko kwenye kongamano Mchungaji/Muhubiri wa Kihindi alizaliwa Mombasa na anayeishi Amerika akasema KUna mwanamke mmoja hapa aliwahi kuumwa miaka kadhaa iliyopita na sasa anaumwa tena na kuna dhamira ya kumfanyia upasuaji....sasa amepona sasa.....Basi mchungaji huyu ambaye mke wake ni mgonjwa akaruka na kusema,AMEN!......Lakini wakati wa shuhuda mara mwanamke mmoja akapita na kusema amepona(na mchungaji akashangaa na kusema haiwezekani muujiza huu asiwe mke wangu)....basi akamtafuta sana mke wake na akamkuta amepumzika kwenye gari na basi yule mchungaji akamsimulia mke wake habari ile yote na mke wake akasema tu.....AMEN!......Na hata sasa ni mzima na hakuwahi kufanyiwa upasuaji tena,yaani muujiza wake ulipokelewa na neno,Amen tu!

Ikiwa yona aliyekuwa mkorofi lakini baada ya kuomba ndani ya tumbo la samaki,Mungu alimwamuru samaki amatapike....vipi wewe uliye mwana mwaminifu?

IKIWA UNATAKA MAMBO YAKO YALIYOMEZWA NA SAMAKI(ADUI).....BASI....OMBA!!!
Na kwa wale waliomba basi NA WASUBIRI!!

Usiruhusu watu kukukatisha tamaa kwa maneno na vijembe....eti oooh ulikuwa wapi kuomba awali hata unamsumbua Mungu sasa? au na wewe unafunga kweli? na mengineyo mengi!.....IKIWA MZAZI HAWEZI KUMFUKUZA AU KUMZIRA MTOTO AKIKOSA,HATA AKOSEE NAMNA GANI,VIPI KUHUSU MUNGU BABA WA MBINGUNI.....UKIWA TAABUNI HATA RAHANI BASI USIACHE KUKIMBILIA KWA MUNGU TU!!

Mtu hawezi kukusaidia ukiwa ndani ya tumbo la samaki ila Mungu tu aliyekuumba wewe na huyo samaki aliyekumeza.....Naam unaweza kuchangua Kumwamini Mungu Au ukaacha kumwamini kabisa na hata Biblia unaweza kuiamini au ukaacha....basi hata maishani mwetu kumejaa machaguo....Uzima na kifo ni kuchagua pia.....kufanikiwa na kushindwa ni  uchaguzi wako mwenyewe......kuzaliwa sio uchaguzi wako bali kufa masikini ni uchaguzi wako......basi watu wameamini kuwa kuwa MASIKINI NDIO UTAKATIFU!!....eti kwasababu maandiko yanasema Heri Masikini....lakini Biblia imesema Heri masikini wa roho na sio hali!

Maamuzi yako yanategemeana sana na habari ulizonazo....maana kile ulichonacho ndio kinakuongoza kufanya maamuzi!

USHUHUDA;
Kuna wakati mchungaji amewahi kushambuliwa na watu mbalimbali kwenye TV na redio na akaitwa kujibu tuhuma....lakini mchungaji akasema siji kujibu lolote maana sijisikii kujibu chochote,lakini kama inawezekana naomba dk 5 tu  nihubiri na wenye vyombo vya habari hivyo na wenyewe wakakataa kabisa....basi mchungaji akakaa kimya kabisa kwasababu hata bosi wake hakujibu kitu aliposhambuliwa (ingwa alijibu mara chache na kukaa kimya mara nyingi sana)
.....Na baada ya miaka minne sasa ni Mchunhaji pekee wa kanisa la mahali pamoja anayehubiri kwenye TV ya serikali na huo ni ushuhuda mkubwa na wengi wamejaribu kutafuta nafasi ya kuhubiri kwenye TV hiyo na wameshindwa maana mafanikio SIO PESA BALI NI MAAMUZI!!

Yakobo aliona mavazi ya Yusufu ambayo yalikuwa yamepakwa damu ya mnyama na ndugu zake na akaamua kuamini kuwa  Yusufu ameliwa na wanyama wakali.....hivyo unaweza ukaamua KUAMINI KWA YALE YANAYOONEKANA AU KUAMINI KWA YALE HALISIA(NENO LA IMANI)

KUMBUKA;
......Mara zote UONGO hupanda kupitia LIFTI lakini UKWELI hupanda kupitia NGAZI,japo ukweli huchelewa kufika juu lakini hufika na Uongo hupanda kwa spidi na kuanguka ni hivyo hivyo tu.

SASA AMUA KUAMINI KATIKA KWELI NA SIO UNACHOKIONA,MAANA UHALISIA UNAWEZA KUWA SIO SAHIHI SANA ILA KILA KWELI NI HALISI!!!

Kama samaki alikuwa na masikio ya kusikia,basi na wewe unaweza kuongea na chochote na kikakusikia....anza sasa kusema na nyumba yako au gari yako(iambie iache kula hela yako ya gereji kila siku),sema na chochote na uamini naam utapata.

ACHA KUWA MWANA DIPLOMASIA MBELE ZA MUNGU,HEBU KUWA HALISI!!
Acha maneno ya kuzungukazunguka JUST GO STRAIGHT TO THE POINT!!!

MFANO;
Hivi kama batimayo baada ya kuita YESUUUUUU MWANA WA DAUDI NIHURUMIE...na baada ya Yesu kusimama,vipi kama Batimayo angeaanza Samahani sana Yesu,samahani nimekusumbua na najua una kazi nyingi lakini........naamini Yesu asingemuelewa,lakini alisema tu NATAKA KUONA TENA!!!

STORI 1;Mungu yupo na unaweza kuamini kuwa yupo na ukamwamini au ukaacha kabisa kumwamini.....Ni kama vile watu wasemavyo oooh hakuna Mungu kabisa,maana kama angekuwepo magonjwa na matatizo yasingekuwepo.....lakini hiyo sio kweli maana uwepo wa watu walio na manywele mengi sana huko mitaani haimanishi hakuna vinyozi....NA MUNGU NDIO HIVYO ALIVYO!

STORI 2;Na kuna wakati RAIS amewahi kutembelea magereza na kuwakuta wafungwa watatu na mheshimiwa akaamua kuuliza ili apate kujua nini hasa watu hawa wako gerezani..KWANINI UKO HAPA..basi majibu yao yalikuwa hivi;
Mfungwa 1; Mimi niko hapa kwasababu mimi sio wa hapa na watu hawa wameamua kunionea...mmmh okey(Rais akajibu)
Mfungwa 2; Mimi ni masikini ndio maana niko hapa,kama  ningekuwa na fedha nisingekuwa hapa...
na Mfungwa 3; Akasema mimi hapa nilipo ni kwa neema tu....basi Raisi akashtuka na kuuliza kwanini,ina maana unafurahia kuwa hapa?....basi yule mfungwa akasema Kweli nimefanya mengi sana mabaya na ilinipasa kufa vibaya lakini nimehurumiwa na kuwekwa hapa.....Basi Raisi akapendezwa na mfungwa huyu na kuamuru aachiliwe ili asije akawachafua wale wasafi....NA HUO NDIO ULIKUWA UHURU WAKE!!!

NA SASA NATAMANI UJUE KUWA UNAWEZA KUAMINI UWEPO WA MUNGU,UNAPASWA KUAMINI NENO NA KUCHAGUA KULIAMINI MAISHANI MWAKO....KUWA HALISI NA MWAMINI BWANA BILA MASHAKA! UWE MUWAZI MBELE YA BWANA.....AMUA KUSAMEHE KILA ALIYEKUKOSEA,NAAM CHAGUA KUTII AMRI HIYO YA MUNGU YA KUSAMEHE!!!

CHOCHOTE KILICHOKUMEZA,NA KIKUTAPIKE SASA....KATIKA JINA LA YESU,AMEN!!!

(Na ibaada hiyo iliisha kwa maombi mazuri sana na Mungu pia akusaidie na wewe uwe na wakati wa kuomba mara tu baada ya kusoma neno hili....tamka neno la msamaha kwa waliokukosea naam sema na samaki huyo aliyemeza mambo yako!!!...endelea....kuomba......)

KARIBU TENA NA TENA,UJIFUNZE NENO LA MUNGU HAPA!!

Imeandikwa na
Na Mwl.Fredy E.Chavala
+255 713 883 797

Wednesday, July 10, 2013

GOSPEL SINGERS' BREAKFAST......Episode IV!

IKIWA WEWE NI MUIMBAJI BASI HII INAKUHUSU MNOOO!!!
NJOO UJIFUNZE UANDISHI WA NYIMBO NA UPANGILIAJI WAKE!!
CHAI NI BUREE KWA WOTE!!!!

Wednesday, July 3, 2013

JUKWAA LA KIOO......MTAMBUE "ORIDER NJOLE" MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI MCHAPAKAZI ASIYE NA MAKUU!!!

Shalom!
Leo ninayo furaha kumleta kwenu mwimbaji wa nyimbo za injili wa kipekee sana kati ya waimbaji wa nyimbo za injili Tanzania!

#PART ONE#

Huyu dada ni mwenyeji wa Iringa(Mhehe aliyeokoka hivyo laana ya kujinyonga haiko juu yake tena) lakini anaishi na kufanya kazi zake Dar es salaam ingawa huzunguka sana Tanzania kwenye mikutano na semina mbalimbali kama mshiriki na mhudumu pia!

Mwimbaji huyu ana moyo wa tofauti sana, kwani mara nyingi kwenye mikutano ya injili kwa mfano wakati ule wa SHEREHE ZA ISHARA NA MIUJIZA...na mingine mingi nimemuona akiwa mhuhudumu tena anayejituma,tofauti na waimbaji wengi...wakishatoa album na kujulikana basi wanajiona mabosi hivyo hawawezi kufanya usafi,kushiriki kazi kanisani wala kuhudumu!!

Orider Njole ni mdada mtaratibu na mcheshi alijishusha,huduma yake iko mbele na sio fedha maana kuishi kwake kunatokana na Baraka ambazo Mungu ameziachilia kupitia kazi ya mikono yake!!

Kama wewe ni msikilizaji sana wa Wapo basi utakua umeshamsikia maana zaidi kupigwa sana nyimbo zake hapo pia amewahi kualikwa mara kadhaa kwenye kanisa la BCIC.

Nikiwa naandaa mikutano au makongamano hata vikao vya waimbaji wa injili amekuwa mbele kusaidia,kusambaza habari kwa wenzake na hata kutoa mchango wake wa fedha ili kufanikisha shughuli hizo!

Orider Njole Amesomea uhudumu wa afya lakini baada ya kuona kama hailipi alienda kusomea Uandishi wa habari....hivyo ni mhudumu wa afya  na kwasasa anaendesha duka lake la Dawa baridi lakini pia ni muandishi wa habari ambapo amefanya na anaendelea kufanya na vyombo kadhaa vya habari hapa nchini....wakati huo anaendelea kuimba nyimbo za injili na ni kiongozi kanisani kwake!

Orider anapenda pia kuwa na muda na watoto,hususani watoto yatima...na kwa hakika anapenda sana watoto na anampenda sana mwanae.

Akiwa nyumbani hujishughulisha na kilimo hata kama ni kidogo na upande mwingine ni mdada anayependa sana michezo!

Ametoa album yake ya kwanza ya nyimbo za injili iitwayo "DUNIANI TUWAPITAJI" yenye nyimbo 8 na tayari ameshafanya video ya album hiyo....na nyimbo zake hususani huo unaobeba album unaendelea kufanya vizuri kwenye redio nyingi na hata video yake pia inafanya vizuri na video hiyo ilifanyika maeneo ya Iringa!!
 MWIMBAJI HUYU NI MFANO WA KUIGWA NA WAIMBAJI WENGINE NA UNAWEZA KUWASILIANA NAE MOJA KWA MOJA KWA MIALIKO YA KIHUDUMA AMA UNAWEZA KUPITIA ANUANI YA BLOG HII!!

Mara nyingine tukipata nafasi ya kuhojiana nae basi tutakuletea habari kwa kina kuhusu mwanadada huyu,karibu sana!!!

.........ITAENDELEA!!!!(Part 2 itahusu mahojiano kati ya mwandishi na Orider Njole)....USIKOSE!!!

Na King Chavala-MC
Hotline; 0713 883 797