Sunday, July 14, 2013

Kutoka Madhabahuni;......."CHOCHOTE KILICHOKUMEZA AU KUMEZA VITU VYAKO,KINAENDA KUTAPIKA!!!!

SHALOM!!
NENO LA MUNGU KUTOKA MADHABAHUNI LEO LINATOKA KATIKA KANISA LA VICTORY CHRISTIAN CENTRE,MBEZI BEACH A,DSM....mahali ambapo Mtumishi wa Mungu Askofu Rev. EDMUND KIVUYE from BUJUMBURA,BURUNDI amekuwa na Kongamanoi la siku mbili mahali hapo na Somo hili limekuwa ni Hitimisho la Kongamano hilo.
NAAM KARIBU UJIFUNZE NENO TOKA MADHABAHUNI!!
******************************************************************************
SOMA BIBLIA
<<Yona 2:10.......Na Mungu akamwambia yule samaki,na samaki akamtapika Yona nje ya bahari!>>

Mtumishi alianza kwa kusema....Chochote kilichokumeza lazima kitakutapika!

"AMEN" ni neno dogo sana lakini ni ufunguo mkubwa sana wa utayari wako kupokea muujiza wako....ni sawa kabisa na Ufunguo mdogo sana unaweza kufungua mlango mkubwa sana,hivyo ni muhimu kutumia ufunguo huo AMEN kila mara maishani mwako.

Unapokaa kwenye kiti lazima ujue kuwa huo ni muujiza na hivyo ukikaa kanisani lazima utegemee miujiza na wewe mwenyewe ni muujiza;Ukiristo sio maisha ya mazoea lakini ni maisha ya ufunuo na ufumbuzi kila siku.

USHUHUDA;
Mchungaji alisema mwaka 1992 mke wake aliwahi kuumwa na alipopelekwa hospitali akapimwa na kuambiwa kuambiwa ana matatizo ya nyongo na ni lazima afanyiwe upasuaji ili apone,lakini mchungaji akasema hapana mke wangu hawezi kupata kisu....basi kulikuwa na na kongamano fulani huko Uingereza naam,mchungaji akaomba ampeleke mke wake huko,na dakatari akamruhusu Mchungaji aende nae.....na huko kwenye kongamano Mchungaji/Muhubiri wa Kihindi alizaliwa Mombasa na anayeishi Amerika akasema KUna mwanamke mmoja hapa aliwahi kuumwa miaka kadhaa iliyopita na sasa anaumwa tena na kuna dhamira ya kumfanyia upasuaji....sasa amepona sasa.....Basi mchungaji huyu ambaye mke wake ni mgonjwa akaruka na kusema,AMEN!......Lakini wakati wa shuhuda mara mwanamke mmoja akapita na kusema amepona(na mchungaji akashangaa na kusema haiwezekani muujiza huu asiwe mke wangu)....basi akamtafuta sana mke wake na akamkuta amepumzika kwenye gari na basi yule mchungaji akamsimulia mke wake habari ile yote na mke wake akasema tu.....AMEN!......Na hata sasa ni mzima na hakuwahi kufanyiwa upasuaji tena,yaani muujiza wake ulipokelewa na neno,Amen tu!

Ikiwa yona aliyekuwa mkorofi lakini baada ya kuomba ndani ya tumbo la samaki,Mungu alimwamuru samaki amatapike....vipi wewe uliye mwana mwaminifu?

IKIWA UNATAKA MAMBO YAKO YALIYOMEZWA NA SAMAKI(ADUI).....BASI....OMBA!!!
Na kwa wale waliomba basi NA WASUBIRI!!

Usiruhusu watu kukukatisha tamaa kwa maneno na vijembe....eti oooh ulikuwa wapi kuomba awali hata unamsumbua Mungu sasa? au na wewe unafunga kweli? na mengineyo mengi!.....IKIWA MZAZI HAWEZI KUMFUKUZA AU KUMZIRA MTOTO AKIKOSA,HATA AKOSEE NAMNA GANI,VIPI KUHUSU MUNGU BABA WA MBINGUNI.....UKIWA TAABUNI HATA RAHANI BASI USIACHE KUKIMBILIA KWA MUNGU TU!!

Mtu hawezi kukusaidia ukiwa ndani ya tumbo la samaki ila Mungu tu aliyekuumba wewe na huyo samaki aliyekumeza.....Naam unaweza kuchangua Kumwamini Mungu Au ukaacha kumwamini kabisa na hata Biblia unaweza kuiamini au ukaacha....basi hata maishani mwetu kumejaa machaguo....Uzima na kifo ni kuchagua pia.....kufanikiwa na kushindwa ni  uchaguzi wako mwenyewe......kuzaliwa sio uchaguzi wako bali kufa masikini ni uchaguzi wako......basi watu wameamini kuwa kuwa MASIKINI NDIO UTAKATIFU!!....eti kwasababu maandiko yanasema Heri Masikini....lakini Biblia imesema Heri masikini wa roho na sio hali!

Maamuzi yako yanategemeana sana na habari ulizonazo....maana kile ulichonacho ndio kinakuongoza kufanya maamuzi!

USHUHUDA;
Kuna wakati mchungaji amewahi kushambuliwa na watu mbalimbali kwenye TV na redio na akaitwa kujibu tuhuma....lakini mchungaji akasema siji kujibu lolote maana sijisikii kujibu chochote,lakini kama inawezekana naomba dk 5 tu  nihubiri na wenye vyombo vya habari hivyo na wenyewe wakakataa kabisa....basi mchungaji akakaa kimya kabisa kwasababu hata bosi wake hakujibu kitu aliposhambuliwa (ingwa alijibu mara chache na kukaa kimya mara nyingi sana)
.....Na baada ya miaka minne sasa ni Mchunhaji pekee wa kanisa la mahali pamoja anayehubiri kwenye TV ya serikali na huo ni ushuhuda mkubwa na wengi wamejaribu kutafuta nafasi ya kuhubiri kwenye TV hiyo na wameshindwa maana mafanikio SIO PESA BALI NI MAAMUZI!!

Yakobo aliona mavazi ya Yusufu ambayo yalikuwa yamepakwa damu ya mnyama na ndugu zake na akaamua kuamini kuwa  Yusufu ameliwa na wanyama wakali.....hivyo unaweza ukaamua KUAMINI KWA YALE YANAYOONEKANA AU KUAMINI KWA YALE HALISIA(NENO LA IMANI)

KUMBUKA;
......Mara zote UONGO hupanda kupitia LIFTI lakini UKWELI hupanda kupitia NGAZI,japo ukweli huchelewa kufika juu lakini hufika na Uongo hupanda kwa spidi na kuanguka ni hivyo hivyo tu.

SASA AMUA KUAMINI KATIKA KWELI NA SIO UNACHOKIONA,MAANA UHALISIA UNAWEZA KUWA SIO SAHIHI SANA ILA KILA KWELI NI HALISI!!!

Kama samaki alikuwa na masikio ya kusikia,basi na wewe unaweza kuongea na chochote na kikakusikia....anza sasa kusema na nyumba yako au gari yako(iambie iache kula hela yako ya gereji kila siku),sema na chochote na uamini naam utapata.

ACHA KUWA MWANA DIPLOMASIA MBELE ZA MUNGU,HEBU KUWA HALISI!!
Acha maneno ya kuzungukazunguka JUST GO STRAIGHT TO THE POINT!!!

MFANO;
Hivi kama batimayo baada ya kuita YESUUUUUU MWANA WA DAUDI NIHURUMIE...na baada ya Yesu kusimama,vipi kama Batimayo angeaanza Samahani sana Yesu,samahani nimekusumbua na najua una kazi nyingi lakini........naamini Yesu asingemuelewa,lakini alisema tu NATAKA KUONA TENA!!!

STORI 1;Mungu yupo na unaweza kuamini kuwa yupo na ukamwamini au ukaacha kabisa kumwamini.....Ni kama vile watu wasemavyo oooh hakuna Mungu kabisa,maana kama angekuwepo magonjwa na matatizo yasingekuwepo.....lakini hiyo sio kweli maana uwepo wa watu walio na manywele mengi sana huko mitaani haimanishi hakuna vinyozi....NA MUNGU NDIO HIVYO ALIVYO!

STORI 2;Na kuna wakati RAIS amewahi kutembelea magereza na kuwakuta wafungwa watatu na mheshimiwa akaamua kuuliza ili apate kujua nini hasa watu hawa wako gerezani..KWANINI UKO HAPA..basi majibu yao yalikuwa hivi;
Mfungwa 1; Mimi niko hapa kwasababu mimi sio wa hapa na watu hawa wameamua kunionea...mmmh okey(Rais akajibu)
Mfungwa 2; Mimi ni masikini ndio maana niko hapa,kama  ningekuwa na fedha nisingekuwa hapa...
na Mfungwa 3; Akasema mimi hapa nilipo ni kwa neema tu....basi Raisi akashtuka na kuuliza kwanini,ina maana unafurahia kuwa hapa?....basi yule mfungwa akasema Kweli nimefanya mengi sana mabaya na ilinipasa kufa vibaya lakini nimehurumiwa na kuwekwa hapa.....Basi Raisi akapendezwa na mfungwa huyu na kuamuru aachiliwe ili asije akawachafua wale wasafi....NA HUO NDIO ULIKUWA UHURU WAKE!!!

NA SASA NATAMANI UJUE KUWA UNAWEZA KUAMINI UWEPO WA MUNGU,UNAPASWA KUAMINI NENO NA KUCHAGUA KULIAMINI MAISHANI MWAKO....KUWA HALISI NA MWAMINI BWANA BILA MASHAKA! UWE MUWAZI MBELE YA BWANA.....AMUA KUSAMEHE KILA ALIYEKUKOSEA,NAAM CHAGUA KUTII AMRI HIYO YA MUNGU YA KUSAMEHE!!!

CHOCHOTE KILICHOKUMEZA,NA KIKUTAPIKE SASA....KATIKA JINA LA YESU,AMEN!!!

(Na ibaada hiyo iliisha kwa maombi mazuri sana na Mungu pia akusaidie na wewe uwe na wakati wa kuomba mara tu baada ya kusoma neno hili....tamka neno la msamaha kwa waliokukosea naam sema na samaki huyo aliyemeza mambo yako!!!...endelea....kuomba......)

KARIBU TENA NA TENA,UJIFUNZE NENO LA MUNGU HAPA!!

Imeandikwa na
Na Mwl.Fredy E.Chavala
+255 713 883 797

No comments:

Post a Comment