Wednesday, January 2, 2013

HERI YA MWAKA MPYA 2013 NA KARIBU TENA GoStaBa Blog KWA AWAMU NYINGINE TENA!!!

Shalom!!

Nawasalimia watu wote katika Jina la Yesu lipitalo majina yote!!! Naamini kila mmoja ni mzima wa afya, zaidi wewe unayesoma hapa sasa!!

HONGERA SANA KUCHAGULIWA KUONA MWAKA 2013, NINATAMBUA SIO KWA UJANJA,AKILI AU UWEZO WETU BALI NI KWA NEEMA YA MUNGU!!

Mambo muhimu ya kuzingatia ni haya;

1.UMERUHUSIWA KUONA MWAKA MPYA 2013, SI KWASABABU UNA STAHILI SANA KULIKO WALIOTANGULIA, HIVYO NI NAFASI YAKO YA KIPEKEE KUJENGA UKUTA MAHALI PALIPOBOMOKA ILI SASA UWEPO UKAMILIFU NDANI YAKO.

2. UMEBAHATIKA KUINGIA MWAKA 2013 KWASABABU HUJAMALIZA KAZI ZAKO, HIVYO USIJARIBU KUISHI KIHASARA HASARA,HAKIKISHA UNAISHI MAKUSUDI YA MUNGU KILA SIKU!

3. MUNGU AMEKUACHA UISHI TENA MWAKA HUU 2013 KWASABABU ANA AGENDA NA WEWE, NI MUHIMU SANA KUOMBA ILI UJUE BWANA ANA AJENDA GANI NA WEWE,HILI NI MUHIMU KUMSIKIA MUNGU VIZURI MAANA KILA MTU ANA AJENDA TOFAUTI NA MWINGINE!!

Yamkini umepokea nabii nyingi sana kwa habari ya mwaka huu mpya,lakini  nataka nikwambie hakuna hata mmoja utakaotimia maishani mwako kama ukiwa nje ya network ya Mungu,inakupasa kubaki nyumbani kwa Bwana,kuomba sana, Kula neno la Mungu na kumwamini Mungu bila shaka yeyote ndani yako!!

INAWEZEKANA MWAKA HUU UKAWA MZURI SANA KWA WENGINE ILA UKAWA MGUMU SANA KWAKO,YOTE YANATEGEMEANA NA IMANI YAKO NA KUJIPANGA KWAKO MBELE ZA MUNGU!!!

Kipekee ninamshukuru Mungu kuingia mwaka mpya na ninaamini nina mengi sana ya kufanya katika Ulimwengu huu,ahsante kwa technolojia kunifanyia madhabahu ya kanisa hili huru la mtandaoni,naamini umeendelea kujifunza mengi na ni matarajio yangu kuwa utajifunza mengi zaidi!!

KWA NIABA YA TIMU NZIMA YA BLOG HII,NINAOMBA NIWATAKIENI KILA LAKHERI NA MAFANIKIO MENGI KATIKA MWAKA HUU WA 2013 NA KARIBU TUENDELEE KUJIFUNZA NA KUKUA KIROHO KWA KUSUDI TU LA KUUJENGA UFALME WA MUNGU HAPA DUNIANI,AMEN!!

Na 
Fredy E.Chavala
President-Chavala Ideas Platform
Box 34048
Dar es salaam
+255-(713/753)-883 797
lacs.project@gmail.com

No comments:

Post a Comment