Thursday, June 20, 2013

HERE ARE FINAL TOUCHES IN TORONTO,CANADA READY FOR BISHOP ZACHARY KAKOBE TO PREACH!!!

FOR THREE DAYS....IN TORONTO,CANADA,THERE WILL BE HEAVY AND VERY STRONG ANNOINT OF JESUS CHRIST WITH MAN OF GOD, BISHOP ZACHARY KAKOBE.

EVENT SCHEDULE:

Thursday June 20 - from 7pm

Friday June 21 - from 7pm

Saturday June 22 - from 5pm

Sunday June 23 - from 5pm

BIBLICAL SIGNS AND WONDERS WITH PRAISE AND WORSHIP, WORSHIP TO BE LED BY DON MOEN, MARTHA MUNIZZI AND ON THE STAGE ALSO THERE WILL BE KRYSTAAL WHO ARE RESIDING IN CANADA!!

OFFICIAL ACCOMMODATION: TORONTO AIRPORT MARRIOTT HOTEL - RESERVATIONS FILLING UP FAST

Toronto Airport Marriott Hotel is the official accommodation for the Bishop Zachary Kakobe Toronto Miracle Healing Crusade and Restoration Retreat. The Toronto Miracle Healing Crusade which will be held at the Rexall Centre (Tennis Stadium) from June 20 - 23, 2013; will be coupled with the Restoration Retreat which will be held at the Toronto Airport Marriott Hotel, as per the following schedule:
Pastors' Breakfast Meeting With Bishop Kakobe
Subject: Church Growth and Revival Impartation Prayer
Day/Date: Friday June 21, 2013
Time: 10.00 AM

All Singles Breakfast With Bishop Kakobe
Subject: Breakthrough Prayer
Day/Date: Saturday June 22, 2013
Time: 10.00 AM

The Couples Covenant Dinner With Bishop Kakobe
Subject: Breaking the Circle of Divorce
Day/Date: Monday June 24, 2013
Time: 07:00 PM

You are strongly encouraged to arrange your accommodation at Toronto Airport Marriott Hotel and enjoy Bishop Zachary Kakobe International Ministries special discount rates. Book your Hotel rooms online 24/7, directly with Toronto Airport Marriott Hotel, 901 Dixon Road, Toronto, Ontario M9W 1J5 Canada. Reservations are filling up fast so make your reservation today.

HERE ARE SOME PICTURES BEHIND THE SCENE; 
PEOPLE AT WORK

THE STAGE




WE BELIEVE THIS CRUSADE WILL BE VERY POWERFUL!!
GOSPEL STANDARD BASE IS WISHING YOU ALL THE BEST, BISHOP ZACHARY KAKOBE WITH THE WHOLE MINISTIRIAL TEAM!!!

King Chavala-MC/Comedian
+255 713 883 797

Monday, June 17, 2013

HABARI NJEMA SANA KWA WAKAZI WA JIJI LA MWANZA.....SHEREHE ZA ISHARA NA MIUJIZA!!!!

WAKAZI WA MWANZA MPOOOOOOOOO
 
Haya tena ni SHEREHE ZA
ISHARA NA MIUJIZA
Pamoja na Mtumishi wa Mungu wa Kimataifa
Mwinjilisti toka Sweden - Rev Johannes Amirtzer
Pamoja na Band yake ya SOS PRAISE TEAM Toka Sweden
 
Wakati wako ni SASAAAA!!
Walete Wagonjwa na wenye shida mbalimbali nao wataombewa na kupokea MUUJIZA wa KIMUNGU Kutoka kwa Mtumishi na Mpakwa mafuta wa Mungu Johannes Amirtzer - TOKA SWEDEN
Ni VIWANJA VYA FURAHISHA - MWANZA
JUNI 19 HADI 23, 2013
SAA 9:30 ALASIRI HADI 12:30JIONI KILA SIKU
 
HIIII SI YA KUKOSA MWALIKE NA JIRANI YAKO
 
GOSPEL STANDARD BASE BLOG INAWATAKIA BARAKA NYINGI ZA BWANA NA MAFANIKIO TELE,HALELUYA!!!!

Thursday, June 13, 2013

TANZANIA GOSPEL SINGERS' BREAKFAST....3rd Episode ON 15th June 2013!!!

SHALOM!
HABARI NJEMA KWA WAIMBAJI WOTE WA NYIMBO ZA INJILI TANZANIA HUSUSANI WAISHIO MKOA WA DAR ES SALAAM AU WATAKAOKUWEPO JIJINI TAREHE HIYO,MNAKARIBISWA TENA KWENYE CHAI MAALUM YA ASUBUHI ITAKAYONYWEWA JMOS YA TAR 15/06/2013 KUANZIA SAA MBILI ASUBUHI MPAKA SITA NA NUSU MCHANA,

CHAI HII NI MAALUM SANA KWANI INAWAPA FURSA WAIMBAJI KUONANA,KUFAHAMIANA,KUSAIDIANA,KUSHAURIANA NA KUANZISHA MASHIRIKIANO,LAKINI JUU YA YOTE KUJIFUNZA NA KUOMBA PAMOJA....AWAMU HII YA TATU MWALIMU WA MUZIKI NA MWANAMUZIKI SAMUEL YONAH ATAKUWA AZINGUMZA KWA KINA KUHUSU MUZIKI KITAALAMU ZAIDI!


HAKUNA KIINGILIO CHOCHOTE,WEWE UKIPATA HABARI HII MWALIKE NA MWIMBAJI MWEZIO MJE WOTE!
HAIJALISHI UNAIMBA INJILI KWA MTINDO UPI...IWE HIP HOPE,RnB,BAND,SEBENE,MDUMANGE,PRAISE NA WORSHIP,KWAYA AU UNAIMBA BINAFSI BASI HII NI NAFASI YAKO!!

TUKIO HILI MUHIMU LINALETWA KWENU NA "CHAVALA IDEAS PLATFORM" KUPITIA BLOG HII YA KIKRISTO "GOSPEL STANDARD BASE" KWA UDHAMINI MKUBWA WA
King Chavala-MC
Praise Power Radio
Mitambo Solution
Christian Bloggers
Na wengine mmoja mmoja wanaoendelea kuchangia mawazo yao!!!

Kwa maelezo zaidi piga 0713 883 797

ITAMBUE NAFASI YAKO KAMA KIJANA ILI ULETE MABADILIKO KATIKA MAISHA YAKO NA JAMII KWA UJUMLA 02


SHALOM TENA WASOMAJI WANGU!!
BADO TUNAENDELEA KUJIFUNZA KAMA VIJANA....

Kama nilivyosema katika sehemu ya kwanza, ni muhimu sana kwako wewe kama kijana kujua nafasi yako katika maisha yako, ujue pia Nafasi yako katika familia yako, uelewe umuhimu ulionao kwa jamii inayokuzunguka na zaidi sana taifa lako.
Umuhimu wako haupatikani kwa kujitazama kwenye kioo na kudhani wewe ni muhimu, ni jambo linalohitaji kuwekeza katika ufahamu sahihi ama kujitambua sawa na vile Mungu alivyokusudia.

Ufike mahali uishi maisha yenye malengo na utambue thamani yako ili usinunuliwe na vitu vyenye thamani isiyolingana na wewe. Hapa inahitaji kujenga mtazamo utakaokusaidia kuwa thabiti katika maamuzi yako, ili ujenge msimamo wenye nidhamu katika maneno, mawazo na matendo yako.

 Jumla ya haya yote inahitaji kujitambua, na sasa tuendelee na maana ya kujitambua maana ni kujitambua tu ndiko kunaweza kukusaidia kujua Nafasi yako na kusimama katika zamu yako na kuleta mabadiliko uliyopangiwa na Mungu wako.

Maana ya Kujitambua
“Kujitambua ni hali ya kuwa na ufahamu au uelewa (kujua) wa kutosha juu ya maisha yako kwa ujumla pamoja na mazingira yanayokuzunguka na hivyo kukufanya uishi maisha yanayofanana au kulingana na kusudi la Mungu kwako, uishi katika ubora wa maisha yanayolingana na kiwango cha ufahamu ulionao au kiwango cha kujitambua kwako kutegemeana na nguvu ya taarifa unazopata” 
 Kijana aliyejitambua, ukimsikiliza maneno yako hutatia shaka kwamba yuko thabiti na hata ukiangalia matendo yake utaona ulinganifu wa ayasemayo na ayatenda. Kijana yoyote hawezi kujitambua mpaka amekutana na ufahamu sahihi ulio juu ya yote anayoyafahamu, aone kupungukiwa kwake kwasababu hajafahamu mambo ya msingi katika maisha yake. 

Juu ya yote ni lazima wewe kama Kijana ujue kuwa ipo sababu ya wewe kuwepo hapa duniani, lipo kusudi la wewe kuwepo hapa duniani, ipo sababu ya wewe kuwa Kijana, hii ni muhimu sana. 

Kujitambua ni kuwa na ufahamu au uelewa juu ya angalau mambo yafuatayo: 

 Historia ya asili yako au maisha yako, ni muhimu Kijana ukajua historia ya maisha yako bila kujali ilikuwa nzuri au sio nzuri, au ya kuvutia au siyo ya kuvutia ili ujue kuwa kuna mahali unatoka, kuna aina ya watu wameunganishwa na maisha yako, hii itakusaidia katika safari ya maisha yako 

 Maumbile yako, au mwili wako, ujue madhaifu ya mwili wako, uelewe na kuutambua mwili wako vizuri na kujua namna ya kuudhibiti katika mazingira tofauti tofauti 

 Kusudi la maisha yako, maono au malengo kwa pasipo kujua sababu ya wewe kuwepo duniani unapoteza maana ya kuwepo duniani 

 Makuzi na malezi yako, maana haya yanaathiri kwa kiwango kikubwa sana hali yako ya baadae, ujue melelewaje na umekua katika mazingira gani ili tabia zako na mwenendo wako zipate maana na uwe na uwezo wa kujifunza kwanini umekuwa na tabia Fulani Fulani, 

 Mazingira na jamii, taifa lako na zana nzima ya uzalendo, ujue kuwa uzalendo haufundishwi kwa kuwapa watu mali na pesa, Mungu amekupa wewe fursa ya kuzaliwa na kuishi Tanzania kwa makusudi na kama hujui basi utaishi kama mnyama na utapoteza ladha na kuwajibika 

 Hisia, utashi na ufahamu wako 

 Maneno na maamuzi yako, 

 Tabia na mwenendo UMUHIMU WA KUJITAMBUA Kujitambua ni muhimu sana kwani kunakusaidia kujua mambo juu ya maisha yako: 

 Ili kutembea au kuishi katika viwango asilia ambavyo umeumbwa navyo (The originality of you) 

 Ili kujua madhaifu uliyonayo kwa ajili ya kujua namna ya kuyashinda 

 Ili kujua thamani yako, uepuke kutumiwa vibaya, usijidharau wala kumtengenezea mtu mwingine mazingira ya kukudharau na hata usimdharau mtu mwingine 

 Ili ujua nafasi yako (majukumu) katika maisha yako na ya wale wanaokuzunguka 

 Ili kujua umuhimu ulionao kwa ajili ya kuleta matokeo yanayotarajiwa kwako 

 Itakusaidia kutumia vizuri rasilimali kama muda, watu nk 

NAAMINI LEO UMEPATA KITU CHA KUKUSAIDIA KATIKA SOMO HILI, NI MATUMAINI YANGU KUWA UTAANZA KUFANYA MABADILIKO KATIKO JAMII YAKO SASA!!
Usikose somo lojalo!
Na Mwl. Raphael Lyela kutoka Youth Kingdom Ministries,Jesus Up!
 
......LITAENDELEA!!!!!!!

TAMASHA KUBWA LA KUMSIFU MUNGU PAMOJA NA WATOTO WA MUNGU (HOCET)

 
SHALOM!!
IMETUPASA,NI VEMA NA HAKI KUMSIFU MUNGU WETU KILA SAA NA KILA WAKATI...MAANA AMETUUMBA ILI TUMWABUDU...LAKINI HIYO PEKE YAKE HAITOSHI,MTUME PAULO ANASEMA DINI ILIYO SAFI ISIYO NA TAKA MBELE ZA MUNGU BABA NI HII KUWATAZAMA YATIMA,WAJANE,WASIO NA MSAADA KATIKA DHIKI ZAO NA KUJILINDA NA DUNIA PASIPO MAWAA (YAK 1:26,27)
....BASI SASA SAFARI HII WATU WA MUNGU TUTAKUSANYIKA PAMOJA KWA AJILI YA KUMSIFU MUNGU,KUZINDUA DVD YA WATOTO WA MUNGU PAMOJA NA KUFANYA CHANGIZO LA KUWASIDIA MTAJI WA KUJIENDESHA WATOTO HAWA AMBAO WAFADHILI WAO WALIWAKIMBIA BAADA YA KUONA WANAMWAMINI MUNGU!....BASI UKIONA TANGAZO HILI NJOO UJUMUIKE NASI ILI TUTIMILIZE MAANDIKO YOTE!
WAIMBAJI WENGI SANA WATAKUWEPO KATIKA KUWASINDIKIZA WATOTO HAWA NA MALENGO MAKUBWA NI KUPATA FEDHA ZA KUTOSHA KUNUNUA CANTER,NG'OMBE WA MAZIWA PAMOJA NA MTAJI WA KUKU WA MAYAI NA NYAMA ILI SHULE HII IWEZE KUJIENDESHA PASIPO KUNGOJA MISAADA MAANA WATOTO HAWA WANAWEZA KUZALISHA NA KUJITEGEMEA HUKU WAKISOMA VIZURI NA KUSOMA NA KWA BIDII!!
IWENI MFANO WA KUIGWA!!!

UNAWEZA KUTUMA MCHANGO WAKO KWA M-PESA KWENDA 0754527955

GOSPEL STANDARD BASE BLOG TUWATAKIENI MAFANIKIO MEMA NA MNAKARIBISHWA KUTUSHIRIKISHA TENA WAKATI WOWOTE ULE MKIWA TAYARI!
President.

Thursday, May 16, 2013

JUKWAA LA KIOO......WAJUE 1st Q CHRISTIAN DANCERS,VIJANA WANAOKUJA KWA KASI NCHINI KATIKA TASNIA YA DANCE!!

Episode One......JUKWAA LA KIOO!!!

SHALOM!
KWA MARA YA KWANZA KATIKA CHUMBA HIKI KIPYA CHA "JUKWAA LA KIOO" CHINI YA UKURASA WA WA "Gospel Music" na "Talents"NA LEO KWA MARA YA KWANZA TUNAANZA NA 1ST Q DANCERS WENYE MAKAO YAO JIJINI DAR ES SALAAM,HILI NI KUNDI LENYE VIJANA MAHIRI NA NIMEBAHATIKA KUWAONA MARA KADHAA KATIKA MATUKIO KADHAA NA LEO NIMEPATA BAHATI YA KUFANYA MAHOJIANO NA MBEBA MAONO NA MKURUGENZI MTENDAJI WA KUNDI HILI DADA GRACE LIFARD MLAWA,NA MAZUNGUMZO YETU YALIKUWA KAMA IFUATAVYO;

GoStaBa:Habari yako dada!

MGN:Ni nzuri sana sijui za kwako?
Mimi ni mzima sana na leo naona nikuhoji kidogo kuhusu kundi lako la 1st Q,naamini hutojali!
karinu sana wala usijali,na mimi ninafurahi kupata nafasi hii ya kuongea na Gospel Standard Base.

GoStaBa: Okey,watu wangependa kujua Kundi lenu linaitwaje?

MGN:1st Q (1st Quadrant)


GoStaBa: Nini maana ya jina hilo na kwa nini mnajiita hivyo?

MGN:1st Quadrant inatoka katika “XY plane”, ambapo AXES zote katika 1st quadrant ni chanya (Positive), ndio maana tukajiita hivyo, kama Biblia ilivyoandika katika Warumi 8:28…..Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote,Mungu hufanya kazi na wale wote wampendao katika kuwapatia mema!.......kwa hiyo nasisi tunaamini kwetu yote ni mema kwasababu tunafanya nae kazi.

GoStaBa: Kundi lenu lilianza lini na lilianzishwa na nani?

MGN:Tulianza mwezi  april mwaka 2012 kwa halisia,lakini wazo lilikuwepo tangu mwaka 2010,Kundi hili ni wazo langu(Grace) ila tulianza na watu watano nao ni Mimi,Belinda,Mgeni ,Tenes na Lisa.Lakini mpaka sasa tunao dancers 12,wakiwemo wasichana 9 na wavulana 3.


GoStaBa:Hili ni wazo jipya kwa kanisa,hususani kundi linalowahusisha wasichana wengi zaidi,Je nini  Changamoto zipi mlizopambana nazo au mnazoendelea kupambana nazo katika kukua kwenu?

MGN:Changamoto ni nyingi lakini hizi chache ndizo naweza kuzisema kwa sasa; ya kwanza ni kuwa <Sio makanisa yote yanaelewa jambo hili kwa hiyo watu hao hawawezi kuwaruhusu> ya pili<Kwa kuwa wengi wa dancers ni wanafunzi  wa secondary na vyuo hivyo muda wa kukutana kufanya mazoezi ni adimu,yaani mpaka wakati wa likizo> ya tatu <Kwasababu watu wengi bado hawajui na hawajakubali,basi kuungwa mkono bado ni kugumu na kusemwa semwa  bila  kusaidiwa> na nyingine ni <hatuko Exposed,lakini bado tunalifanyia kazi ili kuhakikisha tunafahamika> ,na nyinginezo  lakini zingine ni za kawaida na zinatatulika.

GoStaBa: Mmefanikwa kwa kiasi gani mpaka sasa?

MGN:Bado hatujafanikiwa kufikia malengo yetu lakini mpaka sasa tumeshahudhuria na kuhudumu katika matukio/matamasha zaidi 10 tangu mwaka jana mpaka sasa,yakiwemo matamasha matatu ya mwisho ya King Chavala..LAUGH AGAIN CONCERT SERIES na pia tumeshirikishwa kwenye Video ya wimbo wa “KATIKA NYUMBA YA BWANA” wa Amani Kapama.

UNAWEZA KUANGALIA VIDEO CLIP HII KAMA SAMPLE
http://www.youtube.com/watch?v=SVVuCoKZTGg

GoStaBa: Mnalelewa na nani?

MGN:Tunalelewa na Mama Mlawa na kushauriwa na Daniel,Agnes,Doreen,Patrick na wengineo

GoStaBa: Nini mategemeo au mipango yenu mbeleni?

MGN:Mategemeo yetu makubwa sio kuendesha 1st Q kama kundi bali kama ministry au organization ambayo itahusisha vipaji vingi sana walivyo navyo vijana katika kuhubiri injili na sio Dar peke yake bali Tanzania nzima.

GoStaBa: Ni jambo gani ambalo mkisaidiwa mnafikiri mtalifurahia sana kama kundi?

MGN:Tutafurahi sana kama tutapata nafasi ya kufanya kazi/kupeform mahali wa makubaliano ya muda mrefu au uhakika wa kufanya performance angalau mara moja kwa mwezi.

GoStaBa: Ni nani mnatamani kufanya nae kazi?

MGN:Yeyote Yule aliye tayari kufanya kazi nasi kwa moyo mmoja.

GoStaBa: Ni kundi gani(la ndani au nje ya nchi) ambalo mnavutiwa nalo sana na mnatamani kuwa kama wao au kuwazidi? Kwanini?

MGN:Hakuna kundi tunalotamani kuwa kwa wao au kuwazidi ila kuna makundi ambayo tunayakubali ni kama vile RIOT Dancers,DPC Dancers na mengine mengi  ya nje kama vile mastered seed group.


GoStaBa: Una neno au ushauri wowote kwa wasomaji wa Blog hii?

MGN:Naona niwape neno toka katika Biblia kitabu cha 1kor 10:31…..Basi,mlapo au mnywapo,au mtendapo neno lolote,fanyeni  yote kwa utukufu wa Mun gu….. na pia 1kor 12:5-6……tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye Yule. 6-Kisha pana tofauti ya kutenda kazi,bali  Mungu ni yeye Yule azitendaye kazi zote katika wote. Utofauti wetu (Wakristo) katika kutenda kazi usituathiri, ikiwa wote tunafanya kazi  ya Yesu Kristo  tukiongozwa na Roho mtakatifu. Amen.

GoStaBa: Ahsante sana mtumishi kwa muda wako na natumai tutaonana tena na tena!

MGN: Ahsante sana pia ninakushukuru sana na Mungu awabariki ili mzidi kungara ulimwenguni.
....................................................................................................................

BASI KWA UFUPI KAMA TULIVYOMSIKIA MBEBA MAONO NA MKURUGENZI,GRACE LIFARD MLAWA, HILO NDIO KUNDI LA DANCE LA LA 1ST Q  LENYE MAKAO YAKE JIJINI DAR ES SALAAM ,AMBALO LINAENDELEA KUKUA NA WAKO TAYARI  KUFANYA KAZI NA KANISA,MWIMBAJI,DANCERS NA MTUMISHI YEYOTE YULE ALIYE TAYARI AITHA IWE TAMASHA,IBAADA AU HATA KUFANYA VIDEO RECORDING KWA WAIMBAJI WA NDANI NA NJE YA NCHI YA TANZANIA SAWASAWA NA MISINGI NA TARATIBU ZA KUNDI HILO KWA UTUKUFU WA MUNGU.
NATAMANI TUWATIENI MOYO VIJANA HAWA WALIOAMUA KUMTUMIKIA MUNGU KUPITIA VIPAJI VYAO,BASI KWA KUJUA ZAIDI AU KUWAALIKA AU KUTAKA KUSHIRIKIANA NAO BASI WAWEZA KUWAPA KUPITIA ANAUANI ZIFUATAZO;

Simu; +255719868702, +255719406060, +255654767422
Barua pepe;lifarda1@gmail.com
Facebook; 1st Q

KARIBUNI SANA KWA MASWALI NA MAONI AMA USHAURI
+255 713 883 797
lacs.project@gmail.com

Tuesday, May 7, 2013

TANZANIA GOSPEL SINGERS' BREAKFAST-Episode 2!!

SHALOM!
KWA MARA NYINGINE TENA(YA PILI); GOSPEL STANDARD BASE Blog IMEWAANDALIA WAIMBAJI WOTE WA NYIMBO ZA INJILI,CHAI YA ASUBUHI,ITAKAYONYWEWA JUMAMOSI YA TAR 11/05/2013 KUANZIA SAA MBILI ASUBUHI MPAKA SITA NA NUSU MCHANA,PALE VICTORY CHRISTIAN CENTRE-VICTORIA(KWENYE KITUO CHA MAFUTA),ZAMANI KANISA LA VCC!
HII NI CHAI MAALUM AMBAYO INAWAKUTANISHA WAIMBAJI WOTE WA NYIMBO ZA INJILI,KUANZIA WAIMBAJI WA KWAYA,BAND,VIKUNDI NA WAIMBAJI MMOJA MMOJA,NA INAHUSISHA MIZIKI YOTE YA KISWAHILI,KIINGEREZA,KILUGHA NA PIA HIP HOPE NA AINA NYINGINE ZOTE ZA MIZIKI,IKIWA WEWE UNAFANYA MUZIKI WA INJILI BASI HII INAKUHUSU SANA!
HII NI FURSA PEKEE YA KUFAHAMIANA,KUFUNDISHWA,KUCHANGAMOTISHWA,KUOMBA NA KUNYWA CHAI PAMOJA ILI KUJENGA UMOJA NA MSHIKAMANO ZAIDI KUNUA VIWANGO VYA MUZIKI WA INJILI TANZANIA!!
HAKUNA KIINGILIO CHOCHOTE ILI HAUZUILIWI KUTOA MCHANGO WAKO WOWOTE ULE!
IMEDHAMINIWA NA BLOG HII NA KUSIMAMIWA NA "CHAVALA IDEAS PLATFORM"

KWA MAELEZO ZAIDI
+255 713 883 797