Wednesday, December 10, 2014

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 2



Shalom!
Naamini unaendelea vema hata leo,kama ulisoma sehemu ya kwanza(na kama bado nenda kwa wall yangu usome post yenye kichwa kama hiki )...nilianza kwa kujenga msingi wa Kusifu na kuabudu!
Na nikamalizia kwa swali...Nani mwabudu Mungu wa Kweli na imempasa kufanyaje???
LEO
Natamani kusisitiza mambo makubwa mawili tu katika sifa na kuabudu!!
Yaani haya yakae moyoni na kichwani mwa yeyote anayetamani kuugusa moyo wa Mungu kwa sifa na kuabudu,nayo ni haya;
1.LAZIMA KUMJUA NA KUMFAHAMU SANA HUYO MUNGU NA KUWA NA UHUSIANO NAYE.
Huwezi kufanya ibaada yeyote kwa Mungu ikawa ya maana kama unamsikia tu na humfahamu kabisa....imetupasa kumjua tena kumjua zaidi,tena kuwa na uhusiano naye wa karibu....maana kwa Kadri unavyomjua zaidi ndivyo unazidi kumpenda yeye na Kumsifu na kumuabudu kweli!....na hapo Ndio maandiko yanasema "Kusifu kwawapasa wanyofu wa mioyo"...Okey ngoja nitoe mfano huu,Kumsifu Mungu wakati hata hamna uhusiano wa karibu na sawa na kuona mjini gari aina ya Hammer ambayo iko mitaani kwenu na ukaanza kuwasimulia wenzio..."Oyaaa unaona ile hammer,yaani nyumba yetu hii unapita mtaa mmoja ndio nyumba ya mwenye gari ile aisee,yaani ile gari kali kishenzi yaani duh,Nyie Acheni tu mtaa wetu mambo Safi hahaha" sasa hapo wakikuuliza ni Tsh ngapi au umewahi kupanda au anakufahamu unabaki tu Aaah mmmm Oooh...Acha bwana hilo sio lenu, jivunie chenu...JIVUNIE MUNGU MAISHANI MWAKO,SIO KUMSIKIA TU!!
2.LAZIMA MUNGU PEKE YAKE NDIO AINUKE(AWE MAARUFU)
Yaani katika sifa na kuabudu usijitahidi kujiinua au kutaka kuonekana wewe au timu yenu au mchungaji wenu au Kanisa lenu Ila Mungu pekee Ndio wakuinuliwa!!
Kuna ukuta mwembamba sana kati ya kutafuta sifa na umaarufu au kujiona na unyenyekevu wa kutaka Mungu pekee Ndio aonekane!!
Tena sio kwa maigizo bali toka moyoni... Na ukiwa na moyo wa unyenyekevu utashangaa una Amani tele hata uende wapi au watu wawe kumi tu au vyombo visiwepo au sare zisiwepo hata usipopewa maji au nauli na popote ulipo kwa kuwa umeamua kumfanyia Mungu ibaada basi utashangaa sana udhihirisho wa nguvu za Mungu!!!
Tabia za kuonyeshana na watu ufundi wa Sauti au kucheza na kusahau kuwa malengo ni kumuabudu Bwana basi hapo ibaada yote huwa sifuri maana tumejitwalia utukufu machoni pa watu.
(Ila pia haimanishi pia kuwa sifa na kuabudu vinapaswa kufanyika ovyoovyo..ustadi unahitajika mno)
Mungu awasaidie sana wote mnaokaa mbele kuwaelekeza watu au kuwaongoza uweponi mwake ili Mjue hamfanyi kwa ajili yenu Ila.kwa ajili ya Mungu!!!
.....Je ladha ya Kusifu na kuabudu inatokana na.viungo gani???

(c)King Chavvah, 2014
+255 713 883 797

No comments:

Post a Comment