Monday, January 26, 2015

MAMBO MATANO NILIYOJIFUNZA KUTOKA KWA PENSELI!!

MTENGENEZAJI WA PENSELI ANAYO MAMBO 5

NIYAPENDAYO,NA HAYO NI MAFUNZO KWA PENSELI NA SISI LEO!!!

Mtengenezaji wa PENSELI aliiambia penseli haya na mimi leo ninawaambia ninyi;

1.Eeeh PENSELI popote utakapogusa utaacha ALAMA (Haijalishi ni vizuri au vibaya)
>>>NA WEWE PIA KILA UNAPOPITA MAISHANI MWAKO UNAACHA ALAMA KWA WATU.

2.Eeeh PENSELI najua unaweza kukosea mara nyingi,basi usijali,juu yako upo MFUTO ili kufuta kila alama mbaya isiyotakiwa.
>>>NA WEWE PIA NAKUAMBIA HATA UKIFANYA MAKOSA KIASI GANI,MFUTO WA DAMU YA YESU UKO JUU YAKO.....Hakuna awezaye kurudi nyuma kuanza upya,ila pale ulipo panaweza kuwa hatua ya mwanzo mpya!

3.Eeeh PENSELI,Kitu cha muhimu sana kwako ni kile ambacho KIKO NDANI YAKO(Risasi ya graphite),Hata kama uwe na umbo ama umbile lenye mapambo kiasi gani!
>>>NA WEWE PIA TAMBUA YA KUWA KUSUDI LA KUISHI NDANI YAKO NDIO MUHIMU SANA MAISHANI MWAKO KATIKA KUMPENDEZA MUNGU,YAANI LILE MUNGU ALILOKUANDIKIA na haya mengineyo ya nje ni mbwembwe tu!

4.Eeeh PENSELI Hauwezi kuandika vizuri mpaka ukubali KUCHONGWA VIZURI ili uwe sharp(sio ombi unless unataka kuwa pambo)
>>>NA WEWE LAZIMA UJUE JAMBO MOJA KUWA ILI KWENYE MAISHA YAKO UUFURAHIE MWITO WAKO,LAZIMA UKUBALI KUCHONGWA AMA KUPITIA MAGUMU ILI UJIFUNZE KUKUA NA KUKOMAA.

5.Eeeh PENSELI pamoja na yote hayo bado huwezi kuandika au kuifurahia kazi yako,ni lazima UKUBALI KUSHIKWA NA MKONO HODARI ili mwandiko au mchoro uwe bora!
>>>NA WEWE PIA LAZIMA UKUBALI KUSHIKWA NA MUNGU MWENYEWE NA KUFUATA NENO LAKE NA KILA AKITAKACHO NA HAPO NDIO UTAPONA NA KUWA NA FURAHA MAISHANI MWAKO!!!

Ubarikiwe sana kama umenielewa na ukiweza SHARE na wenzako wasome!!!

Na King Chavala MC
+255 713 883 797