Wednesday, December 10, 2014

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 5(mwisho)


Shalom!
Yesu Kristo asifiwe sana!
Naamini uliyekuwa unafuatilia mfululizo huu umejifunza mengi na kubarikiwa pia,leo katika sehemu ya tano...Kuhusu kusifu na kuabudu, kama nilivyoahidi sehemu ya nne,tutaangazia mambo mawili makubwa;

I.NAMNA UNAVYOWEZA KUFANYA IBAADA YA SIFA NA KUABUDU!!
Kumfanyia Bwana ibaada,inategemeana sana na mahusiano yenu...yaani ningeweza kuwianisha na Mama na mwanae,namna ya kumlisha inategemea sana na urahisi wa mtoto huyo kula na kushiba, mwingine hula akipakatwa,mwingine hula akiwa anaoga, mwingine akiwa peke yake,muhimu ni kuwa mtoto amekula!!
Ibaada njema ni ile inayoanzia ndani ya kilindi cha moyo kabisa kwa upendo mkubwa,hivyo unaweza kufanya ibaada hiyo kwa namna nyingi,na hizi ni chache ambazo zimewahi kutumika na watumishi mbalimbali katika Biblia!
Unaweza Kumsifu na Kumwabudu Bwana:
1.Kwa kuimba,Iwe kanisani au popote pale-na hapa inaweza kuwa nyimbo za vitabuni, tenzi au zaburi au nyimbo mpya za kutoka moyoni mwako unapotafakari ukuu wa Mungu!
2.Kwa kupiga kelele-hii inaweza kuwa kelele zisizo na mpangilio au vigelege au miluzi au kelele zenye mpangilio wa nyimbo fulani!
3.Kwa kucheza -furaha ya mdundo unaoanzia ndani na sio ilimradi tu kuna muziki,na kwa habari ya kucheza unaweza kucheza hata kama hakuna muziki wowote
4.Kwa ubunifu na kazi za sanaa-mfano uchongaji,uchoraji, uigizaji na kazi nyingine za sanaa ambazo mwisho wa siku Ni Mungu ndio anasifiwa na kuabudiwa peke yake
5.Kwa kulala -unaweza ukalala namna yeyote ile kama ishara ya kujinyenyekesha mbele za Bwana
6.Kwa kupiga magoti
7.Kwa kukaa kimya mbele za Bwana
8.Kwa Kulia
9.Kwa kucheka
10.Kwa kunena kwa lugha nyingine,ziwe za duniani au lugha za kimbinguni!
11.Kwa kuomba
.....Sasa sifa na kuabudu inawiana na kuingiliana sana na maombi japo unaweza Kumsifu na Kumwabudu Bwana kwa maombi!!
Hizo ni chache katika namna nyingi,ambazo unaweza kujidhihirisha mbele za Bwana!!
Watu wengi wamechukuliwa na sifa na kuabudu ile ya kuimba na kucheza labda na kulia kanisani kwa maombi,na ni sawa tu!
Ila jambo la pili ni

II.NAMNA IMPASAVYO KUWA YEYOTE AKAAYE MBELE KUONGOZA WENGINE KATIKA IBAADA YA SIFA NA KUABUDU!
Wengi hufanya kama mazoea au utaratibu tu wa ibaada kwasababu wameshaguliwa au wamefanya mazoezi au wanajua au wana vipaji lakini ni zaidi ya hapo,imekupasa. Kuwa moyo mnyofu na Ibaada nzuri huanzia ndani yako kwanza kabla wengine hawajapotelea katika wingu,
1.Imempasa mtu huyu kuwa mtakatifu/mtauwa na anayempenda Mungu kiasi cha kupenda kumfamyia ibaada hata akiwa peke yake kabla hata kuwa mbele za watu
2.Imempasa kuwa na Neno la kutosha moyoni mwake,sio maandiko ya kukariri
3.Imempasa kuwa mwombaji, maana imempasa kusikia sauti ya Mungu wazi wazi ili awapo madhabahuni asifanye kwa mazoea
4.Imempasa kuwa na muonekano usioleta maswali kwa watu,yaani mavazi,mapambo na hata kutembea tu.
5.Imempasa kuwa na Amani na watu maana ikiwa mtu huyo ana Ugomvi au maneno maneno na watu,ibaada hiyo haiwezi kukamilika
6.Uongo,uzinzi,Umbeya, Unafiki na udhalimu wowote ule usitajwe kwake akaaye mbele za watu!...maana sifa na kuabudu kwa mwenye dhambi ni kelele mbele za Mungu!
7.Imempasa kuwa mnyenyekevu na aliye jaa hekima,na asiyejaribu kujitutumua au kujiona ni yeye na.bila yeye uwepo ule usingeshuka!
Lazima umaarufu, vyeo,elimu na hadhi viwe chini ya Utukufu wa Mungu,hivyo yeyote akaaye mbele za watu ajue kabisa kuwa yuko hapo kwa ajili ya Kumsifu na Kumuabudu Mungu tu na sio kuonekana!!
Mungu Roho mtakatifu akusaidie sote kuelewa sana zaidi ya maandishi haya,ili ibaada zetu za sifa na kuabudu, ikiwa ni za binafsi au mbele ya watu zipate kibali mbele za Mungu!
Mungu akuwezeshe na Mungu akunyenyekeshe ewe Mwabudu!!
Mpaka hapa Nimemaliza kwa habari ya Kusifu na kuabudu na ninayaacha kwako wewe kujifunza na kufundisha na kushare na wengine pia!!
*Najua utakuwa unajiuliza mbona hamna mistari ya Biblia,ndio! sitaki watu wanaokariri Nataka wanaoelewa!!!
Mungu akubariki sana wewe rafiki yangu!!
*Karibu sana katika Ulimwengu wa Kusifu na Kuabudu,kwa roho na kwa akili kwa kupenda!!

***MWISHO***
(c)King Chavvah, 2014
+255 713 883 797

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 4


Shalom wana wa Mungu!

Wajoli na Wajeuri wa Bwana!
Tumekuwa na mfululizo wa kupendeza kuhusu sifa na kuabudu,na tangu tumeanza leo ni sehemu ya nne kati ya tano...na leo natamani kuzungumzia "Kwanini Sifa na kuabudu maishani mwetu" yaani muunganiko wa sifa na kuabudu na hatma za maisha yetu!
*Najua wengi tunajua Kusifu na kuabudu ni sehemu ya ibaada mbalimbali makanisani na ndio maana watu huanza kwa maombi,sijui matangazo kisha Kusifu na kuabudu, neno,sadaka na mengineyo Ila leo natamani nikujuze kuwa sifa na kuabudu ni zaidi ya hapo!!
Kusifu na kuabudu ni ibaada endelevu kila siku na kila mahali na kwa kila namna!
Ile ifanyikayo kanisani ni namna ya pamoja ya Kusifu na.kuabudu kwa upamoja na kwa utaratibu tuliojiwekea na kama watu wakibaki na picha hiyo pekee hawatafanya ibaada hiyo kwa ukamilifu!!! 

ZINGATIA UKWELI HUU!!
Kila mtu ameubwa kwa kusudi maalum hapa duniani na kila mtu amepewa uwezo fulani halisi unaomwezesha kufanya mambo yale yampasayo kwa urahisi kuliko yeyote mwingine(Yaani kwa mfano mimi sijitahidi kusheresha au kuchekesha maana ipo ndani naturally) na.uwezo huo huitwa kipaji na wazungu huongea kwa maringo zaidi "Gifts & Talents".....na kwa ujumla wake woote mambo haya ili tumwabudu Mungu!
Sasa kama tuna majukumu ya kufanya na hayo yote ni kwa ajili ya Kumwabudu Mungu na kuyafanya majukumu hayo ndio kuishi kwenyewe...tunaachaje kumwabudu Mungu??
Ile hali ya kujua kuwa hakuna jambo unaloweza kufanya kwa akili yako na uwezo wako binafsi na ule ukweli kuwa yote ufanyayo ni kwa utukufu wa Mungu....itakulazimu kuabudu tu,isipokuwa kama umeamua kuwa na Kiburi cha uzima na kujiona kama umejiumba mwenyewe!!
"Katika sifa Mungu hushuka" naamini umewahi kusikia sentensi hiyo Ila unadhani ni kwa ajili ya ile sifa ya kanisani pekee...Je hujawahi kusikia wale watu wa kale waliowahi kushinda vita kwa sifa?? Popote ambapo Yesu anasifiwa lazima uwepo wake uwe Kamilifu.... Sasa ukitaka mambo yako yaende sawia na kwa Ushindi lazima ukubali tu kujumlishia na Ibaada ya sifa na kuabudu!!

Kusifu na kuabudu ni kama vile kusema....MUNGU NI WEWE PEKE YAKO,HAYA YOTE NI YAKO,SHUKRANI TUKUZO NA SIFA ZOTE NI ZAKO,UMETUPA HIVI VYOTE KWA UTUKUFU WAKO,AHSANTE JEHOVA MAANA NI WEWE!!
Yaani kwamba sio kwa uwezo wako wala akili yako bali ni kwa Neema ya Mungu tu!!
Kusifu na kuabudu ni wakati wa shida na wakati wa raha,ukiwa na kusanyiko na hata ukiwa peke yako,ukiwa nyumbani na hata ukiwa mbali,kwa mavazi,muonekano, kelele, kula,kuongea,kufanya kazi na hata katika kujifurahisha!!
Muhimu kujua kuwa Umeumbwa ili umuabudu Mungu,utafundishwa kuwa mtumishi ama kuishi hatma yako au utafunzwa kuwa na ndoto au kuacha Alama itakayodumu ni sawa kabisa lakini msingi wa yote haya ni ili Mungu atukuzike..... Watu wamjue Mungu,waupokee Ufalme wake na wamuishi yeye....na hapo Ndio tunasema Maisha ya Ibaada,na.hiyo ibaada ndio Kusifu na Kumuabudu!!
Unaweza ukachoka Kumsifu alivyo mwema maishani mwako lakini kila uonapo watu wanakufa, wengine wanaumwa na hawa wapata shida....na hayo yawapatayo wenzio wewe huyashuhudii basi choka salama....na ukimjua Mungu sawasawa kuwa yeye hata nini kitokee duniani hakibadilishi Umungu wake...na kama ukijua ni baba yako,na AHADI zake kwako ni za milele,hutaacha kumuabudu leo kwasababu una mashida na machangamoto....Ila utamwabudu tu kwa kuwa yeye ni Mungu na tumaini lako la kesho maana ni hakika na Amina!
Mungu ni mwaminifu sana mara nyingine ni kiburi tu ndio huwa kinatufanya tumsifu na kumuabudu sana aitha tukiwa tuna vingi au tukiwa hatuna basi tunamlilia, na huo kwa hakika ni utoto!!
Basi Mungu akusaidie kuwa na maisha ya Kusifu na Kuabudu kila siku, kila wakati na kila mahali bila kujali nini wala nini na hakika uwepo wa Mungu hautapungua maishani mwako!!!
Kabla ya saa ile ya Agano nitamalizia sehemu ya tano na ya mwisho kwa habari ya mambo makubwa mawili;
i. Namna ambazo unaweza kufanya ibaada ya sifa na kuabudu
ii. Mambo yakupasayo kuzingatia uwapo mstari wa mbele katika kuwaongoza wengine katika sifa na kuabudu!!
Ahsante Bwana Yesu kwa kila asomaye na kuelewa somo hili,lisaidie Kanisa lijue kina na msingi wa Ibaada kuwa ni SIFA NA KUABUDU....maana hata Malaika, maserafi, makerubi,wazee 24,wenye uhai wa nne na Sisi watakatifu tuliyo duniani na hata saa ile ya mwisho kule mbinguni biashara ni moja tu "KUMSIFU NA KUMWABUDU MUNGU"
(Usiache kushare kwa marafiki zako)

+255 713 883 797

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 3


Shalom ndugu yangu!
Naamini unaendelea vema na maisha yako na ninambariki Mungu sana kwa ajili yako na nimemwomba roho mtakatifu akusaidie kuendelea kuelewa somo hili!
Mara ya mwisho niliongelea mambo mawili makubwa kwanza ni Lazima Mtu anayetaka Kumsifu na.kumuabudu Mungu kweli lazima awe na uhusiano naye thabiti na pili katika sifa na kuabudu sio wewe au Kanisa au chochote kuinuliwa zaidi ya Mungu mwenyewe!
...Na nikaacha swali....JE NI VIUNGO VIPI HULETA UTAMU WA KUSIFU NA KUABUDU!!
Basi ninamshukuru sana Mungu kwa ajili yako na natamani niseme nawewe kwa habari ya uzuri wa sifa na kuabudu!
Sisi huwa tunadhani uzuri wa sifa ni Muziki(Melody),nyimbo tuzipendazo Sisi, mavazi yetu,mitetemeko ya waongoza sifa,machozi labda na mihemuko na hapo tunaweza kuruka na kucheza sana lakini hata kama Hayo yote huwepo au ni muhimu Ila msingi wa Utamu wa sifa na kuabudu ni haya yafuatayo;
1.Ibaada ya sifa na kuabudu yenye Utamu mbele za Mungu ni ile inayofanywa na Moyo wa kumpenda yeye,moyo Safi na wenye nia thabiti ya Kumsifu na Kumuabudu!!
2.Siyo nyimbo uzipendazo wewe ndio zinaleta utamu wa sifa mbele za Mungu,sio upendazo wewe maana sio kwa ajili yako Ila kwa ajili yake mwenyewe.... Ingawa ukizama sana utagundua kuwa kile roho mtakatifu anataka na wewe unaingiwa kupenda kile atakacho!!!
*Sasa natoa tahadhari tu.... Acha ubinafsi wa kutaka Kusifu na kuabudu kwa matakwa yako Ila msikilize sana roho ili mara zote umeona wingu lake!
3.Na tatu ni ile hamu ya kumtaka Mungu Atukuzike katika sifa na kuabudu ndio inafanya moyo wako uwe mnyenyekevu na kwa hakika Mungu ajidhihirishe na sio kuwa na hamu ya kutaka kusifiwa au kupongezwa baada ya uwepo kudhihihirika!
*Unajua Mungu akisifiwa hushuka lakini ile hamu yako ya kumuona Mungu zaidi na sio Kiasi wewe uonekane kama wewe ndio huwa unasifu na kuabudu mpaka uwepo unashuka!
4.Na mwisho;Ili ibaada ya Kusifu na kuabudu Iwe na tamu....Ni mara zote ikiwa unafanya ibaada ya sifa na kuabudu lazima uwepo umoja kati ya moyo wako au roho yako na nafsi yako na mwili wako lakini pia ikiwa mnafanya ibaada mkiwa wengi basi iwepo nia moja na mara zote muonekano wako, mkao wako na mavazi yako,yakupe nafasi ya kuwa na utulivu mbele za Mungu.... Haiwezekani ibaada ya sifa na kuabudu Iwe tamu wakati moyo na akili yako na nafsi yako havina ushirikiano....na huwezi kuwa huru kufanya chochote mbele za Mungu kama kucheza,kulia au kurukaruka hali mavazi yako yana thamani kuliko hiyo ibaada kiasi huwezi hata kupiga magoti,huwezi kucheza kwasababu ya hadhi au cheo chako au mavazi yako yanakubana au yanawakwaza wengine!!
Natamani roho mtakatifu akusaidie kuelewa haya,maana ibaada.ya sifa na.kuabudu ni ya Mungu mwenyewe na wakati wote kumbuka "ALITUUMBA ILI TUMUABUDU"
Basi wakati mwingine nitaendelea kuzungumzia kwa kina "Kwanini Sifa na kuabudu maishani mwetu? na nini uhusiano wake na makusudio ambayo Mungu alituumba nayo"


(c)King Chavvah, 2014
+255 713 883 797

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 2



Shalom!
Naamini unaendelea vema hata leo,kama ulisoma sehemu ya kwanza(na kama bado nenda kwa wall yangu usome post yenye kichwa kama hiki )...nilianza kwa kujenga msingi wa Kusifu na kuabudu!
Na nikamalizia kwa swali...Nani mwabudu Mungu wa Kweli na imempasa kufanyaje???
LEO
Natamani kusisitiza mambo makubwa mawili tu katika sifa na kuabudu!!
Yaani haya yakae moyoni na kichwani mwa yeyote anayetamani kuugusa moyo wa Mungu kwa sifa na kuabudu,nayo ni haya;
1.LAZIMA KUMJUA NA KUMFAHAMU SANA HUYO MUNGU NA KUWA NA UHUSIANO NAYE.
Huwezi kufanya ibaada yeyote kwa Mungu ikawa ya maana kama unamsikia tu na humfahamu kabisa....imetupasa kumjua tena kumjua zaidi,tena kuwa na uhusiano naye wa karibu....maana kwa Kadri unavyomjua zaidi ndivyo unazidi kumpenda yeye na Kumsifu na kumuabudu kweli!....na hapo Ndio maandiko yanasema "Kusifu kwawapasa wanyofu wa mioyo"...Okey ngoja nitoe mfano huu,Kumsifu Mungu wakati hata hamna uhusiano wa karibu na sawa na kuona mjini gari aina ya Hammer ambayo iko mitaani kwenu na ukaanza kuwasimulia wenzio..."Oyaaa unaona ile hammer,yaani nyumba yetu hii unapita mtaa mmoja ndio nyumba ya mwenye gari ile aisee,yaani ile gari kali kishenzi yaani duh,Nyie Acheni tu mtaa wetu mambo Safi hahaha" sasa hapo wakikuuliza ni Tsh ngapi au umewahi kupanda au anakufahamu unabaki tu Aaah mmmm Oooh...Acha bwana hilo sio lenu, jivunie chenu...JIVUNIE MUNGU MAISHANI MWAKO,SIO KUMSIKIA TU!!
2.LAZIMA MUNGU PEKE YAKE NDIO AINUKE(AWE MAARUFU)
Yaani katika sifa na kuabudu usijitahidi kujiinua au kutaka kuonekana wewe au timu yenu au mchungaji wenu au Kanisa lenu Ila Mungu pekee Ndio wakuinuliwa!!
Kuna ukuta mwembamba sana kati ya kutafuta sifa na umaarufu au kujiona na unyenyekevu wa kutaka Mungu pekee Ndio aonekane!!
Tena sio kwa maigizo bali toka moyoni... Na ukiwa na moyo wa unyenyekevu utashangaa una Amani tele hata uende wapi au watu wawe kumi tu au vyombo visiwepo au sare zisiwepo hata usipopewa maji au nauli na popote ulipo kwa kuwa umeamua kumfanyia Mungu ibaada basi utashangaa sana udhihirisho wa nguvu za Mungu!!!
Tabia za kuonyeshana na watu ufundi wa Sauti au kucheza na kusahau kuwa malengo ni kumuabudu Bwana basi hapo ibaada yote huwa sifuri maana tumejitwalia utukufu machoni pa watu.
(Ila pia haimanishi pia kuwa sifa na kuabudu vinapaswa kufanyika ovyoovyo..ustadi unahitajika mno)
Mungu awasaidie sana wote mnaokaa mbele kuwaelekeza watu au kuwaongoza uweponi mwake ili Mjue hamfanyi kwa ajili yenu Ila.kwa ajili ya Mungu!!!
.....Je ladha ya Kusifu na kuabudu inatokana na.viungo gani???

(c)King Chavvah, 2014
+255 713 883 797

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 1


Naamini uko poa na unaendelea vizuri!!
Naamini bado una akili timamu na unajielewa zaidi una hofu ya Mungu ndani yako (Kama sivyo basi hapa kwako ni pagumu)
"KUSIFU" na "KUABUDU" ni ibaada kamili mbele za Mungu,msingi wa ibaada zote na inayopaswa kufanywa kwa makini,ustadi na furaha tele kwa ajili ya Mungu na Ibaada hiyo inawapasa wanyofu wa mioyo!!
KUSIFU-Ni ibaada ya kushukuru,kushangilia, kumkubali,kumsifia,kumwadhimisha,na kumtukuza Mungu kwa matendo yake makuu aliyo,anayo na tunayoamini anaendelea kututendea.
Unaweza kumfanyia sifa kwa yale aliyoyatenda kwa wengine au hata ujumla wa matendo yake maishani mwetu!
*Mara nyingi imetafasirika kuwa sifa ni nyimbo za haraka na shangwe Ila natamani Mjue sifa zaidi ni maudhui na makusudi ya moyo wa mtaa sifa!!
KUABUDU-Ni ibaada ya unyenyekevu,heshima na adhama. Kwa Mungu kukubali,kutii na kumuadhimisha kwa sifa na tabia zake...Hapa haijalishi amefanya chochote kwako au hajajibu maombi yako kama uonavyo Ila anaabudiwa kwa JINSI ALIVYO!
Niweke msisitizo hapa yaani hata kama Huna kazi,umefeli au umeachika bado Yeye ni Mungu tu na Ni mtakatifu tu na Ni mwema tu!!!
*Pia kwa wengi imetafasirika kuwa kuabudu ni nyimbo za taratibu,za kulia na hisia kali...lakini Nataka Mjue kuwa kuabudu ni Maudhui na mwelekeo wa Moyo!!
Sasa Nani ni mwabudu halisi na Anayemsifu Mungu kweli???
Na imempasa nini mtu huyooo....??

(c)King Chavvah, 2014
+255 713 883 797