Tuesday, April 30, 2013

ITAMBUE NAFASI YAKO KAMA KIJANA ILI ULETE MABADILIKO KATIKA MAISHA YAKO NA JAMII KWA UJUMLA(01)

Jesus Up!
Karibu katika safu hii ya mafundisho ya vijana yanayoitwa Nafasi ya Kijana. Tutakuwa na mambo kadha wa kadha ya kujifunza kuhusu Nafasi ya Kijana kwa ujumla wake tukimwangalia Kijana na sehemu anazotakiwa kusimama au wajibu anaotegemewa kuwa nao na kuufanyia kazi au majukumu aliyonayo katika maeneo mbali mbali yanayomuhusu.
Ni mafundisho yanayolenga kuleta ufahamu sahihi juu ujana na Kijana kama Ufalme wa Mungu unavyomtambua na kumtegemea pia. Lengo letu kuu ni kuwafanya vijana wawe wanafunzi wa Yesu kwelikweli kwa kufundishwa KWELI ya Neno la Mungu kuhusu Nafasi yao katika upana wa maisha yao.

Ni muhimu kila Kijana akafahamu mambo yafuatayo kuhusu yeye:
1. Ni lazima ujitambue, upate ufahamu sahihi juu ya maisha yako pamoja na mambo yote na jamii inayokuzunguka
2. Ni muhimu ujue wajibu ulionao kwako wewe mwenyewe kama mtu binafsi juu ya maisha yako
3. Kuna haja ya kujua kuwa wewe ni sehemu ya familia yako na lazima ujue wajibu wako kwa wazazi na familia kwa ujumla
4. Ni lazima ujifunze kuwa mzalendo wa taifa lako sawa na jinsi ambavyo Mungu anataka, fahamu kuwa umeunganishwa na ardhi ya Tanzania kwa mafanikio yako, Mungu akikwambia nenda nje ya nchi nenda lakini

Thursday, April 25, 2013

TEACHING CONCERNING "NAFASI YA KIJANA" COMING SOOON!!!!

HELLO SHALOM!!
HERE IS THE SPECIAL PLATFORM FOR YOUTH ISSUES!
AND THE PAGE START THIS WAY!!!
Huwezi kuyajali maisha yako kama hujui thamani yake, huwezi kujua thamani ya maisha yako kama hujajitambua kwa Neno la Mungu, huwezi kuwa na maisha ya mafanikio kama maamuzi yako hayatengenezi mafanikio, hata usipoamua maisha yako yataendelea kama kawaida

NA MWALIMU RAPHAEL LYELA!!!
Jesus Up!

Wednesday, April 24, 2013

KIJANA "PAUL CLEMENT" KUIWEKA WAKFU ALBUM YAKE YA KWANZA "UMENIITA" NDANI YA VCCT,MBEZI BEACH A TAR 28/04/2013!!

SHALOM!
KWA WALE WASOMAJI WA BLOG HII NA WADAU WA MADHABAHU HII YA MTANDAONI,NATUMIA NAFASI KUMTAMBULISHA KWENU KIJANA MPOLE NA MTARATIBU SANA AITWAYE "PAUL CLEMENT", HUYU NI MMOJA WA WAIMBAJI WA KUNDI LA "GLORIOUS WORSHIP TEAM" AMBAYE ZAMANI PIA ALIKUWA "GLORIOUS CELEBRATION"
KIJANA HUYU AMEVUMA SANA NA WIMBO WA "UMENIFANYA IBADA" WA KUNDI HILO,SASA PAMOJA NA KUWA KATIKA KUNDI,SASA AMEKAMILISHA KUREKODI ALBUM YAKE BINAFSI INAYOKWENDA KWA JINA LA "UMENIITA"..KIJANA HUYU NI MMOJA KATI YA WAIMBAJI WACHACHE SANA WANAOWEZA SANA KUIMBA NYIMBO ZA KUABUDU,BASI JUMAPILI HII YA MWISHO WA MWEZI WA NNE,IMEMPENDEZA MUNGU NAE AWEKE WAKFU ALBUM YAKE HIYO NDANI YA HEMA LA VCCT CHINI YA MCHUNGAJI DK HURUMA NKONE KUANZIA SAA TISA MPAKA MUDA WA KUONDOKA!!
NJOO UMUUNGE MKONO KWA KULIPA KIINGILIO CHA 5000/+ AMA UKAE KITI MAALUM PAMOJA NA ZWADI YA CD KWA KULIPA 10,000/= NATUMAI WEWE NA YULE WOTE TUTAKUWEPO KUMUUNGA MKONO MTUMISHI HUYU WA MUNGU!!

"KAMA WEWE UNA MAONO NA UNATAMANI KUFIKA MBALI,BASI JIFUNZE KUWEKEZA KWENYE MAONO YA WENGINE"

MUNGU AKUBARIKI NA KARIBU SANA!!!!

Monday, April 8, 2013

JIFUNZE KULEA KULEA MWANAO KATIKA NAMNA INAYOPASA!!!!


HABARI NJEMA KWA WAZAZI NA WALEZI WOTE,HUU NI MWANGAZA WA KUWASIDIENI KUWALEA WATOTO KATIKA NAMNA INAYOPASA,MWALIMU ERASTO NGUMUO ALIPEWA MAONO HAYA YA KUANDIKA KUHUSU  MALEZI NA MAKUZI YA MTOTO,SASA KITABU KIMETOKA NA UNAPASWA UKIPATE UKIWA KAMA MZAZI AU MLEZI WA WATOTO!!
KWA UHITAJI AU SWALI LOLOTE TAFADHALI PIGA 0754262946

Thursday, April 4, 2013

TANZANIA GOSPEL SINGERS' BREAKFAST TO BE ON 06TH APRIL,2013!!!!

IKIWA WEWE NI MUIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI BINAFSI,KAMA KWAYA AU BAND,UMEREKODI AU BADO,UNAIMBA HIP HOP AU WORSHIP NA KAMA WEWE NI MSHIKA DAU MWENYE MAPENZI MEMA NA MUZIKI WA INJILI TANZANIA BASI HII INAKUHUSU SANA!!
BASI USIKOSE KUJUMUIKA NA WENZAKO!!!
KARIBU SANA SANA NA MUNGU AKUBARIKI!!!

Wednesday, April 3, 2013

Kutoka Madhabahuni>>>...."MJUE SANA MUNGU ILI UWE NA AMANI NA UPATE MAFANIKIO"(02)

SHALOM!
Ninatumai wote tu wazima na tumesherekea vyema sikukuu ya kumbukumbu ya kufa na kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo!
Jumapili hii hatukuwaletea somo toka madhabahuni,badala yake kuna somo kuhusu NGUVU YA KUFUFUKA KWAKE,ambalo utalisoma muda si murefu!

Leo nataka niendelee kidogo kuhusu KUMJUA MUNGU!!

Rejea somo la kwanza
http://gospelstandardbase.blogspot.com/2013/03/kutoka-madhabahunimjue-sana-mungu-ili.html


SASA ENDELEA!!

Nini maana ya KUMJUA MUNGU...TENA SANA?

Kumjua Mungu ni kufahamu zaidi kuhusu kwanini amekuumba,kusudi lako na anatarajia nini kwako...huwezi kujiuliza kwanini Mungu yupo ila unapaswa kujiuliza kwanini wewe upo,Mungu amekuandikia baraka nyingi sana ambazo utazipata tu ukifuata kila agizo akupalo....kumjua Mungu ni kujua neno lake,kushika amri zake,kuelewa hukumu zake,kufahamu kuhusu mamlaka yake na zaidi kujua nafasi yako katika yote hayo!!!
Ukisoma katika Kumb 28...Biblia inasema Itakuwa utapoyashika na kutunza na kufanya maagizo yangu yote baraka hizi zitaambatana nawe!!

Ukimjua Mungu utamfanya wa kwanza katika kila kitu ufanyacho na wala kamwe hutatamani ya duniani zaidi yake na ndio maana mahali pengine katika Mathayo akasema...Mtafuteni kwanza Mungu na haki yake yote na hayo mengine(ambayo mnayo) mtazidishiwa!!

SASA KWA KADRI UNAVYOMJUA MUNGU,NDIO UNAZIDI KUJUA SIRI NYINGI ZA MUNGU,NA HAPO BIBLIA INASEMA.....ILI UWE NA AMANI!

AMANI hii inayozungumziwa hapa sio utulivu kama ulimwengu huu,hapana! bali ni uhakika wa kipekee ukaao ndani ya moyo wa mwamini aupatao katika neno la Mungu pekee!!
Yesu alisema...Amani yangu nawapa, amani yangu nawaachieni,niwapavyo mimi si kama ulimwengu utoavyo! Maana yake ni kuwa amani hii nim zaidi ya amani ya ulimwengu...ni kama vile ulimwengu na sayansi ama ugunduzi unasema kutakuwa na janga ama tatizo fulani,lakini wewe ukisoma neno unagundua kuwa tatizo hilo halikutishi wala kukusumbua kwa kuwa wewe ni mtoto wa Mungu na unalindwa na Mungu na zaidi unayo mamlaka katika ulimwengu wa roho,na hivyo ukiwa na uhakika huo,utakua na amani tele hata kama ukiwa katkati ya watu wasio na amani hata kidogo!!

NA HAPO SASA MAANDIKO YANAMALIZIA KWA KUSEMA...NA NDIVYO MAFANIKIO YATAKAVYOKUJA!!

Mafanikio kibiblia sio mali wala pesa ama vitu vya kuonekana,bali ni baraka ya ukamilifu na utimilifu wa ndoto au mipango fulani aliyo nayo mtu. Afya njema,kukua kiroho,matumizi ya karama za rohoni,kujua kusudi,ulinzi na utulivu ni moja ya mafanikio makubwa sana,hayo magari na majumba huja tu maana ni matokeo ya mafanikio ya rohoni! Sasa shida moja ni kuwa watu wengi hukazia macho kwenye vitu na kusahau mmiliki wa vitu hivyo ambaye ni Mungu mwenyewe!!

KWA HIYO KUMJUA MUNGU NDIO UFUNGUO WA YOTE....KWANZA UNAPATA AMANI YA KUTOSHA NA UHAKIKA WA KILA KESHO NA JUU YA YOTE NDIO UNAYAONA MAFANIKIO MENGI MBELE YAKO!!

KUMBUKA;
Hutumtumikii Mungu au kuokoka ili tubarikiwe au tuwe matajiri,ila ukimtumikia Mungu kwa uaminifu Kufanikiwa na kubarikiwa hakuepukiki!!
BASI MUNGU ATUSAIDIE ILI TUONGEZE JUHUDI YA KUJUA ZAIDI KUHUSU MUNGU NA SIRI ZA NGUVU ZAKE,MAANA NDIPO ILIPO BARAKA YETU!
MUNGU AKUBARIKI,AMEN!


SOMO;
Na Mwl. Chavala,Fredy E.
+255 713 883 797

SADAKA NA DHANA YA UTOAJI (The concept of Giving and Offerings)



UTANGULIZI  :  MAANDIKO NA MISTARI YA KUSIMAMIA

Kumb 28: 1-14; “Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya dunia; na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata, usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako. Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani. Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako. Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga. Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa utokapo. Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako, kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.

Bwana ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubarikia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako. Bwana atakuweka uwe taifa takatifu kwake … na mataifa yote ya dunia watakuona umeitwa kwa jina la Bwana, nao watakuwa na hofu kwako. Bwana atakufanya uwe na wingi wa uheri, katika uzao wa tumbo lako … Bwana atakufunulia hazina yake nzuri … nawe utakopesha mataifa mengi, wala hutakopa wewe. Bwana atakufanya kuwa kichwa, wala si mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakaposikiza maagizo ya Bwana, Mungu wako ... kuyaangalia na kuyafanya; msipokengeuka … kwa lolote, kwenda mkono wa kuume wala kushoto…”

 Kumb 8:10-20; “Nawe utakula ushibe, utamshukuru Bwana, Mungu wako, kwa nchi nzuri aliyokupa. Jihadhari usije ukamsahau Bwana, Mungu wako, kwa kutozishika amri zake, na hukumu zake, na sheria zake, ninazokuamuru leo. Angalia, utakapokuwa umekula na kushiba, na kujenga nyumba nzuri, na kukaa ndani yake; na makundi yako ya ng’ombe na kondoo yatakapoongezeka, na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka, na kila kitu chako kitakapoongezeka; basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau Bwana, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa … Hapo usiseme moyoni mwako, nguvu zangu na uweza wa mkono wangu, ndio ulionipatia utajiri huo. Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake …”


...........ITAENDELEA!!!