Sunday, July 29, 2012

KUTOKA MADHABAHUNI...KKKT DAYOSISI YA KONDE,USHARIKA WA FOREST,MBEYA MJINI!

SERMON: MPENYO WAKO UNATEGEMEANA SANA NA MWITIKIO WAKO!
                 (YOUR BREAKTHROUGH DEPEND ON YOUR RESPONCE)

                      Na Mchungaji MATHEW J. SASALI

Leo siku nzuri aliyoifanya Bwana,nimefanikiwa kuhudhuria ibaada ya kilutheri katika usharika wa Forest,Mbeya ambako leo ilikuwa sikukuu ya Vijana katika kanisa hilo,na mimi kama mmoja wa Waalikwa niliyehudhuria ibaada pamoja na Tamasha la kumsifu na kumwabudu Mungu!
Mchungaji Mathew Sasali ambae ni Manager wa Ushindi FM radio ndio alikuwa mchungaji mwalikwa na mnenaji wa leo, ambaye leo ametulisha neno hilo la Mungu!!


....Kumb 28:1->>
Itakuwa utakapoyashika,kutunza na kuyafanya maagizo ya Mungu yote,baraka hizi zitaambatana nawe...utabarikiwa......


.....Kumb 28:15->>
Na utakaposhindwa kutenda sawasawa na hivi nikuagizavyo,laana hii itaambatana nawe....


Maisha yetu ya kila siku yanategemea sana na vile ambavyo tunaitikia mambo yale yanayokuja mbele yetu,kubarikiwa au kulaaniwa kunatokana na sisi wenyewe na sio shetani,ni dhahiri kuwa watu wengi wanapendwa sana kubarikiwa ila hawapendi kuwa na uhusiano na huyo mtoa baraka!!


Wengi hudhani baraka huja kwa kuwekewa mikono au kuombewa na ndio maana hawachi kutanga tanga huku na kule wakitafuta baraka na kuacha baraka ambazo zinawazunguka.


Sasas leo nataka tuone msingi wa baraka na mpenyo katika maisha yetu!


MPENYO KATIKA MAISHA YETU UNATEGEMEA SANA JINSI TUNAVYOITIKIA KWA


              A.NENO LA MUNGU
Ni namna gani unatii na kulifuata Neno la Mungu?
Ni mara ngapi neno limekwambia fanya hivi na wewe ukafanya vile?
Ni dhahiri kuwa imani yetu huja kwa njia ya neno na imani hiyo haiwi dhahiri mpaka matendo yaonekane wazi...Kwa mfano katika Biblia kuna mifano ya watu wengi sana ambao walitii neno la Mungu na wakapata mipenyo katika maisha yao,naomba nimseme mmoja tu na huyu ni Jemedali wa Vita NAAMANI aliyekuwa na ukoma; alipewa wito na mjakazi tu kuwa katika nchi yao(yule mjakazi) yupo mtu anayeweza kuleta majibu kwa shida yake....tunaona katika maandiko kuwa jemedali huyo aliitikia na akaenda mpaka nchi ile kumwona mtumishi wa Mungu huyo...UNAFIKIRI NI WATU WA NGAPI WENYE VYEO NA HADHI ZA JUU WANAWEZA KUTII NENO LA WATU WALIO CHINI YAO???
Na alipofika huko mtumishi yule wa Mungu hakufanya lolote lile ila alimwambia nenda kajichonvye mara 7 ndani ya mto Yordani basi....kikawaida yule jemedali alihisi kudharauliwa na akataka kugoma kufanya hivyo lakini wasaidizi wake wakamwambia..kwani ukifanya hivyo utapungua nini? na vipi kama angekwambia jambo kubwa usingelifanya?...basi Jemedali alitii neno lile na akafanya kama mtumishi alivyosema na akawa mzima hata leo...kama huamini tukifika mbinguni nikumbushe tumtafute nikuonyeshe!!!


UNAYO NAFASI KUBWA SANA YA KUPATA CHOCHOTE AMBACHO BWANA ANATAKA UPATE LAKINI,HAKIKISHA UNAITIKIA KILA NENO LA MUNGU LINAKUJA MOYONI WAKO!!!


     B. KWA WATU
Mpenyo wako pia unategemea sana jinsi unavyoitikia miito mbalimbali ya watu, Je ni mara ngapi umepata wageni na ukashindwa kuwakirimu ipasavyo? ni mara ngapi unapata wageni lakini umekuwa ukiwapuuzia?
Jinsi unavyokuza uhusiano na kutunza urafiki na kutokuchoka kutenda wema kwa watu mbalimbali wajao maishani mwako ndio unavyojitengenezea mpenyo wako wa kesho....kwa mfano tu huo wa hapo juu unaona jinsi ambavyo Naamani aliitikia wito wa wajakazi wake,lakini pia kuna wakati Ibrahimu alipokea wagen watatu na akawakirimiia sana na wale ndio wakamwambia majira kama haya mwaka ujao mkeo atakuwa na mtoto..
ANGALIA NI WATU WANGAPI UMEWAPOTEZA KWENYE MTANDAO WAKO WA WATU WA MUHIMU NA MARAFIKI!!!


      C.KWA FURSA MBALIMBALI ZINAZOTOKEA KATIKA MAISHA YAKO
Unajua kama daudi hakuitwa kumuua Goliathi lakini aliposikia matusi kwa Mungu wake,akaona hii si nafasi ya kuikosa,hivyo akajitokeza bila kujali vipingamizi vya ndugu na umri wake na akasema yeye anaweza kumuua Goliathi na akafanya hivyo na akawa mfalme!!


HIVYO NDIVYO ILIVYO HATA KWAKO,UPATAPO NAFASI HADIMU ITUMIE VEMA YAMKINI NDIO MPENYO WAKO...IWE KWENYE BIASHARA,KAZI,MAISHA,SHULE NA MENGINE KADHA WA KADHA!!!


Ahsanteni sana kwa kushiriki nasi katika neno hili na MUNGU AWABARIKINI NYOTE MNAPOOENDELEA KUYATAFAKARI MANENO HAYA NA KUYATENDEA KAZI,AMEN!!!



VICTORY CHRISTIAN CENTRE TEBERNACLE WAMSHUKURU MUNGU NDANI YA HEMA LAO LA IBAADA!!


                                                    Dr. Rev. Huruma Nkone Ndani Ya Ibada
Kanisa la VCCT lililo chini ya Rev. Dr. Huruma Nkone siku ya Jumapili ya tarehe 29 July, 2012 wamefanya Ibada ya Shukrani ndani ya Hema Mpya Ya Kisasa ambayo imeagizwa Kutoka South Africa maalum kwa Ajili Ya Ibada.

Hema Hiyo Ya Kisasa yenye uwezo wa Kuchukua Watu takribani 1000 kwa Mara Moja imefungwa katika Kiwanja Cha Kanisa hilo kilicho maeneo ya Mbezi Beach Kawe ambapo Kwa maelezo ya Dr. Huruma Nkone Hema hiyo ni ya Muda Kabla Kanisa halijaanza Ujenzi wa Kanisa Kubwa la Kisasa ambalo litaitwa VCCS-- Victory Christian Centre Sanctuary.
                                Tabernacle Inavyoonekana Kwa Nje, Hapa Watu wakianza Kufika 


Kwa Karibu zaidi

Ibada ya Jana ambayo ilikuwa Maalum kwa ajili ya Kumshukuru Mungu kwa kuwafikisha hatua hiyo ilifanyika ndani ya Hema hiyo Ya Kisasa. Ndani Ya Kanisa hilo,  Kanisa Zima zileweka Zuria la Kisasa lenye Kunyonya Mawimbi Ya Sauti Kwa ajili Ya Vyombo Vya Muziki kwa ajili ya Kuzuia Mwangwi, Ndani ya Hema hiyo kimefungwa Chomo Maalum Cha Kudhibiti Sauti Ili Sauti Isisumbue Majirani ( Sound Proof), Ndani Ya Hema Hilo Limezunguzwa na AC, Viyoyozi Vya Kisasa kwa ajili ya Kuhifadhi ubaridi wakati wa Ibada na Kuondoa Joto, Milango Ya Kanisa hilo ambayo inategemewa Kuwekwa Mwanzoni Mwa mwezi wa 8 ni Milango Ile Maalum "Automatic Doors" ambapo zitakuwa ikifunguka yenyewe Kadri Washirika Watakavyokuwa Wakiingia, mbali na hayo Sound System iliyofungwa ni madhubuti kwa ajili ya hema hiyo.
Hapa Vijana wakifanya Set Up Ya Venue kwa ajili ya Ibada Viti Vyekundu Ni Maalum kwa Ajili ya Hema.
                                    Carpet Maalum kwa ajili ya Kuzia Mwangwi Wa Sauti
                                                                        Ndani Ya Hema

Mzee Kiongozi Wa Kanisa la VCCT Dr. Eda Wandwi akiongea siku Ya Jana Katika Ibada hiyo amesema Kanisa lina Maono Ya Kununua Mabasi yatakayokuwa Yakiwachukua Washirika wa Kanisa Hilo Katika Vituo Maalum na Kuwapeleka Kanisani hapo Kila siku Ya Ibada.

Kanisa la VCCT ambalo liko chini ya Dr. Huruma Nkone, asilimia 60 ya Washirika Wa kanisa Hilo ni Wanafunzi, na Asilimila 80-85 Ya Washirika ni Vijana. Kati Ya Vitu ambavyo Dr. Huruma Nkone ame invest katika Kanisa hilo ni
                                                The Rivers Of Joy Wakienda Sawa

1. "Quality"---- Katika hili Designing Ya Kanisa aliibuni Pastor Mwenyewe, Events za Kanisa kama Campus  Night, Soul Breakfast, Open Mic Open heart na Zingine ni Za Kiwango Kikubwa.
                                                 Pastor Huruma and Pastor Joyce Nkone

2. Raising People's Talents---- Dr. Huruma Nkone amejaaliwa Karama ya Kugundua, Kulea na Kuendeleza Talents Za Watu, The Praise Team, Ushers Organisation, Mcz, teachings, Singing unless mtu hajataka Kutumika lakini yeyote aliye tayari Kutumika Mlango Uko Wazi. Kwa Sasa imeanzishwa Praise Team (Rivers Of Joy Junior) ambayo hii ita raise Praise and Worship Leaders Miaka 10 Ijayo ambao Kwa sasa wako katika professional teachings.
                                                                     Kitu Sebeneeeee
3. PFW---Prayer, Fasting and Word Of God---- Ni Lazima Kila Mwezi  Wiki ya Kwanza Utaratibu wa Kanisa Washirika Kufunga na Kuomba Kama Kanisa, na Kuna Maombi Alfajiri, Mchana na jioni, Kila Mwanzo Wa Mwezi Wiki ya Kwanza ni YA Mungu. Washirika Wamegawiwa katika Vikundi Mbalimbali wanakokaa, Vijana, Wanawake, Wanafunzi Kila Jumamosi Ya Mwisho wa Mwezi, Wana taalum kila Mwanzo Wa Mwezi Jumapili, hakuna Kada mbayo imeachwa bila watu wa aina hiyo Kukutana Kwa ajili ya kujifunza Neno la Mungu.
                      ndani ya Ibada Kukawa kuna dakika 10 za Ku Network na Kusalimiana

Kwa Mawasiliano ya Mtandao....www.vcc.or.tz kwenye facebook Page ya Kanisa inaitwa,"Victory Christian Centre (VCC)", Page ya Vijana Inaitwa "The Bridge Youth Ministry" na Page Ya Wanafunzi inaitwa "Soul Breakfast"
 Juu kwa Nyuma ni Amani Kapama Mpiga drums, Kwenye Mic ni Sarah Shilla ndani ya Praise Team
 Mtumishi Wa Mungu Rev. Dr. Huruma Nkone akiwa Kwenye Prayers Kwa Kumshukuru Mungu.
                                            PAPAA THE BLOGGER.....   Full Technology ndani ya Kanisa.
                                                             Worship Moment
 Professional Sound Engineer and Songs Writer Raphael akiwa Kikazi Zaidi.
 Pastor akiteta Jambo ndani ya Ibada ndani ya dakika Kumi za Ku Network.
Jana Mise alifunika sana na Hii Kitu Saxerphone, Kuna Shule maalum inaanza Mwezi huu kwa ajili ya kufundisha kupiga hii kitu.


The Praise Team Rivers Of Joy.......


HABARI HII INAKUJA KWENU KWA HISANI KUBWA YA PAPAA THE BLOGGER!!!

Monday, July 16, 2012

WOMEN OF VIRTUE ANNUAL CONFERENCE (WHEN WOMEN WORSHIP)


RIGHTEOUS INVASION OF TRUTH (R.I.O.T.) brings to you The Women of Virtue Annual Conference - When Women Worship, which is to be held on 16-20 July, 2012 at the Russian Cultural Centre in Dar es Salaam from 6pm-9pm.

The Conference will be graced by powerful speakers; Apostle Emmanuel Tumwidike, Minister Isaac Mallonga and Pastor Irene Musokwa. Powerful worship experiences led by Pastor Delicia Roberson and the Doorkeepers. The R.I.O.T. Dancers and single artistes, Minza and Grace Mwakasendile, will minister as well.

As it dawned on Queen Esther that she was raised into power at an appointed time for the deliverance of her people, this prophetic conference will unearth a timely RHEMA word for women to rise into their positions in their context. Families, companies, governments and the whole world is waiting for women who know the power of worship and walk in that knowledge.

Just as the children of Issachar knew the times and seasons, women are called for such a time as this to know the times and seasons to deliver what God has placed in them for this generation.

"Yet who knows whether you have come to the kingdom for such a time as this?" Esther 4:14


SOURCE; http://www.facebook.com/events/160910634045364/